Msaada: Nina roho mbaya sana jamani

Msaada: Nina roho mbaya sana jamani

God'sBeliever

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2015
Posts
5,788
Reaction score
3,062
Kuna mda unafika najiona niko tofauti na binadamu wenzangu. Unaweza kuta tupo msibani, ajali au kwenye tukio la mauaji unakuta watu wote wako na huzuni ila mimi niko freshi na nina amani kabisa moyoni wala siwazi yani nachukulia ni jambo la kawaida tuu.

Hata wakati wa usiku wa manene huwa siogopi kutembea nje na hata kama hilo eneo lina mashetani au linahisiwa vibaya mimi napita tuu. Nina hasira za karibu sana na huwa nikigombana na mtu huwa sinaga time nae tena na hata tukija kupatana ni baada ya miaka mingi sana. Hali hii imenifanya kuwa mtu wa visasi na huwa sikubaligi kushindwa jambo kabisa, niko radhi nirudi nipambane na nishinde hilo jambo.

Huwaga najipenda mwenyewe kwanza halafu ndio naangalia na wengine. Ndugu zangu hata wakifa mimi naona poa tuu na ninavyowaandikia hapa baba yangu ni marehemu na bado halinipi shida mimi naona kitu kidogo tuu.

Hata wazazi wangu nawachukuliwa kawaida tuu hata siwaogopi. Shuleni nimewahi kuwa na uadui na wale wababe wa shule na kwanza nilikua sinaga time nao. Kuna mmoja aliwahi kuniambia nina dharau mimi sikumjibu nikaendelea na mambo yangu. Kuna mmoja alinipiga mgongoni hiyo ndo ikawa safari hadi saivi natamani nikamchome kisu.

Mimi raha yangu ni kusikia watu nisiowapenda wamepata matatizo hata kufa kabisa. Mimi watu ninaowapenda ni wale wauaji na makatili waliowahi kutokea hapa duniani. Mimi sipendagi kuonewa kabisa ila nikiona mtu anaonewa ambae hana hatia huwaga nakasirika sana na sa nyingine kuokoa huyo mtu.

Nimekua sina mda sana na wanawake, wakiniletea za kuleta nawapiga chini naendelea na maisha yangu peke yangu, msichana yeyote akinisma vibaya mimi namfata nampiga makofi naondoka zangu maana mimi si mtu wa maneno.

Nimekua na kiburi mno hata ndugu zangu wanalitambua hili na hii imefanya baadhi ya watu wengi kuniogopa sana.

Sasa wakuu kama nilivyojielezea hapo nawezaje kuepukana na hali yangu hii niliyonayo?

Nawasilisha.
 
mbona umeshindwa kutumia jina lako halisi APA jf...anyway kiufupi una tatizo LA kisaikolojia lililotokana na malezi tangu ukiwa mdogo,unaweza kutafuta wataalamu wa saikolojia wakusaidie.
 
Hebu jaribu kujinyonga kwanza, ukifanikiwa basi wewe kweli una roho ngumu, ama kajaribu kulala makaburini usiku mzima, ukifanikiwa hilo tutajua wewe ni katili hasa. Tofauti na hapo inaelekea wewe una gubu tu na hupendi mafanikio ya wengine ndo maana huwezi kusamehe na unashangilia madhila ya wengine unaodai huwapendi.
 
Una pepo tena pepo la ukakamavu; wachawi na magaidi shetani huwavisha pepo hilo; hili pepo ukilitumia vizuri ni fursa! Lakini kiubidamu mrudie Mungu; Kwa mifano yako ni dhahiri kwamba huogopi chochote awe shetani wala Mungu huna mpango naye! Ila dalili sasa zinaonesha upo tayali kubadilika!
Kila LA kheri Kwa kupokea maisha mapya!
 
Una matatizo ya kisaikolojia, unaonekana hupendi kujichanganya sana na watu
Pengine unahisi dunia hii kila mtu ni mbaya wako kutokana na maisha uliyopitia ukiwa mdogo, nadhani ukifuata ushauri wa kisaikolojia utapona au kupata nafuu angalau
ila kupona ni mpaka wewe mwenyewe utake kupona na uji tune kupona
Dunia ni sehemu nzuri zaidi ukiwa na marafiki na upendo, sasa wewe inaonekana hauna tafuta tiba
 
Utakuwa matatizo ya kisaikolojia.......anyway....nenda kwa wataalamu nadhani ukienda chuo kikuu Cha Dar es salaam pale utapata maelekezo......nenda haraka sana.......ugonjwa wa akili huwa unahitaji kuhudumiwa haraka sana kwasababu ukikomaa haunaga kutibu au kupatiwa matibabu utakuathiri miaka yote.....
 
Kuna mda unafika najiona niko tofauti na binadamu wenzangu.
Unaweza kuta tupo msibani, ajali au kwenye tukio la mauaji unakuta watu wote wako na huzuni ila mimi niko freshi na nina amani kabisa moyoni wala siwazi yani nachukulia ni jambo la kawaida tuu

Hata wakati wa usiku wa manene huwa siogopi kutembea nje na hata kama hilo eneo lina mashetani au linahisiwa vibaya mimi napita tuu.

Nina hasira za karibu sana na huwa nikigombana na mtu huwa sinaga time nae tena na hata tukija kupatana ni baada ya miaka mingi sana. Hali hii imenifanya kuwa mtu wa visasi na huwa sikubaligi kushindwa jambo kabisa, niko radhi nirudi nipambane na nishinde hilo jambo.

Huwaga najipenda mwenyewe kwanza halafu ndio naangalia na wengine.

Ndugu zangu hata wakifa mimi naona poa tuu na ninavyowaandikia hapa baba yangu ni marehemu na bado halinipi shida mimi naona kitu kidogo tuu.

Hata wazazi wangu nawachukuliwa kawaida tuu hata siwaogopi.
Shuleni nimewahi kuwa na uadui na wale wababe wa shule na kwanza nilikua sinaga time nao.

Kuna mmoja aliwahi kuniambia nina dharau mimi sikumjibu nikaendelea na mambo yangu.
Kuna mmoja alinipiga mgongoni hiyo ndo ikawa safari hadi saivi natamani nikamchome kisu.

Mimi raha yangu ni kusikia watu nisiowapenda wamepata matatizo hata kufa kabisa.
Mimi watu ninaowapenda ni wale wauaji na makatili waliowahi kutokea hapa duniani.

Mimi sipendagi kuonewa kabisa ila nikiona mtu anaonewa ambae hana hatia huwaga nakasirika sana na sa nyingine kuokoa huyo mtu.

Nimekua sina mda sana na wanawake, wakiniletea za kuleta nawapiga chini naendelea na maisha yangu peke yangu, Msichana yeyote akinisma vibaya mimi namfata nampiga makofi naondoka zangu maana mimi si mtu wa maneno.

Nimekua na kiburi mno hata ndugu zangu wanalitambua hili na hii imefanya baadhi ya watu wengi kuniogopa sana.

Sasa wakuu kama nilivyojielezea hapo nawezaje kuepukana na hali yangu hii niliyonayo?

Nawasilisha.
Hasira hulala kifuani pa mpu.mba.vu.
 
Big up,
Hiyo ni roho ya kikomando,
Kwa nini hukwenda kujifunza ukomando sasa?
 
Back
Top Bottom