Msaada wa kupata ajira ya kueleweka

Nkosilorch

Member
Joined
May 4, 2024
Posts
23
Reaction score
25
Habari za muda huu wakuu, mimi ni mhitimu wa shahada ya awali ya Bima na udhibiti viashiria hatarishi (Bachelor in insurance and risk management) 2022, kiukweli nashukuru sana tangu nimalize chuo sijawahi Kaa bila kazi nilipomaliza mwaka 2022 ni moja ya wanafunzi tuliofaulu vizuri na kuchukuliwa na bank moja kubwa hapa Nchini tulipewa mkataba wa mwaka mmoja kama internship ya insurance and risk management officer.

Duty tulizokuwa tunafanya pale kwenye department ya risk ni, To identify different risks in every department, to recommend method of risk identification, to prepare periodic reports of risk management internally and externally, hizi ni baadhi ya duties tu lakini zipo nyingi sana.

Tulipiga kazi pale kwa mwaka 2022-2023 ilipofika December mwaka 2023 wakatuambia inabidi waje wengine tena kuendana na sera ya serikali, japo pale bank hawakutaka tuondoke ila malipo yali stop kidogo.

Kama zali tu January 2024 nilipigiwa simu naambiwa namba Yako tumepewa chuoni Kuna watu tulikua tunawahitaji huyo mtu anapatikana kwenye Taasisi serikali ambapo alituambia twende tukaripoti kwa ajili ya kuanza intern tena ya insurance and risk officers.

Nimepiga intern pale kuanzia January 2024 mpaka sasa ambapo wametuambia kutokana na sera ya serikali, intern ni mwaka mmoja mmoja inabidi waje wengine tena kwaiyo kwa sasa nipo dilemma japo hapa wametuambia tusiondoke tuwepo tu hapa tutakua tunapata chochote kwa mwisho wa mwezi.

Kuhusu utumishi nimefanya oral mbili za tutorial assistant kwakweli sijafanikiwa kupata kazi mpaka sasa na piah written zingine mbili sijafika oral. Hizo oral mbili tuliambiwa tupo database ila mi siamini mpaka sasa na kada yangu kutangazwa utumishi ni mara chache mno.

Nimekuja mbele yenu kama Kuna mtu anaweza kunishika mkono niweze kupata sehemu ya kueleweka kutokana na kada yangu nitashukuru sana maana age naona inasogea.

Kwa mawasiliano zaidi ni
0719 666 136

Nashukuru sana.
 
Hiyo bank naona kama inawafanya wahitimu manamba wao, huo utaratibu wa kuchukua wahitimu kutoka chuo wanawatumikisha Kwa faida zao baada ya mwaka wanawake dump wanachukua wengine uko kisheria?
 
Hiyo bank naona kama inawafanya wahitimu manamba wao, huo utaratibu wa kuchukua wahitimu kutoka chuo wanawatumikisha Kwa faida zao baada ya mwaka wanawake dump wanachukua wengine uko kisheria?
Cha kushangaza wale jamaa wanaenda wanaomba majina ya wenye ufaulu mkubwa kumbe wanaenda kuwatumikisha baada ya muda Wanawa dump tena.
 
Hiyo bank naona kama inawafanya wahitimu manamba wao, huo utaratibu wa kuchukua wahitimu kutoka chuo wanawatumikisha Kwa faida zao baada ya mwaka wanawake dump wanachukua wengine uko kisheria?
Ni kama wamewachukua kwa 'field' tu; pia kwa ulimwengu wa sasa si rahisi kupata sehemu ya kufanyia 'field'​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…