Naona wadau wamekujibu swali lako moja kuhusu Github na kusahau swali lako la pili kuhusu unahitaji kufahamu nini ili "Ku code forum web app"
Web application kama "Forum" ni complex kiasi na inahitaji "solid understanding" ya technologies kadhaa za "Web programming"
Ngoja nijitahidi kulijibu hili swali kwa lugha rahisi
Unahitaji "Database",hii ni program Maalum kwa ajiri ya kuhifadhi taarifa au data za forum yako
" Iwe majina ya members,emails,passwords,messages,threads,likes etc)
So unahitaji uwe na uelewa kidogo wa Databases na SQL
(SQL ni lugha ya computer inayowezesha web application yako kuzungumza na Database)
Kuna aina nyingi za Database systems kama Mysql,MongoDB,SQLlite...
Point: Jifunze SQL
Part ya pili ni backend
Hii ndiyo part inayohusika na "core logic" ya web application yako
Jinsi gani una rank threads, rank members,una handle vipi errors,members or guests....how forums yako ina behave yote hii ni kazi ya backend
Hapa unahitaji Server side Programming language kama PHP,Python,JavaScript etc
Point:Soma PHP , Python au JavaScript
Part ya mwisho ni Frontend,part ya web application ambayo "end user" ana Iona na Ku interact nayo
Hapa soma CSS, JavaScript na HTML