Changamoto zipo lakini ni za kawaida kama vyuo vingine na hizi changamoto nadhani kwa kuwa miaka ya karibuni wameanzisha course nyingi hivyo kupelekea kupokea wanafunzi wengi. 1. Madarasa ya kusomea, hii inapelekea kusoma kwa shift unaweza kukuta mnasoma mwaka mmoja lakini unakuta wengine wanamalizia muhula wengine wapo likizo hivyo hivyo. 2. Sehemu za kulala pia ni changamoto kuna uwezekano wa jukosa hostel za chuo hivyo ajiandae kupanga hostel nje ya chuo. 3. Changamoto ya ngono ni kawaida sehemu zozote zile. 4. Vibaka upande wa usiku ajichunge sana anapokua anatoka nje ya chuo kipindi cha usiku. Mazingira yapo poa tu kwa kusomea hasa kipindi hichi cha kiangazi maana wametengeneza vimbweta vya kusomea vingi tu chini ya miti kuzunguka chuo. 6. Chuo kipo mjini hivyo changamoto za mjini za kawaida. 7. Chuo kipo karibu na soko hivyo la vyakula la mabibo. 8. Walimu wapo poa tu. 9. Maktaba pia ni changamoto maana maktaba iliyopo ni ndogo lakini watu wanashea hivyo hivyo na mambo yanakwenda lakini nahisi wanlifanyia kazi hilo