Poleeee kwa kuwa bado unampenda sana,ila wahenga walisema akufukuzaye hakwambii...........malizia,usichukue hatua haraka fanya uchunguzi wa kutosha kujua chanzo cha mabadiliko yake kisha ukijua ni kwa sababu upendo haupo tena au amepata mwingine jiondoe mapema japo itakuumiza na si rahisi,kuliko kumlazimisha muendelee naye,kwani wanaume sikuzote wana huruma kwa wanawake kwa hiyo ukimlazimisha anaweza kukuoa kwa sababu ya huruma na sio mapenzi jambo ambalo halifai kwani ndoa lazima iunganishwe na mapenzi au upendo na si kitu kingine.Halafu pia maumivu utakayoyapata baada ya kujua kuwa mmeo alikuoa kwa sababu ya huruma na si mapenzi ni makali zaidi kuliko maumivu utakayoyapata sasa hivi kwa kuachana naye.