Msaada: Nimenunua simu yenye icloud

Msaada: Nimenunua simu yenye icloud

jerryempire

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2017
Posts
5,830
Reaction score
10,090
Habari za muda huu wakuu

Nina shida nahitaji msaada wenu. Siku ya jana nilipitia pitia kupatana nikakutana na simu ya iphone 5s, nikaipenda but sina idea sana na iphone.

Basi nikaonana na muuzaji nkaikagua then nikamlipa but hakulog out account yake ya icloud.

Kufika home ndo wanaozijua iphone wakanambia mistake niliyoifanya. Nilivyompigia muuzaji akasema yeye hiyo simu alimpaga mdogo wake, hivyo mdogo wake alisahau password. Alivyokata simu sikumpata tena.

Je, kuna njia gani ya kuweza kulog out au kudownload vitu?

Msaada tafadhali, simu ndo ninayotumia hivi sasa
 
na hiyo simu kama ni ya uwizi pole yako

usijaribu kulog out hapo ndio utakuwa mwisho wako
na usipolog out kama ni ya uwizi kama hujawai lala mahabusu jiandae
 
Haiwezi toka mpk aliyeweka id aingize password,siku nyingine ukinunua simu kwa mtu hakikisha anafanya hard reset uanze upya ww
 
Hiyp ni sawa na kopo tu pole ... Huwezj fanyia chochote kauze spare na ukifanya masihara unakamatwa na polisi
 
Tumia kama Nokia tochi kupiga na kupigiwa tu na kupiga picha...ila jiandae mda wowote na siku yoyote isiyo na jina kujikuta unapewa kESI isiyo na dhamana na maisha yako ya uraiani yatakua mwisho otherwise Jiandae kutoa hela mara 50 ya ulizompa jamaa akakupa hyo simu.

Kama ulimpa Laki zidisha mara 50 ukikosa JELA ILEEEEEE
 
Mwenye simu alikua na Million 10 alikua na gari aina ya Range rover ambalo hatujui lilipo hadi leo.

Mdogo ake alikutwa kafariki nae pia alikutwa kafariki..sasa Kwa maelezo hayo alaf wewe ndo umekutwa na simu UNAANZAJE JITETEA?
Online simu ni cheap sana hizo iPhone refurbished zipo kibao
 
Habari za muda huu wakuu nlikuwa nashida nahitaji msaada wenu,ni kwamba siku ya jana nilipitia pitia kupatana nikakutana na simu ya iphone 5s,nikaipenda but sina idea san na iphone basi nkaonana na maaskaji nkaikagua then nkamlipa but hakulog out account yake ya icloud,kufika home ndo wanaozjua jua iphone ndo wakanambia mistake nloifanya nlivyompigia mahkaji akasema yeye hyo sm alimpaga mdogo wake,hivyo mdogo wake alisahau password,alivyokata sm skumpata tena,je kuna njia gan ya kuweza kulog out,au kudown load vitu msaada tafadhali smu ndo nnayotumia now
Duh ndugu umeingia choo cha masokwe aisee hapo ni hatari tupu na uki restore ndo inageuka kopo kabisa hata home screen ndo hutoiaccess. itumia tu ivyo ivyo maana kwa sasa kutoa icloud ni shughuli ya kubahatisha
 
Duh ndugu umeingia choo cha masokwe aisee hapo ni hatari tupu na uki restore ndo inageuka kopo kabisa hata home screen ndo hutoiaccess. itumia tu ivyo ivyo maana kwa sasa kutoa icloud ni shughuli ya kubahatisha
Choo cha masokweee khaa
 
uza kopo ilo kwa ajili ya spare parts kama unataka jela isikuusu
 
Hiyo imekula kwako,niuzie better na display,alikua ndio maana Sasa hapatikani hewani.

Kuna vitu vingi katika I Cloud,mail address,jina la utoto,mtaa ulioishi utotoni na maswali mengimengi .
 
Back
Top Bottom