Naomba kufahamu namna ya kupima ujazo wa maji katika tank, nafikiria kujenga karo lenye upana wa futi 3 na urefu wa futi 4, kimo futi 5. (Nikumbusheni formula)
Ujazo ni :
Urefu * Upana * Kimo AU ENEO *KIMO.
Baada ya hapo kama ni maji, unaweza kuzidisha kwa 28.32 ili upate Lita.
Kwa mfano : 4*3*5= 60 cubic feet. Ambazo ukizidisha kwa 28.32, yaani:
60*28.32= LITA 1699.2
Naomba kuwasilisha.