Hii inanikumbusha dogo mmoja aliwahi kuwauliza ndg wa mama yake alipo baba yake. Ndg wa mama wakaona labda ni kwa sababu ya ugumu wa maisha kijijini, wakaamua kumpeleka mjini.
Huku mjini walimpeleka shule. Huko shuleni alikutana na kijana wakawa marafiki na hivyo akawa anaenda nae kwao. Siku moja walimkuta mama wa rafiki yake, akawa anamwangalia sana yule kijana. Hatimaye alimuuliza jina lake na asili ya baba na mama yake. Dogo akaeleza asili ya mama yake na jina lake ila baba alisema hamjui hana historia yoyote juu ya baba.
Mama wa rafiki yake aliposikia jina la mama wa dogo, akajua dogo ni motto wa kaka yake, kwani alimpa mimba mwanafunzi akiwa kidato cha pili miaka ya 1988 na hasa jinsi dogo alivyokuwa anafanana na kaka yake.
Kwa mtindo huo dogo aliweza kukutana na baba yake.
Mungu huwa akipanga jambo, litawezekana, hivyo nawe jitahidi utampata baba siku moja