PreGE2025 Mrisho Gambo: Ananyanyasa Watumishi kisa kuutaka Ubunge

PreGE2025 Mrisho Gambo: Ananyanyasa Watumishi kisa kuutaka Ubunge

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
"Wangapi mlienda kwenye mkutano soko kuu? mlisikia maneno aliyoyapiga mke wangu? baada ya pale walienda kumsimamisha kazi na sasa yupo nyumbani ana amani kabisa na yupo tayari akiambiwa achague kazi au mume wake atachagua mume wake. Wanasema hana vigezo tukaulizana vigezo hana baada ya kuongea jukwaani? miaka mitatu yote alikuwa navyo sasa hivi ndiyo avikose?

"Hata kama unataka kugombea njoo kwa utaratibu usinyanyase watu, kuna mjumbe mmoja wa kamati ya siasa anaitwa Asia alikuwa yupo Arumeru eti kwa sababu anakwenda ziara za mbunge wamemuamisha wamempeleka Ngorongoro lakini mpaka leo yupo Imara amebaki na msimamo wake ule ule kwa sababu Ngorongoro sio mbinguni ni hapahapa duniani. Halafu haya ni mambo ya mpito tu tunakwenda kwenye kura za maoni zikiisha uchaguzi ukiisha, maisha yanaendelea"

Pia, Soma: Mrisho Gambo: Mimi na yeye nani ameumiza wengi?

- Mrisho Mashaka Gambo Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Juni 14, 2025 wakati akizungumza kwenye mkutano mkuu maalumu wa utekelezaji ilani ya CCM uliofanyika katika kata ya Olasiti Jijini Arusha.

VIDEO: Jambo TV
 
Huyu Arusha wamemchoka, janja janja nyingi, kama mmbunge hakuna alichofanya for 5 yrs ! Anatafuta huruma tu, wakubwa pia hawamtaki !

Mapema sana kwenye kura za maoni ataliwa kichwa
 
Leo hii Gambo nayeye analalamika kunyanyaswa?!

Atulie aache kulia lia. Huo ndiyo mfumo walioujenga wao wenyewe nayeye akiwemo.

Mkiwa kwenye madaraka mnakuwa vibri & jeuri mnajenga sera na mifumo gandamizi na mnasahau kuwa kuna kesho hauna nguvu ya madaraka mifumo hiyo hiyo yaweza kuwageukia na nyie pia.
 
Wakiambiwe rekebisheni mifumo mkiwa na vyeo mnaona haiwahusu ila inawahusu Chadema,sasa yanawakumba,na bado hata sheria hizi za uchaguzi hata wao zitawaliza tu,Sasahivi si wanaona haziwahusu
 
"Wangapi mlienda kwenye mkutano soko kuu? mlisikia maneno aliyoyapiga mke wangu? baada ya pale walienda kumsimamisha kazi na sasa yupo nyumbani ana amani kabisa na yupo tayari akiambiwa achague kazi au mume wake atachagua mume wake. Wanasema hana vigezo tukaulizana vigezo hana baada ya kuongea jukwaani? miaka mitatu yote alikuwa navyo sasa hivi ndiyo avikose?

"Hata kama unataka kugombea njoo kwa utaratibu usinyanyase watu, kuna mjumbe mmoja wa kamati ya siasa anaitwa Asia alikuwa yupo Arumeru eti kwa sababu anakwenda ziara za mbunge wamemuamisha wamempeleka Ngorongoro lakini mpaka leo yupo Imara amebaki na msimamo wake ule ule kwa sababu Ngorongoro sio mbinguni ni hapahapa duniani. Halafu haya ni mambo ya mpito tu tunakwenda kwenye kura za maoni zikiisha uchaguzi ukiisha, maisha yanaendelea"

Pia, Soma: Mrisho Gambo: Mimi na yeye nani ameumiza wengi?

- Mrisho Mashaka Gambo Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Juni 14, 2025 wakati akizungumza kwenye mkutano mkuu maalumu wa utekelezaji ilani ya CCM uliofanyika katika kata ya Olasiti Jijini Arusha.

VIDEO: Jambo TV
Vyuma vitaumana Insha-Allah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom