beleza
JF-Expert Member
- Sep 18, 2014
- 397
- 144
Kuna mdogo wangu wa kike (baba moja mama mmoja) aliolewa lakini katika ndoa ile familia yetu yote ilikataa kuwa pamoja na yeye kwa sababu mume wenyewe alikuwa haeleweki kwa tabia zake za kuoa na kuacha kila mahali. Hilo tulilijua baada ya kumchunguza na tutamwambia huyu mdogo wetu juu ya tabia ya huyo mwanaume lakini akasema yeey anamtaka hata kama ana tabia gani.
Poa baba na mama na familia yote ikamsusia na akaenda kwa mzee moja ndio akamuomba aende kwa baba ili apewe idhini amuozeshe yule mzee akafanya kama alivyomuomba na wakafanya ndoa yao ya aina yao. Sasa baada ya miaka kupita na kufanikiwa kupata watoto watatu na yule mume na kujenga nyumba yao hatimae yule mume kamuwacha na kamwambia asifike pale penye nyumba yao.
Poa mimi nikamwambia njoo nyumbani utulie kwa kweli akafika nyumbani na akatulia, sasa ni kama miezi minne ivi imepita. Sasa cha ajabu juzi nimepigiwa simu wanasema karudi kule kwenye nyumba yao na baada ya kufika kule na aliyekuwa mume wake kupata taarifa akampigia mtu wake wa karibu na kumwambia aondoke na haraka sana yeye hamtaki ata kumsikia.
Mimi nikaona ni sawa sababu siameshaachika tayari) tatizo huyu mdogo wangu anataka kukaa na watoto wake lakini huyo bwana alimwambia ukichukua watoto usiniulize kitu au nikiwachukuwa na wewe usiniulize kitu. Sasa na huyu mdogo sijui nimsaidieje kwa kweli.
Tatizo nalionalo, kwanza ni mbishi sana, kisha hataki ushauri wa mtu.
USHAURI WENU TAFADHALI
Poa baba na mama na familia yote ikamsusia na akaenda kwa mzee moja ndio akamuomba aende kwa baba ili apewe idhini amuozeshe yule mzee akafanya kama alivyomuomba na wakafanya ndoa yao ya aina yao. Sasa baada ya miaka kupita na kufanikiwa kupata watoto watatu na yule mume na kujenga nyumba yao hatimae yule mume kamuwacha na kamwambia asifike pale penye nyumba yao.
Poa mimi nikamwambia njoo nyumbani utulie kwa kweli akafika nyumbani na akatulia, sasa ni kama miezi minne ivi imepita. Sasa cha ajabu juzi nimepigiwa simu wanasema karudi kule kwenye nyumba yao na baada ya kufika kule na aliyekuwa mume wake kupata taarifa akampigia mtu wake wa karibu na kumwambia aondoke na haraka sana yeye hamtaki ata kumsikia.
Mimi nikaona ni sawa sababu siameshaachika tayari) tatizo huyu mdogo wangu anataka kukaa na watoto wake lakini huyo bwana alimwambia ukichukua watoto usiniulize kitu au nikiwachukuwa na wewe usiniulize kitu. Sasa na huyu mdogo sijui nimsaidieje kwa kweli.
Tatizo nalionalo, kwanza ni mbishi sana, kisha hataki ushauri wa mtu.
USHAURI WENU TAFADHALI