Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

MBUZI MWENYE BUSARA

Senior Member
Nov 24, 2019
143
151
Sasa nimeongea na mke wangu kuhusu nyumba ambayo nimejenga kwenye kiwanja chake kuhusu umiliki kwasababu yeye alitaka kuandika jina lake tena kwa siri. Nimemuuliza kwanza kwamba tangu tuoane hatujawahi kuongelea kuhusu hicho kiwanja chake.

Akanikumbusha kwamba wakati tunaoana mimi nilimshauri akiuze na ilituletea mtafaruku kweli. Na ni kweli nilisita sana kujenga kwenye kiwanja cha mke wangu kwasababu nilishaona ni mtu mpenda vyake na asiye na muda na vyangu ilihali tayari sisi ni mke na mume.

Na niwarudishe kidogo kilichonifanya nimuone wa tofauti kidogo baada ya kuhamia pale, siku moja mwisho wa mwezi nilienda kuitembelea familia. Asubuhi tukiwa mimi na watoto akaleta mada kwamba Joyce (siyo jina halisi) ambaye yeye ni shangazi kwa Joyce. Joyce ameniomba Jack (siyo jina halisi) yaani mtoto wa Joyce aje aishi hapa na aende shule akikaa kwetu.

Sasa Joyce tuliwahi kukaa naye kama ndugu yake mke wangu, akawa anatusaidia kazi lakini alikuja kuondoka kwa ugomvi na mke wangu. Aliponipa hizo stori akili yangu iliyafanya mrejeo haraka sana nikakumbuka jinsi Joyce alivyoondoka kwa shangazi yake kwa maneno.

Nikamwambia mke hilo kwasasa haitawezekana na sababu niliyompa ni kwamba mtoto wetu kwasasa anasoma 'English Medium' halafu huyu Jack akija aende shule ya kawaida (serikali) mimi sitajisikia vizuri na haitakuwa sawa hata kwa tafsiri za watu wengi.

Nikamshauri kwamba, kama ni kwa ajili ya kwenda shule basi aende kwa shemeji (kaka yake mke) ambaye kimsingi yupo karibu na shule hiyo ya serikali na ni baba mdogo wake Joyce. Mke wangu alikuja juu sana na kuzua ugomvi kidogo nimpige.

Lakini maneno yaliyonikera sana ni kwamba, mimi siwataki ndugu zake na huwa nakuja hapa kuleta vurugu na kwamba anajuta kuolewa na mimi na akakimbilia nje. Baadaye nilimuita, akaja tukaongea, nikaamua kutulia ili nione maisha yanaendaje baada ya pale.

Na hapa wiki moja kabla alinijulisha swala la kuwekewa 'bcone' kwenye like eneo, kwamba inahitahijika 100,000 akanipa na ukomo wa muda, sikutaka maneno nikampa ile hela akalipa. Niliporudi akanionesha risiti, nikamwambia wafuatilie waweke.

Wiki inayofuata akanitaarifu kwamba wameshaweka 'bcone' lakini wanahitaji paspoti saba kwa maandalizi ya hati nikamwambia sawa. Nilipoenda nikamwambia ebu nenda idara ya maji ukaulizie utaratibu wa kupata maji kwa bomba binafsi, yaani kufungiwa mita ya maji kwenye hiyo nyumba.

Alienda baadaye akaniambia wanahitaji tujaze fomu na paspoti mbili, na fomu hurusiwi kuchukua unajazia kule idara ya maji, nikamwambia sawa. Jioni akaniambia kesho nataka nikapige zile picha ajaze hizo fomu na kupeleka zile picha saba kwa ajili ya hati, mimi nikaitikia sawa.

Asubuhi kulipokucha nikamwambia simamisha hilo zoezi hadi nije. Lakini nilimpigia simu jamaa yangu ambaye naye amejaza hiyo fomu, nikamuulizi hivi hizi fomu hurusiwi kutokana nazo ukajazie nyumbani? Jamaa akasema mbona mimi nilijazie nyumbani nikarudisha?!

Nikamwambia sawa, mimi nilikuwa naendelea kukusanya taarifa zangu. Jana nikafanya ziara ya kustukiza, nikafika nyumba lakini nikiwa njiani niliandika ujumbe kumjulia hali yeye na watoto nikamwambia nipo njiani nakuja huko.

