msaada tafadhali - polisi bana

msaada tafadhali - polisi bana

Asante nash.sasa namsubiria apige tena simu nimuulize maswali ya kipolisi na yeye atajuta..kesi nifungue mimi afu anisumbue yeye hawa mapolisi njaa sijui vipi..ubarikiwe.

Inavyoelekea noella unaonekana muoga fulani hivi halafu unazo unazo na ndo maana polisi huyo anakusumbua.. Anatumia udhaifu wako wa uoga na kutojua sheria.. Kitu rahisi cha kufanya.. Mtafute mwanaume mwenye composure na anaejiamini.. Kisha mpigie wewe huyo askari ili muonane halafu umuulize mbele ya jamaa kuhusu suala la kufuta kesi.. Trust me inafanya kazi hii ruse kuliko unavyofikiria..

cc: Paloma..
 
Last edited by a moderator:
Hao kama s polisi wa kituo cha Mabatini, Kijitonyama ... sijui?!Coz mimi pia nilivunjiwa, kufika kwao mpelelezi akanpgia nimuwezeshe hela ya kufanyia upelelezi .... Sht, sikurudi tena!
 
Mod, JF imeingiliwa na members ambao hawapo serious, na hii hali ikiruhusiwa iendelee itaathiri heshima ya genuine members na heshima ya forum. Mtu akiuliza au kutaka ushauri tunastahili kumsaidia/kumpa jibu. kama mtu anaona hoja haina mashiko, ni bora kutokuchangia kuliko kukatishana tamaa na maudhi juu yake. Nawashukuru mliompa ushauri muliza swali.
 
noella, Paloma et al...

Sijui nisemeje, hali ya rushwa (kuomba/kulazimisha/kutengeneza mazingira ya) Tanzania sio jambo geni. Kila mtu aliyepewa wadhifa fulani anataka kutumia nafasi ile kujinufaisha - hata kwa lazima ikibidi.

Hali hii ipo wizara ya ardhi, bandari, TRA, hospitalini na karibu kila sekta hapa nchini. Si juzi tu lara 1 ametumabia ishu kama hii ya rushwa?

Polisi kwa upande wao wamekuwa wahanga wakubwa wa malalamiko haya hasa kwa kuwa wao wana-direct interaction na raia wengi kwa nyakati tofauti na katika matukio tofauti.

Na wao kama watumishi wengine wa nchi hii wameona na wao wachukue chao mapema kwa nafasi walizopewa. Ubaya wake sasa ni kutofanya upelelezi wowote bila kutolewa, kutochunguza tukio lolote lililoripotiwa bila kuona maslahi - ya kifedha- kwao, yani hawafanyi chochote ambacho there's nothing in it for them.

najua hapa si mahali pa kuanza kuelezea kwanini wanafanya hivyo na wala si wakati muafaka wa kuanza kuelezea nini kifanyike kuepusha jambo hili.

Ninachoweza kuwaeleza kama raia wema ni hiki, "Kuijua haki yao, kuijua sheria ni silaha kubwa kwako dhidi ya unyanyasaji wowote." Rushwa tuliiotesha wenyewe, tuliipalilia wenyewe na tunaikuza wenyewe. Hivyo basi hata kuitokomeza ni jukumu letu wenyewe.

Tusiwe warahisi kutafuta solution za mkato hasa pale tunapojikuta mikononi mwa polisi. Tambua haki zako. Kama kweli uko kwenye kosa basi isiwe ndo wakati wa kumtoa buku ili usepe fasta! nenda kalipe fine kituoni.

Dada noella, situation yako ni ngumu mtu kuweza kukushauri kwani hujaieleza kinagaubaga. Bado ninabaki na maswali mengi kichwani.
- uhusiano wako na huyo akutishiaye maisha?
- alikutishia kwa maneno, simu, sms au?
- kwa nini umeamua kufunga kesi?
-nk nk...
 
Last edited by a moderator:
noella, Paloma et al...


.

Ninachoweza kuwaeleza kama raia wema ni hiki, "Kuijua haki yao, kuijua sheria ni silaha kubwa kwako dhidi ya unyanyasaji wowote." Rushwa tuliiotesha wenyewe, tuliipalilia wenyewe na tunaikuza wenyewe. Hivyo basi hata kuitokomeza ni jukumu letu wenyewe.

Tusiwe warahisi kutafuta solution za mkato hasa pale tunapojikuta mikononi mwa polisi. Tambua haki zako. Kama kweli uko kwenye kosa basi isiwe ndo wakati wa kumtoa buku ili usepe fasta! nenda kalipe fine kituoni.

