Msaada, mahusiano yasiyoeleweka

Msaada, mahusiano yasiyoeleweka

CIC malema

Member
Joined
Apr 23, 2021
Posts
10
Reaction score
29
Habari wakuu soma Kwa makini kisha unisaidie mawazo

Mimi ni kijana wa miaka 25 ni HIV+ ninamalizia elimu yangu chuo fulani kikubwa hapa nchini

Nimekua na mahusiano na mdada mmoja ambae amemaliza chuo last year ambaye na yeye ni HIV+ lakini mahusiano yetu yamekua yanachangamoto sana kutokana na umbali tunaoishi ambako kwa sasa yeye yuko mkoa mwingine na mimi japokua mimi nimekua a tendency ya kwenda kuonana nae mara kwa mara na zaidi wakati akiwa ana ishi kwao

Shughuli ilianza mara baada ya nyumbani kwao kumkabidhi biashara yake mwenyewe kwa ajili ya kujikimu tangu hapo tumekua tunaenda katika muelekeo usio mzuri kimahusiano , sababu zimekua nyingi mara yeye yuko busy na shughuli mara hivi na vile yote nikawa navumilia labda sababu ya umbali tulionano

Tukio la kwanza kunshtua ni pale alipoomba tusitishe uhusiano kwa maana kwamba yeye hayuko Happy na uhusiano kwa Sababu tu mimi na yeye tunapishana malengo na miaka by the time mean kanizidi almost 2 years na akadai mimi siko tayari kwa ajili ya ndoa kwa mawazo yake yeye kitu ambacho mimi sikioni kama ni sahihi kwa sababu if kumsaidia kwenye shughuli kadha wa kadha ninafanya hivyo na kimsingi nilikua nimeshampenda sana na mipango ilikua mwaka huu mwishoni tufunge ndoa kama ikishindikana basi mwakani ingewezekana .....nikawa nambembeleza tuendelee na uhusiano (manake mbali na kumpenda ukiwa na situation niliyonayo mimi kupata mtu wa kua nae maishani siku hizi ni mtihani na huko clinic kuna muda unaombwa pesa ili kuunganishwa na mtu na nimeshafika hadi hatua ya kutafuta online lakini ikawa ngumu) akawa kama hataki anasema ananipenda lakini hataki tu uhusiano kila mtu awe free at last nikasema nimekuelewa na nikamwambia "nikishakubali moyoni kwamba nimeachana na wewe sitakaa nirudi".....akaonesha kutokukubaliana na statement yangu hiyo na mimi nikamwambia kama umefikia hatua ya kusema hivi sioni kama hisia tulizoanza nazo bado zipo akadai ikitokea you are able huko mbeleni na ukaona ninafaa kuolewa na wewe utanioa na nikamwambia itakua na maana gani mimi kucheza kamari kwenye swala la kuoa? Yaani manake yeye akipata mtu anaolewa akikosa mimi nipo....kirahisi tu nikamuleza kwamba kwangu haipo na haitatokea kama tunaachana tuachane lakini sio kua mguu ndani mguu nje

Baada ya muda akarudi anasema ananipenda sana ila umbali ni tatizo...nikamwambia nashukuru kwa upendo wako na kimsingi hisia zilikua zimepungua sana juu yake kutokana na situation ya kusema tusitishe uhusiano baada ya hapo tukawa tunawasiliana kwa muda mrefu tu ikafikia hali tukakubaliana kuendelea( kwa sababu kuna muda nakua sina choice na inanibidi iwe hivyo ikumbukwe pia ninakimbizana na lifespan manake sielewi guarantee ya maisha ikoje natamani kuacha japo legacy ya mwanangu hapa ulimwenguni na hata kama nitaishi muda mrefu basi niwe na familia imara hata nitakapokua mzee......ieleweke idea yangu si kwamba nafeel nitakufa mapema Kwa sababu ya hali yangu ila ninaweza kufa muda wowote kwa sababu ni binadamu)