Basi nikafika yeye alikuwa ametoka na watoto, nikafungua nikaingia nikampigia akasema anakuja na kweli wakawasili na watoto, watoto wangu wananipenda sana wakafurahi stori mbili tatu.

Mimi sikutaka kikao kichukue muda, nikaanza kikao na yeye nikamwambia mimi nimekuja kwa mazungumzo na wewe, akastuka sana. Nikamwambia mazungumzo ni ya kawaida ya kifamilia. Tukaongea nikamwambia hiki kiwanja si unajua ni chako, akasema ndiyo.

Nikamwambia lakini bahati nzuri tumejaliwa kujenga nyumba ya familia, akasema ndiyo. Nikamwambia kuna vitu tusipoviweka sawa huko mbeleni vitatuletea shida, akashangaa. Nikamwambia kwasasa tunaelekea kwenye swala la umiliki sasa tuamue mimi na wewe mmliki wa nyumba ya familia yetu kwenye kiwanja chako kitakuwa na umiliki wa nani? Hana jibu!

Nikamuuliza je maji na hilo suala la picha za hati mmiliki ungeandika? Akasema mimi nilijua ni vitu vya kawaida wala sikufikiria yote hayo! Nikamuuliza kwa mkuu wa familia ni nani akasema ni wewe (mimi). Nikamuuliza sasa mbona siku ile ulifanya tu kunipa taarifa tu unataka kwenda kupiga picha bila kuuliza tuandike jina la nani? Akasema mimi niliona hata nikiandika jina langu ni sawa tu na kwasababu nilikupa taarifa niliona hakuna shida.

Nikamwambia sasa mimi natambua kwamba kiwanja ni chako lakini nimejenga nyumba ya familia yangu ambayo ni sisi sote. Nimekuja tupate mwafaka wa hicho kiwanja na mimi nipo kwa ajili kuidhamini familia yangu na katika hii familia tunaojielewa kwasasa ni mimi na wewe vijana wetu bado wadogo.

Nikamwambia mimi nina majibu yangu lakini nahitaji majibu yako juu ya kiwanja hiki. Nikamkumbusha, kwamba siku ile ulivyoongea maneno ya kwamba mimi huwa nakuja kukuletea vurugu na kwamba unajuta kuolewa na mimi nilizingatia na hivyo sitakubaki kuiweka rehani familia kwa kuruhusu mambo yaende kiholela.

Akahamaki na kudai kwanini namkumbusha mambo ya zamani, nikamwambia haikuwa sehemu ya mada lakini nimeona nikukumbushe ili ujirekebishe kimawazo, kauli na kimtazamo na ufahamu mipaka yake kama mke. Akasema yale alitamka kwa hasira kwasababu ulinikemea mbele ya watoto n.k, nikamwambia mimi uliniletea mada yako mbele ya watoto na nilipopinga wewe ndiyo ukaleta ugomvi.

Akasema tuyamalize kwanza haya ndiyo tuje swala la umiliki wa nyumba. Ila nikamwambia mimi siwezi tena kukuruhusu kumiliki hii nyumba kwasababu hustahili, utashindwa kuzuia hisia zako na utaendelea kuropoka zaidi na huenda hata kuna siku utamleta mwanaume humu na sitaweza kuzuia. Naye akasema na wewe unaweza kumleta mwanamke halafu unitoe mimi.

Mwisho akasema nimpe muda atafakari swala la umiliki wa hii nyumba halafu atanipa jibu kwamba hawezi kupata jibu la haraka. Lakini nimemwambia mimi ndiye nina wajibu na jukumu la kulinda, kuhifadhi na kutunza mali za familia hivyo yeye ni mtu wa pili kutoka kwangu na akaona ugumu nipo tayari kumpa pesa yenye thamani ya kiwanja chake, yeye atajua atazifanyaje hizo hela lakini kiwanja kiwe chini ya familia na chini yangu kama mwenyewe dhamana ya familia namba moja.

Kwa hiyo namsubiri aamue halafu nami nitaweka msimamo wa kiti. Japo sasa amenuna lakini mgonjwa haulizwi dawa. Mimi kiukweli sina mpango B ya hilo, nahitaji heshima iwepo kwangu kama mwenye nyumba na siwezi kuwa mtalii kwenye familia yangu. Lazima kiti kiheshimiwe bila hivyo panya watatawala.

