Msaada kuhusu simu za Google Pixels

Mkuu unaweza kwa maamuz yaku kununua huawei p40 pro plus kama cash unayo
Inategemea na matumizi na kiasi gani upo comfortable kutweak simu yako. Kama hujali kusideload apps na unapenda camera ni simu nzuri bado.

Ila kama ni kijana wa mjini huwezi kuishi bila snapchat na apps nyengine zinazotegemea google services itakuwa ngumu kuishi na hii simu.
 
Okay hata muonekano wake tu ni hovyo sijui wanafeli wapi hawa watu
Umarekani mwingi mkuu, wanataka simu zao ziwe kama iphone, wanacopy mambo yote mabaya, battery ndogo, bezell, kutoa 3.5mm jack etc.
 
nimekuuliza wew binafsi
 
nimekuuliza wew binafsi
Mimi natumia mkuu, kikubwa kabisa ninachoangalia ni uwezo wa kurun emulators, toka Vulkan ianze kuenea simu zisizotumia soc za qualcomm zinarun vizuri emulators. Hivyo hitaji langu kubwa inaweza kulitimiza.

Naweza kuishi bila apps za Google, na inatimiza pia hitaji langu la Extreme multitasking.

Vitu ambavyo ningependa viwepo zaidi ni xenon flash kama kwenye mate series, Napenda sana Xenon kuliko hizi led flash, pia wakitoa uwezo wa ku unlock bootloader ni plus zaidi.
 
Japo kuna maeneo sijaelewa kama haya emulators, unlocking bootloader nk...kwan hutaweza kutumia Apk?
 
Japo kuna maeneo sijaelewa kama haya emulators, unlocking bootloader nk...kwan hutaweza kutumia Apk?
simu ambayo bootloader yake ipo locked inaingia apk lakini hutaweza kuweka custom rom na mods mbalimbali zinakuwa limited.

emulators zenyewe zinakuwezesha kurun programs mbalimbali za mifumo mingine, mfano unaweza cheza games za ps2 kwenye simu yako. uka emulate game kali kama la mpira kuliko yanayopatikana playstore.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…