Mbali na hayo baada ya kuendelea na uhusiano hali ilikua mbaya kuna muda unatuma texts zinajibiwa kifupi tu au sim mnaongea as if ni watu msiofahamiana mazungumzo ambayo sio ya uchangamfu hata kama wewe ukiamua kuchangamka manake mimi kwenye uchangamfu na utani niko vyema ninaamini hivyo and ukimuuliza anaishia kusema maisha ni magumu and sometimes hakushiriki mambo yake lakini yako anataka ajue hasa kuhusu fedha na mengineyo mengi kitu ambacho kwangu sikuona kama tatizo ila yeye kwake alikua hayuko tayari ujue kwa siku anaingiza shingapi na ilikua inapelekea yeye kuficha changamoto zinazomkabili kwa kuhofia nitauliza anaingiza kiasi gani na projection ya kila kitu ili biashara yake iende mbele

Usichoke tafadhali....soma unisaidie mawazo

Baada ya hapo hiyo hali haikuwahi kubadilika na ukimuuliza kwanini anadai hatuna story za kupiga ila every time anakua online watsApp na anaweza akaamka ukiacha kumjulia hali na yeye hakujulii hali

Basi siku moja nikaamua kumuuliza ili tujue hatma yetu ni ipi akanijibu jibu la kila siku kwamba anachanganyikiwa kwamba plan zangu na zake ni tofauti mara mimi mwanafunzi kitu ambacho kwa muda mrefu nimekua nikiachukia kusikia kwa sababu kuna mahitaji nampatia na mimi silii kwake kwamba sina hiki...nina vyanzo vyangu halali vya mapato .....baada ya kusema hivyo mimi nikamwambia fanya unachoona ni sahihi kwako wala usijilazimishe kua na Mimi...ukimuambia hivi hajibu anakaa kimya kirefu then ananiita malema...... Halafu anasema tuliache Mungu ataliamua

Kwa muda huu sina matumaini na yeye sana niko na mambo yangu na nimepunguza mawasiliano nae japokua yeye kwa sasa ameanza kunitafuta

Na muda huu kuna wadada kama wanne hivi ambao nina fikiri ni VE- ambao wote wanaonesha nia ya kutaka kua na mimi kwa sababu kitambo niliwahi watongoza na baada ya kujua hali yangu nikaamua kuwapotezea kwa sababu nitaumia mmoja akiambukizwa kwa sababu yangu kama mimi nilivyoambukizwa na mtu baada ya makosa ya utumizi wa mpira na kuna nyakati nawaza kua na mmoja wapo ambae yeye ni mstaarabu na anajitambua japo niwe natumia condom lakini nikiwaza kilichonitokea mimi naacha kumpa sana matumaini na zaidi ninakua nawaza for how long nitatumia nae condom asilazimishe tusitumie?


Kutokana na situation hiyo binafsi niko njia panda hapa

Huyu mmoja kati ya wanne wasio na hali kama yangu yuko very committed na hajui hali yangu na sio yeye tu asiejua almost hata watu wangu wengi wa karibu hawajui isipokua huyu partner niliekua nae na wafanyakazi wa CTC

Na wa pili ni huyu ambae ana hali kama yangu japokua kwa sasa mambo yake siyasomi vyema na anarudirudi kwangu

Je nichague kipi? Niamua nini?
 
Usilazimishe mapenzi, huyo mwanamke hakutaki, muelewe endelea na maisha yako, hiyo kurudi kuwasiliana nawe sio kwamba ndio karudisha mapenzi hapana, inawezekana huko anakotega nae bado hapajaeleweka ndio maana anakukeep keep ili pakibuma anarudi kwako....upo tayari kuwa mpenzi wa dharura????

Usipaparikie ndoa umri wako mbona ni wa kujipanga kwanza, ndoa ni zaidi ya hivyo vimahusiano vya kichina, ndoa ni majukumu uko tayari???

Hongera kwa kuwa na roho nzuri, Mungu akupe mke mwema mdogo wangu.
 
Usilazimishe mapenzi, huyo mwanamke hakutaki, muelewe endelea na maisha yako, hiyo kurudi kuwasiliana nawe sio kwamba ndio karudisha mapenzi hapana, inawezekana huko anakotega nae bado hapajaeleweka ndio maana anakukeep keep ili pakibuma anarudi kwako....upo tayari kuwa mpenzi wa dharura????

Usipaparikie ndoa umri wako mbona ni wa kujipanga kwanza, ndoa ni zaidi ya hivyo vimahusiano vya kichina, ndoa ni majukumu uko tayari???