...


kwa taifa letu hili....watu wengi hawajui sheria na haki zao za msingi pindi wanapokabiliana na polisi. bahati mbaya polisi wanatumia mwanya huo kuwakandamiza raia hao simply bse hawajui kitu.

AU mie sizijui wajibu za polisi?!?!? Mentor nirestishe wka dady basi anipe maelimu...........
 
Last edited by a moderator:
Hao kama s polisi wa kituo cha Mabatini, Kijitonyama ... sijui?!Coz mimi pia nilivunjiwa, kufika kwao mpelelezi akanpgia nimuwezeshe hela ya kufanyia upelelezi .... Sht, sikurudi tena!

hahahhaha ulijuajeee.ndo haohao..kumbe ndo tabia yao ee.hawanipati ng'oo
 
noella, Paloma et al...



Dada noella, situation yako ni ngumu mtu kuweza kukushauri kwani hujaieleza kinagaubaga. Bado ninabaki na maswali mengi kichwani.
- uhusiano wako na huyo akutishiaye maisha?
- alikutishia kwa maneno, simu, sms au?
- kwa nini umeamua kufunga kesi?
-nk nk...

- alikuwa ni boyfriend wangu wa miaka mitano
- alinitishia kwa sms na maneno
- polisi ndo kanishauri aitwe aonywe mbele ya polisi na ndugu yake yoyote then tufunge kesi
 
kwa taifa letu hili....watu wengi hawajui sheria na haki zao za msingi pindi wanapokabiliana na polisi. bahati mbaya polisi wanatumia mwanya huo kuwakandamiza raia hao simply bse hawajui kitu.

AU mie sizijui wajibu za polisi?!?!? Mentor nirestishe wka dady basi anipe maelimu...........

Ka vp pumzika kwangu afu mi ntakuwa namuuliza on ur behalf muache daddy ale pensheni na mai waifu wake pliz!
 
- alikuwa ni boyfriend wangu wa miaka mitano
- alinitishia kwa sms na maneno
- polisi ndo kanishauri aitwe aonywe mbele ya polisi na ndugu yake yoyote then tufunge kesi

- Hili limeshafanyika? mbele ya nani?
 
- Hili limeshafanyika? mbele ya nani?

yani bado haijafanyika amenambia hivyo afu akanambia niandae hela kwa ajili ya kufunga hiyo kesi baada ya kutoa onyo ndo nikaingia humu nipate mwongozo,sijarudi bado, hii ishu kanambia jumanne juzi
 
yani bado haijafanyika amenambia hivyo afu akanambia niandae hela kwa ajili ya kufunga hiyo kesi baada ya kutoa onyo ndo nikaingia humu nipate mwongozo,sijarudi bado, hii ishu kanambia jumanne juzi

Basi mwite nduguyo (wa kiume) na huyo uliyemshitaki muende polisi hapo mkafunge kesi. Mkimaliza akikuitisha fedha ya kufunga kesi muambie akuandikie na risiti kabisa yenye force number yake.

Baba aliniambia askari wanaogopa kujulikana force nambaaaa...jaribu iyo!!!
 
Ka vp pumzika kwangu afu mi ntakuwa namuuliza on ur behalf muache daddy ale pensheni na mai waifu wake pliz!

thanks.
but ni speshel kwa ajili ya mshua wako tu!!! kama vipi tupotezee tu ntapata mwingine..........au nitaghairi!
 
ndio maana nilisema sipendi police

cc Mentor sosoliso Lyagwa saudari

Paloma, mimi sikuwatetea police kwa matendo yao mabaya, na wala sina urafiki wowote na police, sipendi uovu wa aina yeyote kwenye maisha yangu yote, ila naogopa sana kumchukia mtu yeyote kupita kiasi, yaani hadi mimi mwenyewe niumie kwa ajili hiyo, tuwe na kiasi katika yote hii inatusaidia katika maisha yetu binafsi, tunaambiwa tuwe na hasira lakini tusitende dhambi.

Hakika kuna mpolomoko mkubwa sana wa maadili sehemu za kazi na kwa police hata tafiti zinaonesha ya kwamba wao ni too much hasa kwenywe rushwa za aina zote yaani pesa, ngono nk. Inapotokea unakumbana nao kwenye area ambazo wewe binafsi hauko sure kama huyu dada mwenye thread ni better ukauliza hata kwenye jukwaa kama hili na hakika watu watatoa assistance ya kutosha ili kuepukana na kadhia ya hawa jamaa nna njaa zao.

Police wa Tanzania ni tatizo sana, nadhani na pia jilani zetu Kenya nao pia wako hivyo, mimi sipendi matendo yao.
 
Back
Top Bottom