JosephMagige
Member
- Apr 24, 2021
- 6
- 6
Habari member wenzangu wa jf mm ni kijana wa miaka 21 ningependa kupata msaada wa tatizo hili linalonisumbua kwa takribani mwaka 1 sasa la kuhisi maumivu makali sana katika korodani zangu hasa mara nyingi uume unapokuwa umesimama kwa muda mrefu au napokuwa na dem gheto baada ya kufanya romance kwa muda maumivu haya hutokea na pindi yatokeapo kuna kitu kama mshipa huonekana kutuna katika mfuko wa korodani ila baada ya muda hupotea na maumivu huisha kabisa nimejaribu kwenda hospital napomuelezea doctor huhisi ni hernia ila nimepiga ultra sound mara mbili zote majibu yake ni kuwa amna tatizo naombeni msaada wenu ndugu kwa yeyote mwenye uelewa na tatizo hili maana linanitesa sana