Endelea kuwaogopa. Najua kuwaogopa huko hakukuzuii kuwa nao kwenye discussion shule au kijamii/kanisani...etc etc.
Natamani kukuambia ujitahidi uendelee kujitunza utaona mafanikio yatakavyokuja kwako kwa wingi.
Mithali 6:32 ilivyosema, "Kila aziniye na mwanamke hana akili kabisa" haikukosea mdogo wangu. Angalia marafiki zako ambao sio madomo zege wanatumia muda gani kwa sasa kufikiria hao wanawake. Its a lot of time, resources and energy ambayo ingeelekezwa kwingine wangekuwa mbali kuliko wanavyodhani.
Vijana wa kiume huwa hatupewi hii elimu. Kijana wa kiume anasifika kwa idadi ya wadada aliotembea nao. Siwezi kukuamulia, lakini be very proud of who you are. Hizo hofu ulizonazo ni mapito tu. Kadri muda unavyozidi kwenda utakutana na binti ambaye hata hutohitaji mbinu za JF kuweza kuzungumza naye. Ni raha sana to let love take its course..mtakutana darasani, kazini, kanisani, barabarani, mtaani...mtaanza kama marafiki na baada ya muda hutohitaji kwenda kozi ya kutongoza, it will be so easy mdogo wangu.
Kama kijana wa kiume, rijali...ni sahihi kuwaza hayo lakini do not dwell in them. Umri huo wako ni umri wa kutengeneza mahusiano ya kukujenga kielimu zaidi. Ukishaanza kuendekeza kutongoza kila binti anayepita machoni pako huwezi tena kuwa na mahusiano mazuri na wadada maana wote utataka kuwavua nguo.
I wish you all the best shuleni kwako..usiogope kuwa domo zege, it is the best thing to happen to you kwa sasa!
[HASHTAG]#blessings[/HASHTAG]