Steven Sambali
JF-Expert Member
- Jul 31, 2008
- 364
- 182
Wana Mtandao,
Kuna ombi kutoka kwa aliyekuwa Balozi (Konsula) wa Ubalozi wa Poland nchini Tanzania Prof. Augeniusz Rzewulski kanitumia ujumbe akiomba msaada wa kupata habari za huyu Msanii maarufu wa zamani nchini Tanzania, Fundi wa Kimataifa - Yakobo.
Huyu Msanii sanamu zake za kimakakonde alizokuwa akichonga kwenye shina la mti wa Mpingo ndiyo zilizokuwa zikipewa wageni wengi wanaokuja Tanzania.
Hata Obama alipokuja alipewa sanamu kama hiyo ingawa yeye Yakobo alishafariki ila ufundi wake hadi leo unaendelezwa na hao aliowaacha hadi leo wanachonga au kumwiga.
Mwenge siku moja nilibahatika kuziona kwa karibu na Archtect Chagula alianza kuzisifia hadi nikavutiwa na kuanza kuziangalia kwa karibu. Akaniambia nichukue picha kadhaa za hizo sanamu ambazo hadi leo ninazo. Kama siyo huyo Chagula basi nadhani nisingelikuwa na habari yoyote kuhusu hizo sanamu. Ni Mzee Rzewulski ndiye kaja kuniambia mwanzilishi huyu.
Prof. Rzewulski akiwa Tanzania bado ubalozini, alibahatika kuwasiliana naye na akamuomba amchongee sanamu moja. Kuna uwezekano mkubwa ndiyo ilikuwa sanamu yake ya mwisho ambayo hadi leo anayo hapa Poland. Baadaye alijulishwa amefariki na akafika kutoa pole na rambirambi kwa familia yake Fundi Yakobo. Hii ilikuwa mwaka 1996.
Kwa mapenzi makubwa aliyonayo kwake, mwezi wa nne ameamaua kufanya maonyesho ya Marehemu Yakobo na hasa sanamu zake ziitwazo UJAMAA.
Kama kuna mtu ana habari ni wapi naweza kuwasiliana na kupata habari zaidi, picha, Audio, Film nk basi itakuwa vema sana kufanikisha maonyesho hayo na wakati huo huo kutangaza jina la nchi kwani Watanzania tumekuwa tukilalamika Wakenya kutangaza vivutio vyetu vya utalii wakati sisi wenyewe hatufanyi hivyo.
Kama kuna mtu ana Email ya nyumba ya Makumbusho, Nation Museum, wafanyakazi wa TBS, Radio Tanzania, Michuzi Blogs, Mjengwa, Manyerere Jackton, Jasusi na waandishi wengine wengi na watu wa historia au waliobahatika kumfahamu, basi naomba msaada wenu.
Natanguliza asante. Mungu Ibariki Tanzania.
Majibu niandikie hapa JF au nitumie email: Ssambali@hotmail.com
Kuna ombi kutoka kwa aliyekuwa Balozi (Konsula) wa Ubalozi wa Poland nchini Tanzania Prof. Augeniusz Rzewulski kanitumia ujumbe akiomba msaada wa kupata habari za huyu Msanii maarufu wa zamani nchini Tanzania, Fundi wa Kimataifa - Yakobo.
Huyu Msanii sanamu zake za kimakakonde alizokuwa akichonga kwenye shina la mti wa Mpingo ndiyo zilizokuwa zikipewa wageni wengi wanaokuja Tanzania.
Hata Obama alipokuja alipewa sanamu kama hiyo ingawa yeye Yakobo alishafariki ila ufundi wake hadi leo unaendelezwa na hao aliowaacha hadi leo wanachonga au kumwiga.
Mwenge siku moja nilibahatika kuziona kwa karibu na Archtect Chagula alianza kuzisifia hadi nikavutiwa na kuanza kuziangalia kwa karibu. Akaniambia nichukue picha kadhaa za hizo sanamu ambazo hadi leo ninazo. Kama siyo huyo Chagula basi nadhani nisingelikuwa na habari yoyote kuhusu hizo sanamu. Ni Mzee Rzewulski ndiye kaja kuniambia mwanzilishi huyu.
Prof. Rzewulski akiwa Tanzania bado ubalozini, alibahatika kuwasiliana naye na akamuomba amchongee sanamu moja. Kuna uwezekano mkubwa ndiyo ilikuwa sanamu yake ya mwisho ambayo hadi leo anayo hapa Poland. Baadaye alijulishwa amefariki na akafika kutoa pole na rambirambi kwa familia yake Fundi Yakobo. Hii ilikuwa mwaka 1996.
Kwa mapenzi makubwa aliyonayo kwake, mwezi wa nne ameamaua kufanya maonyesho ya Marehemu Yakobo na hasa sanamu zake ziitwazo UJAMAA.
Kama kuna mtu ana habari ni wapi naweza kuwasiliana na kupata habari zaidi, picha, Audio, Film nk basi itakuwa vema sana kufanikisha maonyesho hayo na wakati huo huo kutangaza jina la nchi kwani Watanzania tumekuwa tukilalamika Wakenya kutangaza vivutio vyetu vya utalii wakati sisi wenyewe hatufanyi hivyo.
Kama kuna mtu ana Email ya nyumba ya Makumbusho, Nation Museum, wafanyakazi wa TBS, Radio Tanzania, Michuzi Blogs, Mjengwa, Manyerere Jackton, Jasusi na waandishi wengine wengi na watu wa historia au waliobahatika kumfahamu, basi naomba msaada wenu.
Natanguliza asante. Mungu Ibariki Tanzania.
Majibu niandikie hapa JF au nitumie email: Ssambali@hotmail.com