- Thread starter
- #21
Kama jamaa yako ni Bushoke mpotezee utafanya nini. Kama una real care then mpe hints, let him find out mwenyewe. Halafu, start to mind your business.
nimekuelewa sana kwa hili
Kama jamaa yako ni Bushoke mpotezee utafanya nini. Kama una real care then mpe hints, let him find out mwenyewe. Halafu, start to mind your business.
kama unaelewa maeneo au sehemu anazoingia huyo mwanamke na hao jamaa zake wa nje mchukue jamaa bila kumwambia then ashuhudie basi kazi yako itaisha maana yawezekana hawezi kuelewa kwa kuelezwa je hata picha napo asielewe???
Its non of your business. Wako kwani unauhakika gani kuwa ha do nje. Beware of life when you dont even know yourself!! PATHETIC.
Wewe siyo mmbea kama wengine wanavyojaribu kusema hapa. Kama kweli unamjali tafuta hata simcard tofauti au kama ana email, mwandikie meseji yenye maelezo na maelekezo sahihi yatakayomuongoza kuuona ukweli. Utakuwa umemsaidia na labda kumuokoa na kifo.
Kwa wakati huu hayo ni mahusiano ya ndoa na si ya u-girl friend na u-boyfriend, ni hatua tata sana ina changamoto zake nyingi so kwa mke wake kuwa kicheche ni sehemu ya changamoto ambazo rafiki yako anapitia kwa kujua ama kutojua, pengine baada ya muda atatulia na maisha yakaendelea hakuna kinachoshindikana chini ya jua.Swali ni kwamba ungependa jamaa ambwage mkewe au amuadhibu? na una hakika gani kama atampata mwingine tena wa type hiyo? Na wewe je mahusiano yako yapo salama kiasi gani? Kaa pembeni inawezekana si wewe tu unayoyaona pengine kuna rafiki zake au ndugu wanaona na wametulia au wameshampa ushauri na akachuna kulinda ndoa yake.
Wakati mwingine ni vizuri kumuacha mtu afanye makosa ili ajifunze.Ni hatari lakini salama!!!!!
Watasema mchonganishi we acha kaa kimya
ya ngoswe muachie ngoswe
asante kwa ushauri ingawa naamini mara ya kwanza yule msichana ndo alimcomvic anione mbaya