Hongera kwa kuwa na roho nzuri, Mungu akupe mke mwema mdogo wangu.
Asante Mungu akubariki

Kuhusu ndoa ninatazama hali yangu ninahisi yafaa nikiwahi
Majukumu ninayaweza kwa asilimia kubwa

Ninashukuru nitafanyia kazi
 
Habari wakuu soma Kwa makini kisha unisaidie mawazo

Mimi ni kijana wa miaka 25 ni HIV+ ninamalizia elimu yangu chuo fulani kikubwa hapa nchini

Nimekua na mahusiano na mdada mmoja ambae amemaliza chuo last year ambaye na yeye ni HIV+ lakini mahusiano yetu yamekua yanachangamoto sana kutokana na umbali tunaoishi ambako kwa sasa yeye yuko mkoa mwingine na mimi japokua mimi nimekua a tendency ya kwenda kuonana nae mara kwa mara na zaidi wakati akiwa ana ishi kwao

Shughuli ilianza mara baada ya nyumbani kwao kumkabidhi biashara yake mwenyewe kwa ajili ya kujikimu tangu hapo tumekua tunaenda katika muelekeo usio mzuri kimahusiano , sababu zimekua nyingi mara yeye yuko busy na shughuli mara hivi na vile yote nikawa navumilia labda sababu ya umbali tulionano
Tukio la kwanza kunshtua ni pale alipoomba tusitishe uhusiano kwa maana kwamba yeye hayuko Happy na uhusiano kwa Sababu tu mimi na yeye tunapishana malengo na miaka by the time mean kanizidi almost 2 years na akadai mimi siko tayari kwa ajili ya ndoa kwa mawazo yake yeye kitu ambacho mimi sikioni kama ni sahihi kwa sababu if kumsaidia kwenye shughuli kadha wa kadha ninafanya hivyo ....na kimsingi nilikua nimeshampenda sana na mipango ilikua mwaka huu mwishoni tufunge ndoa kama ikishindikana basi mwakani ingewezekana .....nikawa nambembeleza tuendelee na uhusiano (manake mbali na kumpenda ukiwa na situation niliyonayo mimi kupata mtu wa kua nae maishani siku hizi ni mtihani na huko clinic kuna muda unaombwa pesa ili kuunganishwa na mtu na nimeshafika hadi hatua ya kutafuta online lakini ikawa ngumu) akawa kama hataki anasema ananipenda lakini hataki tu uhusiano kila mtu awe free at last nikasema nimekuelewa na nikamwambia "nikishakubali moyoni kwamba nimeachana na wewe sitakaa nirudi".....akaonesha kutokukubaliana na statement yangu hiyo na mimi nikamwambia kama umefikia hatua ya kusema hivi sioni kama hisia tulizoanza nazo bado zipo akadai ikitokea you are able huko mbeleni na ukaona ninafaa kuolewa na wewe utanioa na nikamwambia itakua na maana gani mimi kucheza kamari kwenye swala la kuoa? Yaani manake yeye akipata mtu anaolewa akikosa mimi nipo....kirahisi tu nikamuleza kwamba kwangu haipo na haitatokea kama tunaachana tuachane lakini sio kua mguu ndani mguu nje

Baada ya muda akarudi anasema ananipenda sana ila umbali ni tatizo...nikamwambia nashukuru kwa upendo wako na kimsingi hisia zilikua zimepungua sana juu yake kutokana na situation ya kusema tusitishe uhusiano baada ya hapo tukawa tunawasiliana kwa muda mrefu tu ikafikia hali tukakubaliana kuendelea( kwa sababu kuna muda nakua sina choice na inanibidi iwe hivyo ikumbukwe pia ninakimbizana na lifespan manake sielewi guarantee ya maisha ikoje natamani kuacha japo legacy ya mwanangu hapa ulimwenguni na hata kama nitaishi muda mrefu basi niwe na familia imara hata nitakapokua mzee......ieleweke idea yangu si kwamba nafeel nitakufa mapema Kwa sababu ya hali yangu ila ninaweza kufa muda wowote kwa sababu ni binadamu)

