Msaada kuhusu elimu na Vyeo Jeshini

Mmhh mkuu sasa mbona nina ndugu yangu ana Diploma ila hivi sasa ninavyoandika ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini

Halafu hivi mazoezi yote hayo wanafanya wote wanaume na wanawake au kuna mazoezi ambayo wanawake wanakuwa excluded?
 
Umesaidia sana mkuu yaani umejibu mule mule ila nitajaribu kufuatilia na kwa sasa kama mambo yamebadilika

Shukrani sana
 
Kuna wenzake wana masters bado wanajitolea huko JKT mwaka wa 3 sasa.

Jeshini hamna mshahara kuna 'posho' tu.
Mmhh haya mambo yanachanganya sana yaani mtu ana masters ila bado anasota JKT miaka 3?

Mbona nina ndugu yangu mwingine ana diploma lakini hivi sasa ninavyoandika ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini au labda jeshini ni connections tu?
 
Oohh huyo mwalimu wenu alichukua muda gani hadi kupata nyota mbili?
 
Sasa mbona unatuchora wakati mtu wa kumfanyia reference unae
 
Anha kwahiyo mshahara unategemea na mtu anafanyia kazi kitengo gani huko jeshini?
 
Hapana mkuu haendi kwa sababu ya pesa anaenda kwa sababu anapenda jeshi ila tu anahitaji kujua kuhusu course zake na hilo la mshahara ni kama swali la nyongeza tu ila yeye jeshi analipenda

Halafu sijaelewa hapo uliposema marekani hadi mageneral wanaenda operation yaani inakuwaje? Na je hawa wa tanzania hawaendi?
 
Nadhani mambo yamebadirika saizi, nakupa hii ni experience kutoka kwa jamaa zangu nliomaliza nao form six 2015

Kabla yetu, yaani waliomaliza six mwaka 2014 walikua wakienda jkt kwa mujibu wakabakizwa jeshini walifanya course kwa muda wa miezi 9 Tu then wakapata nyota but kwa tuliomaliza 2015 mambo yalibadirika kidogo maana Mimi kuna jamaa zangu walibakizwa jeshini wakakaa kwanza kwa muda wa mwaka mzima bila kufanya chochote just wapo Tu kambini wanaamka, wanakula na kulala ili kupimwa uvumilivu.

Baada ya hapo mwaka uliofata 2016 walipelekwa course ya miezi mitatu, maana wao walikua wamepitia jkt after form6 so ile miezi mitatu waliyopekekwa course ilikua kukamilisha miezi sita ndipo wakapata bakabaka, wakafanya kazi mpaka 2018, ndipo wakapelekwa Monduli kwa ajili ya course ya uafisa (nyota), na course ya uafisa kwa sasa hivi ni kama mtu anaechukua degree, so kwa mtu alietoka six anasoma uafisa kwa muda wa miaka mitatu kama anaechukua bachelor, but kama ana degree tayari huyo basi anafanya course kwa muda wa miezi Tisa tuu

Zamani ilikua mtu mwenye bachelor anenda moja kwa moja kufanya course ya uafisa (nyota) kama akichaguliwa kujiunga na jeshi, but kwa sasa si hivo tena, mtu mwenye bachelor akichaguliwa anaenda kuanza course ya ucadet kwa muda wa miezi 6 (wanaita kumtoa uraia wa kawaida) baada ya hapo anapata bakabaka then anasubiri intake ya kwenda kusoma uafisa (nyota) kwa muda wa miezi Tisa ila inategemea na mambo mengi kama vile Afya, connection, nidhamu, so kwa sasa mtu kuishia ucadet (bakabaka) ingawa ana degree yake ni kitu cha kawaida Sana kama amekosa vitu nilivyovitaja hapo , hope nimesaidia kwa namna moja ama nyingine.

NB: ukimaliza course ya uafisa kama Umetokea form six au Una bachelor unapata nyota moja (ingawa hapa sina uhakika Sana kama nimekosea watanisahihisha wengine)
 
Itamchukua takribani miaka miaka 2 kasoro hivi kutoka jkt hadi kuwa officer wa nyota moja (Luteni - usu)
Hapo ni nje na kusubirishwa kabla ya kwenda kozi yaani tunaasume ameenda smoothly mwanzo mwisho
Duuh aise kwahiyo inaweza kuchukua hata miezi mtu kusubiri kutoka kwenye course moja kwenda nyingine?
 
Mmhh mkuu sasa mbona nina ndugu yangu ana Diploma ila hivi sasa ninavyoandika ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini
Halafu hivi mazoezi yote hayo wanafanya wote wanaume na wanawake au kuna mazoezi ambayo wanawake wanakuwa excluded?

Sasa hayo maswali si ungemuuliza huyo ndugu yako.??

Tatizo umei set akili yako kitu fulani alafu unakuja kuuliza ,unaambia ukweli unaukataa..

Jeshini sikuhizi ni kama enzi za nyerere uzalendo kwanza mbwembwe nyingine baadae..

Ataanza JKT, kisha atasota kwa muda fulani kupimwa uvumilivu, kisha atpewa bakabaka, kisha itamchukua muda si chini ya mwaka mmoja kuwa mwanajeshi wa kawaida, baada ya hapo atapelekwa kusoma u afisa(miezi 9), lakini hii yote inategemea connection pia so anaweza sota zaidi..
 
Msomi ukienda jeshini kwa ajiri ya ukosefu wa ajira kwa fani uliyosemea ipo siku utakuja jijutia huo uamuzi. Nenda jeshini kwa kupenda mwenyewe binafsi toka moyoni mwako..
Yeah yeye analipenda jeshi.

Na kwanini umesema hivyo mkuu?
 
Na hata mimi ndicho nilichogundua kwamba jeshini ni connection tu maana kila mtu anaongea lake

Nina ndugu yangu ana diploma ila hivi sasa ana nyota mbili na hajafikisha hata miaka minne jeshini
 
Kuna wenzake wana masters bado wanajitolea huko JKT mwaka wa 3 sasa.

Jeshini hamna mshahara kuna 'posho' tu.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Mkuu inabidi mfate uzalendo na siyo pesa wenye ni wafanyabiashara Tu na si ajira
 
Kama unawaza vyeo jeshini utapata tabu sana kwa nyakati hizi na degree yako bora ukalime nyanya ziwe resources viwandani huko. Jeshi linahitaji kwanza kuwa na self committment na kupenda sio vipaumbele vya vyeo na mishahara.
 
Usisikize porojo za watu, hakuna mtu anayesota JKT zaidi ya miaka miwili, JKT mwisho wa kukaa ni miwili tu na baada ya hapo kama hukupata ajira ni nyumbani.
Sawa Sawa Mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…