MAKOLE
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 618
- 280
Ilikuwepo hadithi moja ya fisi iliyozua kisa cha "Tamaa ilimponza fisi" Mnyama huyu alialikwa kwenye sherehe mbili tofauti na zote zilifanyika kwa wakati mmoja. Fisi hakuwahi kuwa na busara na alipokuta chakula katika sherehe ya mwanzo hakijawa tayari alikwenda kwenye sherehe nyingine ili kuwahi makulaji.
Alifika na kukuta watu wanasafisha majamvi kuashiria kwamba tayari kumeliwa na akaamua kurudi sherehe ile ya awali ambapo napo alikuta tayari watu wameshakula"
Paliondokea bwana mmoja kwa jina la Mrisho Gambo aliyekuwa na majigambo kwenye zama za utawala wake.
Ikumbukwe kwamba Mrisho Gambo aliwahi kuwa mkuu wa wilaya ya Korogwe aliyekuwa na mbwembwe na tambo nyingi za kiuongozi.
Ikumbukwe pia kwa sasa bwana Mrisho Gambo anasubiri huruma ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete ili apangiwe kazi nyingine baada ya uteuzi wake kutenguliwa hivi karibuni.
Leo katika ukurasa wake wa facebook ametokelezea akiueleza umma kwamba ametumiwa salamu nyingi na wana wa Korogwe ambao "eti" wanamsihi arudi na kuokota fomu ya ubunge katika moja ya majimbo mawili ya mjini hapo......
Hili halishangazi sana kwani ni haki yake, ila tayarai bwana Gambo alishawahi kujigamba kwamba anakwenda Ilala kuwakilisha wana Ilala huko Dodoma akiwa na lengo la kumpokea kijiti Mbunge wa sasa!
Ushauri wangu ni kwamba bwana mkubwa awe na msimamo kwani tamaa ilimponza fisi?