msaada kuhusu startimes

msaada kuhusu startimes

delako

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2012
Posts
3,011
Reaction score
2,049
Kuna thread iliwahi letwa hapa barazan kuwa waweza kuangalia startimes bila kulipia!!NAOMBA KWA ANAYEJUA HATUA ZA KUPITA HILI NAMI NIWEZE KUANGALIA BURE...!NIMEFIKIA MAAMUZ HAYA BAADA YA VODA+STARTIMES KUNITAPELI KWAN 16/8/13 NILILIPIA 10,000/ KWA M PESA NA SMS YA UTHIBITISHO TOKA VODA IKAJA BUT TOKA SIKU HIYO MPAKA LEO HAWAJANIPA HIYO AIRTIME WALA KURUDISHA SALIO LANGU.NIMEULIZA VODA WANASEMA PESA INAONEKANA ILITUMWA KWENDA STARTIMES NA NIKIULIZA HUKO STARTIMES NI KM HAWAJIELEWI NI MAJANGAAA KWENDA MBELE.NAOMBA KUWASILISHA.NIPO DAR
 
kweli voda ni majanga elfu tano yangu imeyeyuka nimebaki na msg tu
 
kweli voda ni majanga elfu tano yangu imeyeyuka nimebaki na msg tu

Aisee nimecheka sana maana kuna jamaa yangu naye alitumiwa elfu kumi na salio akaangalia na msg ikaonekana. Cha kushangaza baada ya nusu saa akaletewa msg inamtaarifu kuwa muhamala umeshindikana kuangalia salio hamna kitu, aliishia kubaki na msg ya kupokea elfu kumi
 
Nipeni maujanja nichek bure japo kwa wiki 1!!Naomba huo msaada
 
Kama nataka kununua decorda hipi nichague kati ya hizi? STARTIMES, TING, DIGITEK naomba ushauri
 
Hawa jamaa wanatumia kanuni ya MTEJA MFALME kabla ya kupata huduma na ukipata huduma slogan inabadilika japo hawasemi na kuwa MTEJA ----, Hata mie niliwahi kununua umeme wa LUKU jamaa aliniambia nimnunulie kwa niaba process yote ikakamilika but no umeme nikaenda Voda wakasema nenda Tanesco na nikaenda Tanesco wakasema nenda Voda mbaya zaidi niliekuwa namnunulia nae ni mchungu kwenye hela nilipompa hiyo story akachukulia poa kwa kuwa ela alikuwa hajanipa nilichokuwa nafanya ni kununua alafu ananirejeshea (hapa ndio machungu yalipozidi)

Transaction za kidigitali ni nzuri ila kwa mazingira kama haya wanatufanya tuzidi kupenda kufanya mihamala ya face to face kwani walichotakiwa ni kuweka utaratibu wa nini cha kufanya endapo mihamala ya namna hiyo inaposhindwa kufanya kazi.

Nenda TCRA japokuwaTCRA nao sijui majukumu yao ni nini maana kwa issue kama hizi nadhani wao ndio wahusika kuhakikisha watumia huduma za simu wanahudiwa kikamilifu na mbaya zaidi sidhani kama wapo digitally kiasi kwamba ukipeleka shida yako hata kama upo kijijini through simu unahudiwa, wao wapo busy na kampeni ya kutotumia lugha chafu kwenye mitandao sasa sijui ubora wa utoaji huduma nani anasimamia
 
Wahanga wote naomba niwape pole sana. Pengine hilo si makosa yao, bado ni makovu ya lile janga la moto lililowakumba tarehe kama hiyo iliyotajwa na mleta uzi.

Bila shaka Vodacom kama watakuwa wanapitia malalamiko ya watu humu, waje watueleze ina maana ma-folders/ma-files muhimu ya kumbukumbu za wateja wao ndio zimepotea??

Nasema hili kwa sababu hata leo hii ukienda duka la Voda utakuta wateja wengi wanalia na upotevu wa kumbukumbu zao muhimu.
 
Kama nataka kununua decorda hipi nichague kati ya hizi? STARTIMES, TING, DIGITEK naomba ushauri

Kuondoa longolongo weka dish lako tu chanel zote muhimu unaona including za kimataifa na hulipii maana huduma zingine tunalipia lakini ukikaa kwenye runinga kuna channel wala hatuangalii
 
Kama nataka kununua decorda hipi nichague kati ya hizi? STARTIMES, TING, DIGITEK naomba ushauri
Mkuu kama bajeti inaruhusu DSTV ndiyo mpango mzima na burudani ya michezo mbalimbali juu.
 
Ukienda hapo mliman cty unapoingea na customer care ni km anakushangaa au anastaajab kuacha kaz zako kwenda kufuatilia 10000/.
 
Kwan kuona bure yawezekana au zilikuwa polojo??Naomba msaada
 
Back
Top Bottom