Mbali na hayo baada ya kuendelea na uhusiano hali ilikua mbaya kuna muda unatuma texts zinajibiwa kifupi tu au sim mnaongea as if ni watu msiofahamiana mazungumzo ambayo sio ya uchangamfu hata kama wewe ukiamua kuchangamka manake mimi kwenye uchangamfu na utani niko vyema ninaamini hivyo and ukimuuliza anaishia kusema maisha ni magumu and sometimes hakushiriki mambo yake lakini yako anataka ajue hasa kuhusu fedha na mengineyo mengi kitu ambacho kwangu sikuona kama tatizo ila yeye kwake alikua hayuko tayari ujue kwa siku anaingiza shingapi na ilikua inapelekea yeye kuficha changamoto zinazomkabili kwa kuhofia nitauliza anaingiza kiasi gani na projection ya kila kitu ili biashara yake iende mbele

Usichoke tafadhali....soma unisaidie mawazo

Baada ya hapo hiyo hali haikuwahi kubadilika na ukimuuliza kwanini anadai hatuna story za kupiga ila every time anakua online watsApp na anaweza akaamka ukiacha kumjulia hali na yeye hakujulii hali

Basi siku moja nikaamua kumuuliza ili tujue hatma yetu ni ipi akanijibu jibu la kila siku kwamba anachanganyikiwa kwamba plan zangu na zake ni tofauti mara mimi mwanafunzi kitu ambacho kwa muda mrefu nimekua nikiachukia kusikia kwa sababu kuna mahitaji nampatia na mimi silii kwake kwamba sina hiki...nina vyanzo vyangu halali vya mapato .....baada ya kusema hivyo mimi nikamwambia fanya unachoona ni sahihi kwako wala usijilazimishe kua na Mimi...ukimuambia hivi hajibu anakaa kimya kirefu then ananiita malema...... Halafu anasema tuliache Mungu ataliamua

Kwa muda huu sina matumaini na yeye sana niko na mambo yangu na nimepunguza mawasiliano nae japokua yeye kwa sasa ameanza kunitafuta

Na muda huu kuna wadada kama wanne hivi ambao nina fikiri ni VE- ambao wote wanaonesha nia ya kutaka kua na mimi kwa sababu kitambo niliwahi watongoza na baada ya kujua hali yangu nikaamua kuwapotezea kwa sababu nitaumia mmoja akiambukizwa kwa sababu yangu kama mimi nilivyoambukizwa na mtu baada ya makosa ya utumizi wa mpira na kuna nyakati nawaza kua na mmoja wapo ambae yeye ni mstaarabu na anajitambua japo niwe natumia condom lakini nikiwaza kilichonitokea mimi naacha kumpa sana matumaini na zaidi ninakua nawaza for how long nitatumia nae condom asilazimishe tusitumie?


Kutokana na situation hiyo binafsi niko njia panda hapa

Huyu mmoja kati ya wanne wasio na hali kama yangu yuko very committed na hajui hali yangu na sio yeye tu asiejua almost hata watu wangu wengi wa karibu hawajui isipokua huyu partner niliekua nae na wafanyakazi wa CTC

Na wa pili ni huyu ambae ana hali kama yangu japokua kwa sasa mambo yake siyasomi vyema na anarudirudi kwangu

Je nichague kipi?
Niamua nini?
Aisee
Pole sana

Kifupi huyo mwenye hali kama yako ni opportunist
Na usiji victimize kissi hicho jiamini and your choice will come at the right time

Haya maisha yetu Mungu anayajua
 
Usilazimishe mapenzi, huyo mwanamke hakutaki, muelewe endelea na maisha yako, hiyo kurudi kuwasiliana nawe sio kwamba ndio karudisha mapenzi hapana, inawezekana huko anakotega nae bado hapajaeleweka ndio maana anakukeep keep ili pakibuma anarudi kwako....upo tayari kuwa mpenzi wa dharura????

Usipaparikie ndoa umri wako mbona ni wa kujipanga kwanza, ndoa ni zaidi ya hivyo vimahusiano vya kichina, ndoa ni majukumu uko tayari???

Hongera kwa kuwa na roho nzuri, Mungu akupe mke mwema mdogo wangu.
Ushauri mzuri, aufuate.
 
Asante Mungu akubariki

Kuhusu ndoa ninatazama hali yangu ninahisi yafaa nikiwahi
Majukumu ninayaweza kwa asilimia kubwa

Ninashukuru nitafanyia kazi
Kwani hali yako ina nini mzee baba? Hiyo mbona kawaida tu pata dawa zako maisha yanaendelea....hiyo hali isikuendeshe, ukikubali ikuendeshe utaangukia pua.

