Pole sana!
Tatizo sio modem bali ni traffic jam kwenye network yao. tiGO kimeo, wameanzisha data services kwa bei ndogo tena unlimited; yaani haina kikomo cha kiasi cha data unachotumia. Inapotokea ukabrowse muda mrefu, modem inakata yenyewe na wakati mwingine inakuja message eti 'subscribe data package'.
Mwanzoni ilikuwa poa lakini tangu watu waijue imekuwa na msongamano mkubwa. Kama tiGO wanataka kukamata wateja, basi mafundi wao wafanyekazi kurekebisha capCITY ya system yao au watuwekee limit kama wanavyofanya providers wengine.
Bure ghali!