Msaada wa kupata software ya mahadhurio ya wafanyakazi.

Msaada wa kupata software ya mahadhurio ya wafanyakazi.

TEMBO WANGU

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2014
Posts
930
Reaction score
1,297
Wakuu, nauliza naweza kupata software inaonyesha mfanyakazi ameingia saa ngapi, ametoka saa ngapi, na hiyo taarifa imfikie mwajiri mda huo huo, iwe kwa njia ya sms au email, msaada wadau.
 
software zipo nyingi, hiyo waliyosema biometric machine ndio rahisi maana kila mfanyakazi utampa kadi na kila akiingia mlangoni mashine itasoma kadi yake na muda anaoingia.

pia ziko za kutengeneza kuwa kila mfanyakazi akija lazima alogin kwenye komputa yake na messaji kwenda kwa bosi.

pia hata cctv camera zinaweza kufanya kazi hiyo kwa kupitia muda kila mtu anaingia getini.
 
Si kazini tunatumia daftari. Ukifika unaandika jina sahihi na muda wa kuingia. Ikija hii machine ya Biometric security machine nahisi watu watalia sana. Maana mtu anafika saa 4 asubuhi anaandika saa 1
 
Si kazini tunatumia daftari. Ukifika unaandika jina sahihi na muda wa kuingia. Ikija hii machine ya Biometric security machine nahisi watu watalia sana. Maana mtu anafika saa 4 asubuhi anaandika saa 1

Bila shaka itakuwa ofis fulani fulani za serikali hasa Halmashauri.
 
Biometric itafaa sana maana kila uingiapo ma kutoka lazima uweke kidole chako
 
Wakuu, nauliza naweza kupata software inaonyesha mfanyakazi ameingia saa ngapi, ametoka saa ngapi, na hiyo taarifa imfikie mwajiri mda huo huo, iwe kwa njia ya sms au email, msaada wadau.

Tatizo lako ni dogo,sijajua kwani kuna gharama kama mtaweza kuimudu tuwasiliane mapema nikusaidie.Kwa hiyo issue yako unahitaji biometric system(finger scan inatosha for your case).Hii itakupa muda wa kuingia,kutoka,overtime mtu alizofanya kazi,report ya wachelewaji kazini,report ya wanaowahi kutoka kazini etc.Pia inaondoa ghost workers(wafanyakzazi hewa),it is expensive somehow lakini in a long run inalipa so if you are serious let me know and see how I can help you.
 
Back
Top Bottom