Kwanini unahisi kwa hali hiyo unahitaji kuwahi? Mi bana nikionaga kijana wa kiume 20s anaongea habari za ndoa sijui naonaje yani naona unajitwisha mzigo.
 
Kwani hali yako ina nini mzee baba? Hiyo mbona kawaida tu pata dawa zako maisha yanaendelea....hiyo hali isikuendeshe, ukikubali ikuendeshe utaangukia pua.

Kwanini unahisi kwa hali hiyo unahitaji kuwahi? Mi bana nikionaga kijana wa kiume 20s anaongea habari za ndoa sijui naonaje yani naona unajitwisha mzigo.
Ok sawa asante
 
Pole sana kwa hiyo hali unayo pitia hasa kwenye afya ni Jambo la muhimu ujilinde kwa hali na Mali, swala la mapenzi na kusheshimiana ni vitu viwili tofauti; inaonyesha unamuhehimu sana ukichanganya na kupenda hapo umeonyesha ukomavu, Sasa iweje meenzio hivyo vitu vyote viwili hana? Ni kwanini usitafute mtaalam wa ushauri nasaa akupe namna ya kuepuka hilo tatizo. Jichunguze wewe ni nani na yeye ni nani unaweza pata njia ya kuondokana na msongo wa mawazo unao kuandama. Kwa wanaume Jambo Hilo ni hatari waweza poteza pumzi.
Sawa mkuu nashukuru
 
Pole sana kwa hiyo hali unayo pitia hasa kwenye afya ni Jambo la muhimu ujilinde kwa hali na Mali, swala la mapenzi na kusheshimiana ni vitu viwili tofauti; inaonyesha unamuhehimu sana ukichanganya na kupenda hapo umeonyesha ukomavu, Sasa iweje mwenzio hivyo vitu vyote viwili hana? Ni kwanini usitafute mtaalam wa ushauri nasaa akupe namna ya kuepuka hilo tatizo. Jichunguze wewe ni nani na yeye ni nani unaweza pata njia ya kuondokana na msongo wa mawazo unao kuandama. Kwa wanaume Jambo Hilo ni hatari waweza poteza pumzi.
 
Pole sana kwa ambayo moyo wako unapitia,

Ukweli ni kwamba haya mahusiano uliyopo sasa ni mahusiano hata mkiingia kwenye ndoa ni majuto,

Swala la ndoa mwanamke halazishwi, ukiona unatumia nguvu sana jua ana mahusiano mengine au ana mipango binafsi,

Kwakua unapata changamo sana kupata mwenza kutokana na changamoto uliyonayo nashauri mkubalie aliyetari kua na wewe kwenye mahusiano, inaonesha ni mwanamke sahihi kwako ndoa sio tendo tu kuna maisha mengine kama kujaliwa, kuheshimiwa, watoto, kupendwa na kuthaminiwa kama baba, kuhusu condom vumilia kheri utumie kinga milele lakini uwe na amani ya roho.

Pole kwa unayo yapitia.
 
Ivi kumbe huu ugonjwa watu wanajisegregate kias hiki? Watu tunavyochapana peku kitaa huku...daaa very sad.
 
Habari wakuu soma Kwa makini kisha unisaidie mawazo

Mimi ni kijana wa miaka 25 ni HIV+ ninamalizia elimu yangu chuo fulani kikubwa hapa nchini

Nimekua na mahusiano na mdada mmoja ambae amemaliza chuo last year ambaye na yeye ni HIV+ lakini mahusiano yetu yamekua yanachangamoto sana kutokana na umbali tunaoishi ambako kwa sasa yeye yuko mkoa mwingine na mimi japokua mimi nimekua a tendency ya kwenda kuonana nae mara kwa mara na zaidi wakati akiwa ana ishi kwao

Shughuli ilianza mara baada ya nyumbani kwao kumkabidhi biashara yake mwenyewe kwa ajili ya kujikimu tangu hapo tumekua tunaenda katika muelekeo usio mzuri kimahusiano , sababu zimekua nyingi mara yeye yuko busy na shughuli mara hivi na vile yote nikawa navumilia labda sababu ya umbali tulionano

