Msaada: Tutoeni ushamba mimi na mke wangu

Msaada: Tutoeni ushamba mimi na mke wangu

Bwana Chiniko

Member
Joined
Jul 18, 2016
Posts
20
Reaction score
9
Heshima kwenu wakubwa zangu wa jukwaa hili na marahaba kwa wale wote niliowatangulia kuliona jua.

Mimi na mke wangu tumefunga ndoa takatifu wiki moja iliyopita, hivyo tukapanga tukatembee nchini Afrika Kusini.

Maana tangu kuzaliwa kwetu hatujawahi fika katika nchi hiyo na sio siri wote tunahamu ya kwenda kutoa ushamba.

Ifahamike kwamba sio mimi wala mke wangu aliyewahi kupanda ndege tangu kuzaliwa kwetu. Nahitaji kuelekezwa taratibu za ukataji tiketi, kupata passport ya kusafiria na namna ya kuingia airport kupanda chombo kuelekea South Afrika. Ili tusionekane washamba wa mambo ya kidigital.

Nb: Afrika Kusini nina ndugu, jamaa na marafiki wengi wanaishi huko, hivyo sehemu yakufikia sio shida.

Nawasilisha kwenu.
 
ahaaaaa passport za kusafiria mnazo? hili ndo LA muhimu kwanza
 
Wenyewe wanajua nafahamu taratibu zote hizo, isitoshe nikiwambia utani utakuwa mwingi sana, maana nawaelewa hawa jamaa zangu, itakuwa wimbo wa Taifa.
umesema una ndugu na jamaa wengi sana...Ina maana waote watakudhihaki?
 
Nenda ofisi za Fastjet watakuelekeza mkuu. Huku utaishiwa kupondwa
 
Heshima kwenu wakubwa zangu wa jukwaa hill na marahaba kwa wale wote niliowatangulia kuliona jua.

Mimi na mke wangu tumefunga ndoa takatifu wiki moja iliyopita, hivyo tukapanga tukatembee nchini Afrika kusini.

Maana tangu kuzaliwa kwetu hatujawahi fika katika nchi hiyo na sio siri wote tunahamu ya kwenda kutoa ushamba.

Ifahamike kwamba sio mimi wala mke wangu aliyewahi kupanda ndege tangu kuzaliwa kwetu.

Nahitaji kuelekezwa taratibu za ukataji tiketi, kupata passport ya kusafiria na namna ya kuingia airport kupanda chombo kuelekea SA.

Ili tusionekane washamba wa mambo ya kidigital.

Nb: Afrika kusini nina ndugu, jamaa na marafiki wengi wanaishi huko, hivyo sehemu yakufikia sio shida.

Nawasilisha kwenu.
Angalia usisafiri muda wa kazi , utakamatwa na policcm .
 
Heshima kwenu wakubwa zangu wa jukwaa hill na marahaba kwa wale wote niliowatangulia kuliona jua.

Mimi na mke wangu tumefunga ndoa takatifu wiki moja iliyopita, hivyo tukapanga tukatembee nchini Afrika kusini.

Maana tangu kuzaliwa kwetu hatujawahi fika katika nchi hiyo na sio siri wote tunahamu ya kwenda kutoa ushamba.

Ifahamike kwamba sio mimi wala mke wangu aliyewahi kupanda ndege tangu kuzaliwa kwetu.

Nahitaji kuelekezwa taratibu za ukataji tiketi, kupata passport ya kusafiria na namna ya kuingia airport kupanda chombo kuelekea SA.

Ili tusionekane washamba wa mambo ya kidigital.

Nb: Afrika kusini nina ndugu, jamaa na marafiki wengi wanaishi huko, hivyo sehemu yakufikia sio shida.

Nawasilisha kwenu.
Hakikisha mko na Pasport valid, inategemea unakata ticket ndege gan ila taratibu za airport ni zile zile kikubwa ubebe mzigo kulingana na kilo utazopewa kwenye ticket maana ukizidisha hapo huo upepo utaotolewa hadi mood itaisha, kuhusu taratibu sasa ukishafika airport kila kitu utapewa maelezo kikubwa kuwa makini na usijitie ujuaji sana ukiona mazingira huyaelewi kaa mahali anza kusoma vibao kishkaji ramani zikigoma unaweza tu kuuliza kiakili nafkiri wewe ni mjanja.
NB: Epuka kuweka mziki mkubwa kweny headphon utaokufanya usisikie matangazo ya spika za airport unaweza jikuta ndege imeondoka wewe bado upo airport.
Safari njema wewe na mama muombeni pia Mungu sana maisha ya ndoa official yanajulikana
 
Nenda Ubungo Stand kaulie basi ya machinga
 
Nenda ofisi za uhamiaji mahali ulipo Jaza fomu na uambatanishe yote yanayohitajika ili mpate passport,baada ya hapo nenda ofisi za ndege utakayopenda kusafiri nayo ili upate tiketi zenu. Mambo mengine utayajua tu ukiwa safarini
 
Hivi kwenda south visa haina umuhimu enheee? Na zile chanjo sijui za homa ya manjano na pepopunda kule hawahitaji?
 
Usikubali ukifka Airport mtu akukabidhi begi umshikie,mara nyingi huwa ni drugs
 
Back
Top Bottom