Msaada kwenye interview

Chibidu

JF-Expert Member
Dec 19, 2008
387
49
Wakuu poleni kwa majukumu mazito ya kuikwamua nchi yetu. Wakubwa naomba msaada wenu. Nimeitwa kwenye interview ya kazi kwenye kampuni moja ya usafirishaji. Tatizo langu ni kuwa, mara ya mwisho nilifanya interview wakati natafuta kazi mwaka 1998. Sasa nahisi nimepitwa na wakati, maana tangu nipate kazi mwaka huo sijawahi kuomba kazi nyingine mpaka leo na wala sijawahi kushiriki kwenye kuwafanyia watu interview. Wale wazoefu naomba mnisaidie, ni vitu gani siku hizi waajiri wanauliza sana? Nadhani mtakuwa mmenisaidia sana mimi na wengine wanaojiandaa kwa interview za kazi. Asanteni kwa kunivumilia
 
Mimi siyo mtaalam sana wa interviews, ila nimekuwa nikona mambo haya yakiulizwa na kupimwa

  1. Ufahamu juu ya kampuni uliyoomba kazi
  2. Ufahamu wa kazi uliyoomba na uwezo wa kumudu kazi uliyoiomba-Fahamu kwa undani majukumu ya kazi uliyoimba na wadau mtakaofanya nao kazi kwa pamoja
  3. Added values ulizonazo
  4. Uwezo wa kujieleza
  5. Relevant experience- Wengine huuliza specific questions kutoka kwa CV yako
  6. General knowledge
 
Mkuu kinachohitajika kwenye hizi interviews ni kuonyesha kuwa una uwezo wa kufanya waliyoorodesha kwenye job descriptions bila kusahau uwe na mifano ambayo wakikuuliza zaidi uwe na uwezo wa kawajibu. Mwishoni unaweza kujiuza kwao kwa kuwaeleza ni kitu gani (mfano ujuzi n.k) ambacho utawaletea au kuwaongezea kwenye kampuni yao kama wakikuajiri wewe.
Kumbuka pia kupata kazi si interview peke yake, wanaangalia pia kama unaweza ku click/patana na wafanyakazi wao wengine - hivyo usiwe mkavu sana na jaribu kuongea nao kama unawafahamu bila utani!! Kila na heri
 
Wakuu mliojitolea kunipatia hizi nondo nawashukuru sana. Mmenisaidia kuniongezea confidence. Tuendelee kuepeana maarifa
 
Explain to us about yourself.............

That is the main question which they asked. Jingine wameuliza kuhusu mshahara ninaotaka...Sikuona swali jingine la maana. Sijui jamaa walikuwa wamechoka!!! Sikuona hata swali moja professional lililoulizwa. Labda inawezekana walishampata mtu wao sasa walikuwa wanatimiza wajibu tu.
 
Jamani maswali mengine mbona ya kuumiza vichwa vya watu tu! Sasa wewe si unajua kazi uliyoiomba na maswali yote yata base kwenye hilo?
Sasa unataka nani ajibu nini kwa kitu asichokijua.

Mtafute Katibu mwenezi wa CCM yeye huwa ana majibu hata kabla ya maswali.
 
Back
Top Bottom