Tukio la kwanza kunshtua ni pale alipoomba tusitishe uhusiano kwa maana kwamba yeye hayuko Happy na uhusiano kwa Sababu tu mimi na yeye tunapishana malengo na miaka by the time mean kanizidi almost 2 years na akadai mimi siko tayari kwa ajili ya ndoa kwa mawazo yake yeye kitu ambacho mimi sikioni kama ni sahihi kwa sababu if kumsaidia kwenye shughuli kadha wa kadha ninafanya hivyo na kimsingi nilikua nimeshampenda sana na mipango ilikua mwaka huu mwishoni tufunge ndoa kama ikishindikana basi mwakani ingewezekana .....nikawa nambembeleza tuendelee na uhusiano (manake mbali na kumpenda ukiwa na situation niliyonayo mimi kupata mtu wa kua nae maishani siku hizi ni mtihani na huko clinic kuna muda unaombwa pesa ili kuunganishwa na mtu na nimeshafika hadi hatua ya kutafuta online lakini ikawa ngumu) akawa kama hataki anasema ananipenda lakini hataki tu uhusiano kila mtu awe free at last nikasema nimekuelewa na nikamwambia "nikishakubali moyoni kwamba nimeachana na wewe sitakaa nirudi".....akaonesha kutokukubaliana na statement yangu hiyo na mimi nikamwambia kama umefikia hatua ya kusema hivi sioni kama hisia tulizoanza nazo bado zipo akadai ikitokea you are able huko mbeleni na ukaona ninafaa kuolewa na wewe utanioa na nikamwambia itakua na maana gani mimi kucheza kamari kwenye swala la kuoa? Yaani manake yeye akipata mtu anaolewa akikosa mimi nipo....kirahisi tu nikamuleza kwamba kwangu haipo na haitatokea kama tunaachana tuachane lakini sio kua mguu ndani mguu nje

Baada ya muda akarudi anasema ananipenda sana ila umbali ni tatizo...nikamwambia nashukuru kwa upendo wako na kimsingi hisia zilikua zimepungua sana juu yake kutokana na situation ya kusema tusitishe uhusiano baada ya hapo tukawa tunawasiliana kwa muda mrefu tu ikafikia hali tukakubaliana kuendelea( kwa sababu kuna muda nakua sina choice na inanibidi iwe hivyo ikumbukwe pia ninakimbizana na lifespan manake sielewi guarantee ya maisha ikoje natamani kuacha japo legacy ya mwanangu hapa ulimwenguni na hata kama nitaishi muda mrefu basi niwe na familia imara hata nitakapokua mzee......ieleweke idea yangu si kwamba nafeel nitakufa mapema Kwa sababu ya hali yangu ila ninaweza kufa muda wowote kwa sababu ni binadamu)

Mbali na hayo baada ya kuendelea na uhusiano hali ilikua mbaya kuna muda unatuma texts zinajibiwa kifupi tu au sim mnaongea as if ni watu msiofahamiana mazungumzo ambayo sio ya uchangamfu hata kama wewe ukiamua kuchangamka manake mimi kwenye uchangamfu na utani niko vyema ninaamini hivyo and ukimuuliza anaishia kusema maisha ni magumu and sometimes hakushiriki mambo yake lakini yako anataka ajue hasa kuhusu fedha na mengineyo mengi kitu ambacho kwangu sikuona kama tatizo ila yeye kwake alikua hayuko tayari ujue kwa siku anaingiza shingapi na ilikua inapelekea yeye kuficha changamoto zinazomkabili kwa kuhofia nitauliza anaingiza kiasi gani na projection ya kila kitu ili biashara yake iende mbele

Usichoke tafadhali....soma unisaidie mawazo

Baada ya hapo hiyo hali haikuwahi kubadilika na ukimuuliza kwanini anadai hatuna story za kupiga ila every time anakua online watsApp na anaweza akaamka ukiacha kumjulia hali na yeye hakujulii hali

Basi siku moja nikaamua kumuuliza ili tujue hatma yetu ni ipi akanijibu jibu la kila siku kwamba anachanganyikiwa kwamba plan zangu na zake ni tofauti mara mimi mwanafunzi kitu ambacho kwa muda mrefu nimekua nikiachukia kusikia kwa sababu kuna mahitaji nampatia na mimi silii kwake kwamba sina hiki...nina vyanzo vyangu halali vya mapato .....baada ya kusema hivyo mimi nikamwambia fanya unachoona ni sahihi kwako wala usijilazimishe kua na Mimi...ukimuambia hivi hajibu anakaa kimya kirefu then ananiita malema...... Halafu anasema tuliache Mungu ataliamua

