Msaada kwa mliotangulia kujenga

Msaada kwa mliotangulia kujenga

Dexta

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2015
Posts
2,322
Reaction score
5,803
Habari za mchana wakuu?

Ninaomba wenye uzoefu na maswala ya ujenzi mnisaidie hapa.

Kulingana na ramani hii, mpaka nyumba ikamilike inaweza kutumia tofali ngapi na bati ngapi?

Nawasilisha.
IMG-20221016-WA0026.jpg
 
Habari za mchana wakuu?

Ninaomba wenye uzoefu na maswala ya ujenzi mnisaidie hapa.

Kulingana na ramani hii, mpaka nyumba ikamilike inaweza kutumia tofali ngapi na bati ngapi?

Nawasilisha.View attachment 2390129
Tofali 1500
Bati 90
Mbao 2*3 200

msingi mpaka kuezeka andaa 10m

Ila ongea na fundi akudesignie kuwepo na mlango wa nyuma
 
Tofari 1200
Bati 75 mpaka 80

Speaking from experience

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
Daah msiwe wepesi kupotosha hata kama umejenga mara 100.

Heabu hiyo umeipataje?.

Ramani haina vupimo unakadiria kwa macho.

1. Je msingi utatumia tofali ngapi?
3. Bomba/walling itatumia ngapi?
3. Bati umetumia vipimo vipi kupata hiyo idadi?
4. Umemuuliza anatumia bati aina ipi? Kawaida au IT5 ?
 
Makadirio ya standard room yaani 4m kwa 3.5m unatakiwa uwe na tofati kati ya 2000 hadi 2500.
1. 4x2=8
2. 3.5x2=7

Jumla ya mzunguko ni 15m.

Note: 1m=tofali 2.
15x2=30 laini moja.

1 A. Msingi wa laini 7
7x30=210 hizi ni tofali za msingi.

1. B. Walling hadi kwenye lenta
30x laini 10=300.

Hivyo chumba kimoja kuanzia msingi hadi lenta ni tofali 510 tu.

Jitahidini kuheshimu taaluma.

Hayo makadirio ya chumba kimoja tofali 2500 ni upotoshaji mkubwa sana
 
1. 4x2=8
2. 3.5x2=7

Jumla ya mzunguko ni 15m.

Note: 1m=tofali 2.
15x2=30 laini moja.

1 A. Msingi wa laini 7
7x30=210 hizi ni tofali za msingi.

1. B. Walling hadi kwenye lenta
30x laini 10=300.

Hivyo chumba kimoja kuanzia msingi hadi lenta ni tofali 510 tu.

Jitahidini kuheshimu taaluma.

Hayo makadirio ya chumba kimoja tofali 2500 ni upotoshaji mkubwa sana

Mkuu naona umejibu bila kudig deep ,hiyo raman ina vyumba viwili ,sebule pamoja na jiko! Nimejibu in general anahitaji jumla ya tofali kati ya 2000 hadi 2500 kwa nyumba hiyo kwa kuchukulia ya standard room ya 4m kwa 3.5m means jiko na sebule vitafuata proportionality ya standard room ,sijamaanisha kwamba chumba kimoja kitakula tofali 2000 hata kanjanja hawezi kusema hivyo....Nimebobea kwenye ujenzi kwahiyo BOQ hainipi shida hata kama atapandisha ya ghorofa.
 
Habari za mchana wakuu?

Ninaomba wenye uzoefu na maswala ya ujenzi mnisaidie hapa.

Kulingana na ramani hii, mpaka nyumba ikamilike inaweza kutumia tofali ngapi na bati ngapi?

Nawasilisha.View attachment 2390129
Kabla ya yote yatupasa kujua yafuatayo:
1. Location... Inajengwa wapi?
2. Landscape ipoje? Tambalale au slope
3. Aina gani ya udongo upo hapo. Hapa huamua msingi ujengweje

Baada ya kujua hayo, tunaweza jua idadi kamili ya materials
 
Mleta Mada amefanya kuwe na Majibu tofauti, kwanza hajasema vipimo vya nyumba yake, pili hatutajua mlalo wa kiwanja chake, kama Kiko tambarale au kipo kwenye mwinuko.

Kwahiyo majibu mengi atakayopata hapa yatakuwa ni Makadirio zaidi kuliko Uhalisia.
 
Back
Top Bottom