Msaada wa kibiashara

Mkuu kakaye utatambua faida au hasara achilia mbali mtaji ambao unajulikana ulipokua unaanza biashara ulianza na kiasi gani..kwa urahisi ni kwamba unatakiwa uitengeneze ya mwezi mmoja mmoja kwa kuwa kuna gharama zingine zinalipwa kwa mwezi kama umeme,maji na wewe mwenyewe kama mshahara unapata au umeajiri na madeni ya mwezi husika...unajumlisha vyote hivyo kama gharama za uendeshaji na unajumlisha kile ulichokua unauza kila siku kwa muda wa mwezi mzima utatoa hizo gharama za mwezi mzima utapata faida ya mwezi mzima....
 
Asante isanga family ila fafanua kwa wiki nataka nimuelimishe mke wangu
 
Weka kila kitu namaanisha kila senti inayoingia na kutoka kwenye maandishi hapo utakuwa na uwezo wa kucalculate faida na hasara kiurahisi sana...faida ni ile pesa inahobaki baada ya kutoa matumizi yako yote ikiwemo mtaji na matumizi kama kulipa wafanyakazi,kodi,umeme,taka na vyote vinavyohusiana na hiyo biashara.
 
Back
Top Bottom