Naomba kuwasilisha kwa ajili yenu kujifunza na kutoa ushauri.

Asanteni.

Pia soma: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
 
Mkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia. Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja.

Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.

2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa.

Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje. Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
 
Unafanya swala la muhimu kabisa, hasa katika kutunza familia yako. Watu wengi wanaweza wasielewe kitu unachokipambania, kwa kua kiwanja ni cha mkeo lakini, mi nakushauri endelea kupambania haki ya familia yako, wanawake wanaongozwaga na hisia, sio akili unaweza kumuamini akaandika jina lake baadae akaja kuleta mwanaume.

Alafu pia, inatakiwa mwanamke ajue nafasi yake kama mwanamke na awe na UTII, ndoa bila UTII haitafika popote.
 
Mkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia.
Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja. Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.
2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa. Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje.
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
Katapishwe ulicholishwa mkuu
 
Mkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia.
Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja. Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.
2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa. Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje.
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
Unampa mamlaka mwanamke!?, Akikupiga tukio, baadae utaleta Uzi huku tukusaidie .

Yaani kumuandikisha mwanamke umiliki wa Nyumba, especially unayoishi wewe mwanaume na watoto wako, ni sawa na Kumsomesha mwanamke kwa kutegemea kumuoa, Lolote linaweza kutokea na ukabaki mdomo wazi.
 
Nilivyosoma stori aisee, nimependa namna unavyoweka wazi majibu ya mke, umepata mke mwenye hekima sana, ana majibu yenye busara na upole.

Nikirudi kwako, embu rahisisha tu mambo. Mwache aandike kwa jina lake maana hata kiwanja ni chake, yaan ukiona MTU anakwambia ngoja nikajifikirie ujue bado hajaafiki, watoto analea mama pale ,wewe unakuja Mara mojamoja, kwann usimwamini mkeo, mbona kama umekaa attention sana.

Hata mkiachana kwa ajili ya watoto bado itakubidi uwaachie Nyumba(kwa mwanaume Mwenye akili hawez taka watoto wataabike pa kuishi), ulisema una kiwanja kama ulivyosema wewe ni mwanaume ,kichwa cha familia em pambana tena jenga kwenye kiwanja chako then waandike wanao.

Usitumie ubabe, tafadhali mwachie tu kama zawadi hiyo Nyumba. Ni mkeo huyo analea na kuishi hapo na watoto wako.(usipojiangalia, ndoa yako ndo inaenda kufall apart Mkuu)
 
Ukishaona mnagombea umiliki wa nyumba huku mmeoana ujue ndoa inaelekea pabaya, akikataa umiliki wa pamoja mwachie tuu, anza kujenga yako na weka clear ni yako 100% na unafanya hivyo kwa sababu ya alichofanya nyumba ya kwanza, hakikisha unajenga nzuri kuliko yake, sounds utoto lakini dawa ya moto ni moto na kisheria wote mtashindwa mtaishia kugawana nusu kwa nusu tuu
 
Mkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia.
Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja. Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.
2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa. Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje.
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
Nakwambia kwa uzoefu kama unaamua mke wako kila.kitu uandike kwa jina lake umejiroga.bora ungeandika kwa majina ya watoto.

Kama una hela tafuta na mali zako za siri lakini usisahau ilitokea la kutokea mnagawana pasu.

Aisee ndoa ni majanga.
 
Nilivyosoma stori aisee,nimependa namna unavyoweka waz majibu ya mke...umepata mke mwenye hekima sana...ana majibu yenye busara na upole....nikirudi kwako....embu rahisisha tu mambo... Mwache aandike kwa jina lake maana hata kiwanja ni chake....yaan ukiona MTU anakwambia ngoja nikajifikirie ujue bado hajaafiki....watoto analea mama pale ,wewe unakuja Mara mojamoja,kwann usimwamini mkeo...mbona kama umekaa attention sana...hata mkiachana kwa ajili ya watoto bado itakubidi uwaachie Nyumba(kwa mwanaume Mwenye akili hawez taka watoto wataabike pa kuishi)....ulisema una kiwanja...kama ulivyosema wewe ni mwanaume ,kichwa cha familia...em pambana tena jenga kwenye kiwanja chako then waandike wanao...Usitumie ubabe,tafadhali...mwachie tu kama zawadi hiyo Nyumba.... Ni mkeo huyo analea na kuishi hapo na watoto wako.(usipojiangalia,ndoa yako ndo inaenda kufall apart Mkuu)
Haha.. wewe unajiona unamjua mke wake kuliko yeye anawfikia kufanya maamuzi ya kijasiri km haya?

