Msaada mtoto ananyonya sana

Msaada mtoto ananyonya sana

momara

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2019
Posts
463
Reaction score
491
Habari

Ndugu zangu nina mtoto wa kiume wa miezi 3 ananyonya sana mpaka mama yake anachoka na hashibi ukimtoa analia.

Clinic wameshaur mtoto anyonye tu maziwa ya mama hadi afikishe miezi 6.

Je nini naweza kufanya kumsaidia mtoto na mamake?
 
Habari

Ndugu zangu nina mtoto wa kiume wa miezi 3 ananyonya sana mpaka mama yake anachoka na hashibi ukimtoa analia.

Clinic wameshaur mtoto anyonye tu maziwa ya mama hadi afikishe miezi 6.

Je nini naweza kufanya kumsaidia mtoto na mamake?
Mama naye aongeze kula chakula bora.
 
Asipo nyonya shida,,akinyonya shida,,,maziwa ndio chakula yake acha anyonye kadri awezavyo,,,mama ndio ahakikishe anakula vizuri zaidi ili maziwa yapatikane ya kutosha kwa ajili ya kukidhi haja ya mtoto ya unyonyaji!!!
 
Habari

Ndugu zangu nina mtoto wa kiume wa miezi 3 ananyonya sana mpaka mama yake anachoka na hashibi ukimtoa analia.

Clinic wameshaur mtoto anyonye tu maziwa ya mama hadi afikishe miezi 6.

Je nini naweza kufanya kumsaidia mtoto na mamake?
Hizi nadharia za kumnyonyesha mtoto Kwa miezi sita bila kumpa hata maji ni ujinga! Mpeni maziwa ya ng'ombe. Muanzishieni na uji mwepesi acheni kufuata kanuni za wazungu
 
Bila shaka atakuwa first born wenu. Hongereni sana.
1. Inaweza tu kuwa ni phase tu ya ukuaji wake, na ikapita tu bila shida baada ya muda fulani. Hapa mama ndo anapaswa kula vyakula vinavyochochea utoaji wa maziwa kama mbegu za maboga, pilipili manga etc.

2. Wanawake wanatofautiana kwenye kutoa maziwa. Kuna wanaotoa kidogo, wengine mengi. Kuna wanaotoa mepesi na wengine mazito etc. So usikute maziwa hhayamtoshii mtoto.
Kama hana tatizo lolote, mnaweza muanzishia maziwa ya kopo. Hii mnajaribu tu kuona ni kwa nini analia akitolewa kwa nyonyo.
Kama tatizo litaendelea, rudi kaongeeni na wataalamu.

NB. Huu sio ushauri wa kitaalamu. Ni experience yangu ya kulea watoto wangu wawili kwa miaka saba.
 
Tatizo siku hizi wamekuja na kasumba za ajabu mahospitalini kuwa mtoto apewe maziwa ya mama tu kwa miezi sita. Huu ni upuuzi wa hali ya juu.

Sisi tulilewa kwa kunyonyeshwa maziwa ya mama lakini tulipewa uji mwepesi kama kawaida na mpaka leo tuna watoto pia.

Nahisi itakuwa ni mtoto wenu wa kwanza, kama kuna mama yako ama mama mkwe wako au mtu mzima yeyote alie karibu mshirikisheni katika kukupeni ushauri. Atakuelekezeni jinsi ya kutengeneza uji wa mwepesi wa mtoto mchanga.

Vijijini mtoto wa mwezi mmoja anakandikwa ugali na wanakuwa fresh tu.
 
Tatizo siku hizi wamekuja na kasumba za ajabu mahospitalini kuwa mtoto apewe maziwa ya mama tu kwa miezi sita. Huu ni upuuzi wa hali ya juu.

Sisi tulilewa kwa kunyonyeshwa maziwa ya mama lakini tulipewa uji mwepesi kama kawaida na mpaka leo tuna watoto pia.

Nahisi itakuwa ni mtoto wenu wa kwanza, kama kuna mama yako ama mama mkwe wako au mtu mzima yeyote alie karibu mshirikisheni katika kukupeni ushauri. Atakuelekezeni jinsi ya kutengeneza uji wa mwepesi wa mtoto mchanga.

Vijijini mtoto wa mwezi mmoja anakandikwa ugali na wanakuwa fresh tu.
Asante
 
Mwendo wa supu, uji, na mitori vinywewe vya moto, weka na pilipili manga kwenye uji na mtori...

...hivyo ni vya kuongezea juu ya lunch na dinner, sio mbadala.

Mtoto atanyonya na mengine mtakamua mtauza!
 
Andaa unga wa uji dona/sembe andaa mwenyewe home osha mahindi yakasagwe....unachukua unga hata nusu kikombe unaloweka kwenye maji kikombe kimoja na nusu, unga utatuama chini maji yatabaki juu...chukua hayo maji yachemshe, kanatokea kauji flani laini sana mpe mtoto atashiba, atalala vizuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom