Habari wana wakubwa
Kwa kweni nakuja mbele yenu kutaka msaada niko na mke wangu mwaka wa 8 sasa na tumebahatika kupata watoto 2 wa kike na wa kiume.
Kwa hakika nampenda sana mke wangu kwani tumetoka mbali alinivumilia kuishi na mm kipindi kigumu cha kipato changu kua pia kwa kunizalia watoto.
Shida ni kua mke wangu kila siku tunakwaruzana kisa simu akiona simu inapigwa yeye ataikimbilia akiona jina la mwanamke basi anaweza kuipokea ili ajuwe ni nani au anataka musikilize shirika ukimalize aanze kuhoji huyo ni nani na anatala nn? Ukimiambia kua ni rafiki hakuelewi hapo ataanza oooo unawana wake kwa kua siku hizi una kazi kila nikijitahidi kumuelewesha basi hakubali ananiona kicheche
Hadi naiona ndoa haina amani mpaka natamani hata kutoa maamuzi mabaya ila tatizo watoto wangu bado wadogo nimekua namchoka kwa kutokuniamini hadi maneno machafu yanamyoka hutamani kumpiga ila najihisi nitamuonea.
Mimi simu yake sishiki wala sifuatiliii maana sioni sababu na nimemnunulia simu mbili ila anaweza akazifungia hata wiki eti hazina chaji wakati nyumbani pana umeme namtilia salio kwa mwezi basi unaweza kuisha mwezi bila ya yeye kutumia hilo salio.
Kwa kweli nampenda sana ila kuacha kutumia simu kwa ajili yake siko tayari kwani kazini kwangu kia na simu ni jamabo la lazima .