Mrithi wa Khamenei (Mojtaba) aamuru Kombora la kwanza

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
5,188
Reaction score
17,715
Iran imerusha makombora yake ya kwanza kuelekea Israeli leo Jumatatu Machi 09, 2026 baada ya kuteuliwa kwa Kiongozi mpya mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu, Ayatollah Seyyed Mojtaba Khamenei.

Kituo cha utangazaji cha Serikali ya Iran IRIB kimesema kwenye chaneli yake ya Telegram kwamba Iran imefyatua wimbi la kwanza la makombora chini ya Ayatollah Mojtaba Khamenei kuelekea maeneo yaliyokaliwa.

Imechapisha picha ya kombora lenye kauli mbiu "Kwa Amri Yako, Sayyid Mojtaba," marejeleo ya kidini ya madhehebu ya Kishia.

Wakati haya yakijiri, Waziri Mkuu wa Qatar na Waziri wa Mambo ya nje, Mohammed bin Abdulrahman Al Thani ametoa wito wa kupunguzwa kwa kiwango cha vita vya Iran.

Akiongea na Sky News Al Thani amesema hawakutarajia mashambulizi ya jirani yao Iran dhidi ya nchi za Ghuba, akiongeza kwamba uhalali na visingizio vya Tehran wanavyotumia vimekataliwa kabisa.

Wakati huo huo shambulizi la droni lililofanywa ana Iran nchini Bahrain limewajeruhi raia 32 katika kisiwa cha Sitre.
 
Nimependa roho ya kupambana ya waajemi, hawa magaidi namba moja duniani(Israel na Marekani) wanatakiwa wapate watu wa kuwatandika siku moja.

Hata hivyo, dunia inahitaji another superpower, japo China hafai kuwa superpower.
 
Sawa Sawa Lakini Nchi Zinazogombana Pia Zinazidiana Mbinu
Waongee Kutoa Tofauti Vinginevyo Kuna Upande Utaumia Vibaya
 
Nimependa roho ya kupambana ya waajemi, hawa magaidi namba moja duniani(Israel na Marekani) wanatakiwa wapate watu wa kuwatandika siku moja.

Hata hivyo, dunia inahitaji another superpower, japo China hafai kuwa superpower.
Wewe unataka nchi gani iwe Super Power. Ifanyeni basi Tanganyika yenu iwe Super Power.
 
Mojtaba Khamenei ni majeruhi alijeruhiwa kwa makombora yaliyomuua baba yake,na wala sidhani hata kama anawezabkuongea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…