JONASON
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 461
- 706
Ndugu zangu wanajamii forum naomba anayejua au mwenye access na mtu au kiumbe chochote mwenye kutoa utajiri ambaye ana mashart yoyote yasiyo husisha kuuwa au kutesa mtu mwingine au ndugu yako aniunganishe au tuwasiliane pm au hatakujiunga freemason bas anisaidie huko maana nimechoka na unasikini, dhiki na kudharauliwa..
Mimi ni kijana nimesoma mpaka level ya shahada ya kwanza nimemaliza sasa Nina miaka mitano toka nimemaliza nimeandika barua za maombi nyingi toka nimemaliza takriban kila siku nafanya maombi sio chini ya taasisi kumi mpaka saba nimeshaomba kujitolea ila ni chenga tupu nimejaribu kutafuta hata contact za matajir wakubwa nikaomba wanipe shavu hata kuuza duka ila hamna wote kimya na Mimi siangalii kiwango cha mshahara ili mradi niya mudu maisha nitoke nyumbani kwa wazee niweze hata kujitegemea maana chuoni nilikosa mkopo Wa serikali ikabidi wazee wauze vitu kadhaa niweze kusoma nije niwasaidie ila bado nimekua mzigo na mtaji hawana Wa kunipa na bado kuna madogo wanataka ada nimejitahidi kuchukua kila hatua nimezunguka interview nyingi nimejikuta namaliza nauli tu na Mimi ni mtu Wa dini nimefika hadi Tanganyika Pecker's kawe kwa Boniphace mwamposa nimewekewa mikono nikaombewa ila bado sana sana sasa kaka , Dada , wadogo na wazazi wanaona Mimi ni mtu Wa ajabu kwa vile sina muendelezo mzuri toka nimemaliza elimu yangu ya shahada japokua nasaidia suala la Kilimo na kupiga vibarua kupata fedha hata za kununulia mashati na suruali na moka za kuendea ktk usaili ila napoteza muelekeo napambana kwa njia ambazo sipati kitu na pia nilipitia JKT kwa mujibu Wa sheria hivyo nidhamu ipo nikiomba hata kazi za ulinzi sipati.
Basi ombi langu lilikuwa ni hilo wana jf wenzangu mnisaidie sisi sote ni ndugu na Mungu ni wetu ..NB: ushauri na maoni naruhusu ila usiniseme vibaya wala usiniongelee vibaya unitoe katika mood ..Nawasilisha