Huoni alimdanganya kuhusu kujaza fomu nyumbani?

Mzes wangu aliwahi niambia "ikitokea umeoa kijana wangu kumbuka kwamba mkeo sio ndugu yako"
 
Haha.. wewe unajiona unamjua mke wake kuliko yeye anawfikia kufanya maamuzi ya kijasiri km haya?

Huoni alimdanganya kuhusu kujaza fomu nyumbani?

Mzes wangu aliwahi niambia "ikitokea umeoa kijana wangu kumbuka kwamba mkeo sio ndugu yako"
Hata mume siyo ndugu ila sasa mmejenga kwa ajili ya watoto...kwann mfarakane kwa vitu vya kupita mkuu
 
Unampa mamlaka mwanamke!?, Akikupiga tukio, baadae utaleta Uzi huku tukusaidie
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
.

Yaani kumuandikisha mwanamke umiliki wa Nyumba, especially unayoishi wewe mwanaume na watoto wako, ni sawa na Kumsomesha mwanamke kwa kutegemea kumuoa, Lolote linaweza kutokea na ukabaki mdomo wazi

Unampa mamlaka mwanamke!?, Akikupiga tukio, baadae utaleta Uzi huku tukusaidie .

Yaani kumuandikisha mwanamke umiliki wa Nyumba, especially unayoishi wewe mwanaume na watoto wako, ni sawa na Kumsomesha mwanamke kwa kutegemea kumuoa, Lolote linaweza kutokea na ukabaki mdomo wazi.
Mkuu, kama ni mtu wa kupiga matukio, atakupiga ukimpa umiliki au hata usipompa umiliki.
 
Mkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia.
Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja. Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.
2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa. Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje.
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
ni sahihi kabisa,mama hawezi watupa watoto wajanja huandika umiliki wa watoto,ama unaweza kuandika umiliki wa mme na mke
 
ushauri wa bure kwa wengine unapooa na kukuta mwenzio ana umiliki wa kiwanja ama nini kitu cha kwanza mkubaliane kubadili umiliki,ni juzi jamaa alipewa kiwanja kama zawadi siku ya ndoa kutoka kwa mama mkwe badae wakajenga kwenye kiwanja ambacho kina umiliki wa mama mkwe,juzi jamaa kaambiwa afungashe virago mama anataka nyumba yake
 
To yeye dada angu unaongea kana kwamba haujsoma mtiririko wa hii story. Kuna mapishano makubwa sana baina ya hawa wawili. Na navyoona mimi mke wa mwandishi ana majibu flani ivi. Sasa sitaki kumhukumu huyu mleta mada kama ni perfect au la...anajua yeye

Mama yangu aliwahi kuniambia...mwanangu hizi ardhi hatuend nazo popote. Ushawah kunisikia nikihangaikia..sina huo muda. Nitazikwa kwenye kasehemu kadogo sana. Hata kama una kiwanja ni chako..ilimradi umepata mwenza mkaelewana..usiwe mtu mbinafsi na kila mara kutaka kama kucompete. Sanasana utachoweza fanya andika majina ya watoto wenu isiwe tabu. Lakini mali hizi zinatafutwa. Katu usiondoe utu wako kisa hivi vitu vya duniani hapa. Utaviacha tu.

Kila mtu ana namna yake lakin mkishaanza hiki changu, hiki chako akati mmekuwa pamoja muda mrefu kuna shida pahala. Na kati yenu kuna tension sana ni basi tu mleta mada una hekima sana kama baba. Heshima kwako bro!

Its not a matter of competition.. its a matter of togetherness and unity towards the better life and future. I sence evilness baina yenu. Basi muitafute hekima ya muumba wenu afu msolve matatizo yenu. Shetani hapendi familia, na msipoangalia mtaja jenga ukuta baadae...lakin hatuombei hilo. Seek more wisdom..follow it. Something is so wrong.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom