Msaada nasumbuliwa na maumivu ya shingo

Msaada nasumbuliwa na maumivu ya shingo

Travis_Kitengo

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2021
Posts
316
Reaction score
905
Habari za wakati huu wana Jf,

Jamani kama miez miwili iliyopita nilikuwa nasumbuliwa na maumivu ya kichwa na macho kuvuta, misuli ya shingo kuuma nikaenda hospital nikaambiwa nina shida ya macho (Myopia) nikashauriwa tiba yake ni miwani.

Baada ya vipimo nikaambiwa natakiwa kuvaa miwani yenye lens power -0.25. Sasa baada ya kuanza kutumia miwani hali bado haijawa sawa pia nafanya kazi inayonihitaji kutumia computer na nikiwa natumia computer huku nimevaa miwani baada ya dakika chache huwa naanza kuhisi macho kuuma, kichwa kuuma mpk misuli ya shingo na mabega huwa inauma na huwa nahisi shingo kuchoka.

Issue nyingine pia kuna muda huwa nahisi kama misuli ya shingo, mabega , mikono na unyayo vinakuwa kama vinawaka moto.

Naombeni ushauri wa kitaalamu hapa issue inaweza kuwa ni nini na matibabu yake.​
 
Hiyo ni shida ndogo sana, unahitajika matambiko, nitafute nikupige nyungu...
 
Embu weka nondo hapa mkuu.
Kile kitaa kikiwaka blue, ile miale yake sio mizuri, itakusababishia kichwa kuuma, mwili kuchoka, na kupelekea hali ya presha ambayo nahisi mleta mada ndio kinachomsumbua (miguu kuwaka moto). Hii hali ilishanitokea; suluhisho ni kukiziba kile kitaa kama hana mbadala wa kitendea kazi kingine zaidi ya hicho.​
 
Kuna uwezekano mkubwa shida yako siyo macho. Kama unakaa muda mrefu na posture mbovu inaweza kukuletea shida. Vilevile inawezekana pia ni shida ya disc (kwenye uti wa mgongo). Kitaalamu tunaita Herniated disc . Mara nyingi tiba yake hii ni mazoezi kutoka kwa wataalam wa mazoezi, au unaweza pata steroid injection na ukawa sawa tu.
 
Kile kitaa kikiwaka blue, ile miale yake sio mizuri, itakusababishia kichwa kuuma, mwili kuchoka, na kupelekea hali ya presha ambayo nahisi mleta mada ndio kinachomsumbua (miguu kuwaka moto). Hii hali ilishanitokea; suluhisho ni kukiziba kile kitaa kama hana mbadala wa kitendea kazi kingine zaidi ya hicho.​
Ok nadhani uko sure mkuu, maana nilisoma remote sensing kwamba hata kulala karibu na Suboffer muda huo ikiwa on ile miale yake ya blue si mizuri kabisa kiafya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom