Msaada kwenu tafadhali: Gharama za Passport

Msaada kwenu tafadhali: Gharama za Passport

Joined
Oct 29, 2012
Posts
86
Reaction score
4
Nina imani nitasaidiwa haraka.

Naombeni mnijuze gharama na "process" ya kukata paspoti ya kimataifa kwa hapa Tanzania. Nataka kusafiri kwenda Marekani.

Jamani nipo "serious", hebu nijuzeni na wala sina maana nyengine yoyote zaidi ya kutaka kujua.
 
Ukitaka fasta taarisha laki na nusu within two weeks unaipata...! Ukitaka ki halali ni tsh 50000 ila kaa tayari kuisubiri miezi kumi na mbili
 
km uko dar nenda wizara ya mambo ya ndani ukachukue fomu uijaze na gharama za passport kubwa ni sh 50,000/=
au nenda pale manispaa kuna branch za uhamiaji juu ghorofani uliza watakuonesha


Nina hakika 90%, mada hii niliotuma hapa si mahala pake, ila nina imani nitasaidiwa haraka.

Naombeni mnijuze gharama na "process" ya kukata paspoti ya kimataifa kwa hapa Tanzania. Nataka kusafiri kwenda Marekani.

Jamani nipo "serious", hebu nijuzeni na wala sina maana nyengine yoyote zaidi ya kutaka kujua.
 
Kwa kufata process zote kihalali nilitumia elfu hamsini tu na ilitoka ndani ya siku kumi. Njia ya mkato andaa laki na nusu mpaka lakini tatu ukichelewa sana utapata ndani ya siku tatu.
SPEAKING FROM EXPERIENCE
 
Labda tumsaidie muuliza swali kwa kumwambia vitu gani anavyotakiwa kwenda navyo ili asikumbane na nenda rudi
 
Nenda pale kurasini ukiwa umevaa shati la mikono mirefu lenye thamani ya laki 2,nakuhakikishia ndani ya wiki 2 unaipata...
 
Elfu hamsini tu na unapata ndani ya two weeks. No hongo wala longolongo.
Nenda mwenyewe, chukua fomu, kajaze huko kwako, wape wadhamini wajaze nafasi zao na kusaini ambatanisha chetichako cha kuzaliwa, kama umeajiriwa kwenye taasisi ijulikanayo/rasmi ambatanisha na barua toka kwa mkuu wako na hatimaye peleka Uhamiaji pamoja na cash, ukiziwakilisha utaambiwa ulipe kama ziko ok, utapatiwa risiti halafu Utachukuliwa alama za vidole (nadhani sasa itakuwa digital), picha nk hapohapo uhamiaji. Utapangiwa siku ya kuchukua.
 
Jamani na mimi niko serious naombeni gharama za kupata visa ya UK

Pia vile vile anayejua gharama ya kupata ya DUBAI. je hizi nitazipata kwa shs ngapi kila moja na kwa muda gani maana nina wiki kama 3 hivi tu
 
Wote Mliotoa Hongo Ni MAPOPOMA! Utatoaje Hongo Wakati Ni Haki Yako? Ukiwahi Kujaza na Kuirudisha Basi Ndani Ya Siku 10 Za Kazi Unapata Pasipoti Yako ILA Ukiwa Kimbelembele UNAPOPOMIWA Tu Kama Mlivyofanyiwa Na Mkome Kuhonga.
 
Nina imani nitasaidiwa haraka.

Naombeni mnijuze gharama na "process" ya kukata paspoti ya kimataifa kwa hapa Tanzania. Nataka kusafiri kwenda Marekani.

Jamani nipo "serious", hebu nijuzeni na wala sina maana nyengine yoyote zaidi ya kutaka kujua.

Usisahau pia cheti cha kuzaliwa cha mzazi wako mmoja au Affidavit, cheti chako cha kuzaliwa, barua ya utambulisho toka kwa mwajiri au serikali ya mtaa, leaving certificate form four au cheti cha elimu ya msingi, na 50,000/ . Passport unapata baada ya siku 14 bila longolongo, otherwise utokee usumbufu kama majina kuwa na dosari .
 
jamani mbona hiyo ya UK hamnijibu? Au mpaka nianzishe uzi mwingine tujaze server!
 
Ingia website ya ubalozi wa uk tz tafuta sehemu ya visa aplic jaza kuwa na viza kadi kulipia online
 
Shukrani sana kwa kunijuza vyema. Ahsante nawashuru kwa wenu wema.
Shukrani tena nasema, Mungu wa pekee awape rehema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom