Msaada: Hela ya unga, nakufa njaa

Msaada: Hela ya unga, nakufa njaa

Uza smartphone yako itatosha kununua unga na mtaji mdogo. Shalom.
 
Jf kuna uwezekano mkubw wa kuingia hata bila kuwa na MB, kama ilivyo kwangu pia. Jieleze kiufasaha endapo kama ni kweli umebanana tukusaidie.
 
Niliwahi kusimuliwa hadithi moja na mama yangu sisi ni wakristo lakini katika kupanga panga siku moja mama alikuta kitabu cha kiislamu kufungua ndani akakuta hadithi moja inasema hivi kuna mtu na mwanawe walikuwa maskini sana walikuwa waliishi nje, mbali ya mji ili ufike kwenye mji ni lazima upite kwenye pori. Kazi ya yule mtu na mwanae ilikuwa kujidamka na kwenda mjini kuomba na kurudi nyumbani. Kila siku walifanya hivyo lakini mara nyingi kama si mara zote waliambulia patupu. Siku moja wakati wakivuka lile pori yule baba maskini akawaza 'kwa nini nisikate kuni wakati naomba kwenye kijiwe changu nitaziweka niuze'?, basi akakata mzigo kiasi tu akaubeba ile kuingia mjini tu akasikia kunii we mzee mwenye kuni leta, akauza zile kuni wakanunua unga wakarudi nyumbani kesho yake wakakata kuni nyingi zaidi ikawa hata kabla ya kufika kijiweni kuni zinakuwa zimekwisha. Walibadili maisha yao kwani walikuwa wauza kuni maarufu kwenye maharusi, shule na matumizi ya nyumbani.Jamani sote kuna wakati tumepitia magumu yasioandikika lakini KUOMBA NI MWIKO.
 
USHAURI: njaa ni janga lisilotatuliwa kwa msaada wa siku moja. njaa si kama mtu aliekosa pango ya nyumba, huduma ya afya au matatizo mengine ya kawaida. ni vyema baada ya kupata msaada wa kujikinga na njaa kwa leo, ukae chini na kutafakari namna ya kujikwamua kwa muda mrefu zaidi ikiwemo kutafuta kazi au shughuli yoyote ya kujiingizia kipato............. pia ni ngekushauri uombe msaada wa chakula kuliko pesa maana unashida ya chakula. ukiomba msaada wa pesa moja kwa moja si watu wote watachukulia una shida maana kuna wimbi la matapeli pia wanaojifanya wanashida ilhali hawana.... niko mbali na home jioni nitaku inbox
 
Labda anataka cocaine.... na kwa nini asiuze smartphone yake akanunua unga
 
Wapendwa salaam alyk, tumsifu Yesu Kristo wana JF,

Kuanzia jana siko vizuri nimehangaika nimekosa nimetafuta bado sijapata wapendwa ninashida ya kusaidiwa hela ya unga tuu.

Please nisaidieni wana JF mwenzenu nakufa njaa.
Komaa mzee ...kama una miguu na mikono yote pambana utafute hela hata kwa kubeba kokoto...
Hata mimi hapa sina hela lakini napambana siombi ombi
 
Haya ni majibu mepesi kwa maswali magumu
Siyo majibu mepesi ni majibu sahihi ila kwa vile ww hujui maana ya freebasics yamekuwa majibu mepesi. . Huenda ana sbb zingine lkn kwa JF kuna 0.freebasics.com ni bure kbsa bila kuwa na salio hata hii post nimeituma kwa freebasics.com
Inafanya kazi kwa mtandao wa voda, Tigo na Airtel kwa opera min, mozila na chrome. Ukibishana jaribu ujioneee. Ingia opera min ingia sehemu ya kuandika anuani (enter address) andika www.0.freebasics.com
N:B
Mm ni mtumiaji mzuri sana wa www.0.freebasics.com kwahiyo huwa natumia mpaka kwenye pc
 
Unga gani ndugu? Maana neno unga lina maana nyingi na unga upo wa ina nyingi pia
 
Jamani mbona mnahoji pesa ya bando? Hamjui kuna kukopa?
Najua hii hali I wish ungekuwa karibu nami tungegawana unga na mchele nilivyo navyo, na maharage na njegere vyote ningekupa.

Ila kwakuwa ni mtandaoni sina jinsi, I wish ningekukutana njiani.
 
mkuu pole na majukumu kwa kuwa una uhakika wa kupata kaka unaonaje ukiweka simu yako rehani kwa mangi upate then ukiwa vizuri urejeshe deni lake.Kila mtu huwa anapitiwa na changamoto tatizo ni jinsi gani ya kuadress hili jambo
 
Back
Top Bottom