msaada tutani

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,845
2,667
wadau ningependa mnijuze na ikiwezekana kupata tiba ya huyu mzazi wangu.

Ni kwamba, aliwahi kupata ajali miaka mingi iliyopita na kuumia mguu (hii sehemu ambayo unaweza kupigia mpira) Kilichifanyika, alitolewa ngozi kiasi sehemu ya mwili ikawekwa pale mguuni.

Sasa miaka hii ya uzeeni, mguu ulikwaruzika na ile ngozi inakuwa ngumu kushikana na kufunga, so kidonda hakiponi na ni muda sasa. nahitaji sana apone lakini pamoja na juhudi za hospitali bado panasumbua. hopefully kuna mwana JF atakayekuwa na suluhu katika hili.

Naombeni mawazo yenu
 
wadau ningependa mnijuze na ikiwezekana kupata tiba ya huyu mzazi wangu. ni kwamba, aliwahi kupata ajali miaka mingi iliyopita na kuumia mguu (hii sehemu ambayo unaweza kupigia mpira) Kilichifanyika, alitolewa ngozi kiasi sehemu ya mwili ikawekwa pale mguuni. sasa miaka hii ya uzeeni, mguu ulikwaruzika na ile ngozi inakuwa ngumu kushikana na kufunga, so kidonda hakiponi na ni muda sasa. nahitaji sana apone lakini pamoja na juhudi za hospitali bado panasumbua. hopefully kuna mwana JF atakayekuwa na suluhu katika hili. naombeni mawazo yenu
Pole, inafaa umpeleke hospitali ya kueleweka. Vidonda vidonda kwa watu wazima yaweza kuwa chochote- hata kansa, ama kutokupona shauri ya magonjwa kama kisukari. Anaishi wapi?
 
Pole, inafaa umpeleke hospitali ya kueleweka. Vidonda vidonda kwa watu wazima yaweza kuwa chochote- hata kansa, ama kutokupona shauri ya magonjwa kama kisukari. Anaishi wapi?

Safiri ukamwone Doctor Bake pale Burere Kibaha
 
Nashukuru kwa mchango wenu. bila ya shaka hana sukari na pia anasema hamna maumivi ya ziada sana zaidi ya eneo la mguu. kumbuka kuwa hiyo sehemu ya kidonda ina ngozi nyepesi sana. sio ngozi yake asilia kwani ilipandikizwa hapo mguuni tu. yuko hapahapa bongo- Tabata
 
Nashukuru kwa mchango wenu. bila ya shaka hana sukari na pia anasema hamna maumivi ya ziada sana zaidi ya eneo la mguu. kumbuka kuwa hiyo sehemu ya kidonda ina ngozi nyepesi sana. sio ngozi yake asilia kwani ilipandikizwa hapo mguuni tu. yuko hapahapa bongo- Tabata
kama yuko tabata, mpeleke muhimbili. ni-pm kama wataka contact persons.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom