Kirachacha
Member
- Jan 8, 2013
- 67
- 48
Wasalam.
Mimi ni mdada naishi Arusha na nnasoma chuo,ada najilipia na nina mtoto mdogo. Nna msichana wangu wa kazi anaetokea Busaka iko Chato Geita. Huyu binti aliishia form 2 baada ya kukosa ada. Japo alikuwa na nia ya kusoma mazingira ya kwao ni magumu. Kwenda shule ndo abahatishe, hata akienda shule nyumbani hawezi kusoma, yeye na wadogo zake ndio wakafanye vibarua nyumbani wapate kula.
Mimi nilivyomchukua nia yangu ilikuwa anisaidie kumwangalia mwanangu wakati mimi nasoma, akikuwa kidogo na mimi nikimaliza chuo nimpeleke akasome QT au hata kozi fupi tu ili na yeye ajipatie ujuzi utakaomsaidia mbeleni, hilo halijabadilika.
Kinachofanya nije kwenu ni kwamba ana mdogo wake ambae licha ya kwamba wazazi walimwambia asije akafaulu maana hawawezi kumsomesha alifanya vizuri na akapata nafasi ya kwenda form 1 huko huko kwao. Tangu januari hajahudhuria shuleni mpaka wazazi walipoanza kusumbuliwa na mgambo. Sasa leo wamempigia huyu dada yake (binti yangu)wakitaka atume pesa ya ada. Alivyoniomba ushauri nimeshindwa kumwambia moja kwa moja kama atume au la maana yeye mwenyewe ana wasiwasi kwamba anaweza akajikamua akatuma mshahara wake lakini ikawa kazi bure. Wingi wa kazi, kukosa mwanya wa kujisomea nk vikafanya asipate chochote shuleni.
Sasa nafikiria kumsaidia ila nahitaji support kidogo.
Naweza kumchukua nikae nae pamoja na dada yake nimtafutue na shule. Kama kuna yeyote anaeweza kuniunga mkono kwa msaada wa hali, mali au mawazo ntashukuru sana. Kwa atakaependa kujua zaidi awe huru kuniuliza kwa PM, mawasiliano zaidi naweza kutoa baadae.
Ahsanteni.
Mimi ni mdada naishi Arusha na nnasoma chuo,ada najilipia na nina mtoto mdogo. Nna msichana wangu wa kazi anaetokea Busaka iko Chato Geita. Huyu binti aliishia form 2 baada ya kukosa ada. Japo alikuwa na nia ya kusoma mazingira ya kwao ni magumu. Kwenda shule ndo abahatishe, hata akienda shule nyumbani hawezi kusoma, yeye na wadogo zake ndio wakafanye vibarua nyumbani wapate kula.
Mimi nilivyomchukua nia yangu ilikuwa anisaidie kumwangalia mwanangu wakati mimi nasoma, akikuwa kidogo na mimi nikimaliza chuo nimpeleke akasome QT au hata kozi fupi tu ili na yeye ajipatie ujuzi utakaomsaidia mbeleni, hilo halijabadilika.
Kinachofanya nije kwenu ni kwamba ana mdogo wake ambae licha ya kwamba wazazi walimwambia asije akafaulu maana hawawezi kumsomesha alifanya vizuri na akapata nafasi ya kwenda form 1 huko huko kwao. Tangu januari hajahudhuria shuleni mpaka wazazi walipoanza kusumbuliwa na mgambo. Sasa leo wamempigia huyu dada yake (binti yangu)wakitaka atume pesa ya ada. Alivyoniomba ushauri nimeshindwa kumwambia moja kwa moja kama atume au la maana yeye mwenyewe ana wasiwasi kwamba anaweza akajikamua akatuma mshahara wake lakini ikawa kazi bure. Wingi wa kazi, kukosa mwanya wa kujisomea nk vikafanya asipate chochote shuleni.
Sasa nafikiria kumsaidia ila nahitaji support kidogo.
Naweza kumchukua nikae nae pamoja na dada yake nimtafutue na shule. Kama kuna yeyote anaeweza kuniunga mkono kwa msaada wa hali, mali au mawazo ntashukuru sana. Kwa atakaependa kujua zaidi awe huru kuniuliza kwa PM, mawasiliano zaidi naweza kutoa baadae.
Ahsanteni.