Kwa muda huu sina matumaini na yeye sana niko na mambo yangu na nimepunguza mawasiliano nae japokua yeye kwa sasa ameanza kunitafuta

Na muda huu kuna wadada kama wanne hivi ambao nina fikiri ni VE- ambao wote wanaonesha nia ya kutaka kua na mimi kwa sababu kitambo niliwahi watongoza na baada ya kujua hali yangu nikaamua kuwapotezea kwa sababu nitaumia mmoja akiambukizwa kwa sababu yangu kama mimi nilivyoambukizwa na mtu baada ya makosa ya utumizi wa mpira na kuna nyakati nawaza kua na mmoja wapo ambae yeye ni mstaarabu na anajitambua japo niwe natumia condom lakini nikiwaza kilichonitokea mimi naacha kumpa sana matumaini na zaidi ninakua nawaza for how long nitatumia nae condom asilazimishe tusitumie?


Kutokana na situation hiyo binafsi niko njia panda hapa

Huyu mmoja kati ya wanne wasio na hali kama yangu yuko very committed na hajui hali yangu na sio yeye tu asiejua almost hata watu wangu wengi wa karibu hawajui isipokua huyu partner niliekua nae na wafanyakazi wa CTC

Na wa pili ni huyu ambae ana hali kama yangu japokua kwa sasa mambo yake siyasomi vyema na anarudirudi kwangu

Je nichague kipi? Niamua nini?
Kwanza nikupe pongezi wewe ni shujaa,
Pili nikuombe umsamehe na maisha yaendelee..ninachoamini ni kwamba kutofautiana katika mahusiano ni kawaida hakuna mahusiano yaliyonyooka....cha kufanya kama uko mwaka wa mwisho chuo,mwambie unataka kwenda kujitambulisha kwao na hatua zingine za kuoana ziendelee pindi unapomaliza chuo unafunga ndoa chap..

Kaka kupata mchumba wa kuoa imekuwa issue sana hata kwa sisi tulio negative,atleast wewe unaye huyo tena ameshajua na kufanya biashara maisha mbona yatasonga tu
 
Pole sana kwa ambayo moyo wako unapitia,

Ukweli ni kwamba haya mahusiano uliyopo sasa ni mahusiano hata mkiingia kwenye ndoa ni majuto,

Swala la ndoa mwanamke halazishwi, ukiona unatumia nguvu sana jua ana mahusiano mengine au ana mipango binafsi,

Kwakua unapata changamo sana kupata mwenza kutokana na changamoto uliyonayo nashauri mkubalie aliyetari kua na wewe kwenye mahusiano, inaonesha ni mwanamke sahihi kwako ndoa sio tendo tu kuna maisha mengine kama kujaliwa, kuheshimiwa, watoto, kupendwa na kuthaminiwa kama baba, kuhusu condom vumilia kheri utumie kinga milele lakini uwe na amani ya roho.

Pole kwa unayo yapitia.
Asante sana
 
Kwanza nikupe pongezi wewe ni shujaa,
Pili nikuombe umsamehe na maisha yaendelee..ninachoamini ni kwamba kutofautiana katika mahusiano ni kawaida hakuna mahusiano yaliyonyooka....cha kufanya kama uko mwaka wa mwisho chuo,mwambie unataka kwenda kujitambulisha kwao na hatua zingine za kuoana ziendelee pindi unapomaliza chuo unafunga ndoa chap..

Kaka kupata mchumba wa kuoa imekuwa issue sana hata kwa sisi tulio negative,atleast wewe unaye huyo tena ameshajua na kufanya biashara maisha mbona yatasonga tu
Ok sawa asante
 
Ivi kumbe huu ugonjwa watu wanajisegregate kias hiki? Watu tunavyochapana peku kitaa huku...daaa very sad.
Wanajisegragate vipi?

Jamii ina stigmatise na wao ndio wanafeel inferior
 
Cool down...usipaparikie mahusiano, hebu kula life kwanza ( ngono ikaushie maana ishaleta soo), piga heneiken, kitomoto humu duniani kuna raha ajabu
 
Back
Top Bottom