Mkuu,
Hiyo ni dhana na tatizo kubwa sana kwa vijana wetu. Punde tu baada ya kumaliza elimu yao ya Sekondari ya Juu, huwaza zaidi kuhusu kujiunga na Chuo. Hujidanganya na kuokoteza Uongo wa hapa na pale. Uongo huo na ushauri wanaopeana, hujijaza ujinga na uzandiki.
Yaani, kila Mara wao huwaza tu kuhusu kujiunga Chuo hata kabla ya matokeo kutoka. Sikatai wao kujishauri, La hasha!. Lakini, kujijaza ujinga ni aina mbaya ya tabia.
Cha msingi kaa naye chini, tafuta details za kutosha kuhusu Chuo husika. Muambie kwa nini anadhani Chuo hicho ni kizuri?
Muambie katika maelezo yake ajikite zaidi katika maeneo haya;
1) Mazingira ya Chuo
2) Ubora wa vifaa na walimu
3) Ushindani wa wataalamu wao baada ya kuhitimu.
Nakuhakikishia hana lolote analolijua. Wanadanganya tu kwenye magroup yako ya WhatsApp.
Unaweza kufatilia kuhusu hicho Chuo huku mitandaoni.