Kwa mda mrefu nilikuwa nasikia habari za hazina ya mjerumani lakini mara nyingi nimekuwa mgumu wa kuamini habari hizo kwa kuona ni moja ya mradi wa wapiga wa mjini a.k.a borntown` lakini hili swala nimeshuhudia kwa macho yangu na kwa mara ya kwanza mkoani tabora wilaya ya sikonge sehemu inayoitwa masiki, kuna mzee mmoja nilikutana nae akawa anasimulia habari hizo kuhusu sehemu ambapo kumewekwa bunduki tatu ambazo zimefungwa kwenye nyaya huku zinaning'inia zikichungulia tundu la kuingilia ndani ya pango, na juu ya pango upande wa kuingilia nje kumeandika 1914.
Sehemu yenyewe ni Tabora wilaya ya Sikonge sehemu inaitwa Masiki.
Nimefika na nimeona hayo![/QUOTE
Hizi ni habari za kufikirika tu na hazina ukweli wowote. wengi wamefilisika kutokana na hii ishu. Ukiingia jiandae kuwalipa watu wa kuchimba, waganga wa kutoa mashetani kwenye "hazina". Na ki ukweli hakuna aliyewahi kufanikiwa. rejea ile story ya rupia ya mwaka .... eti ukiipata we ni milionea. Poor tanzanian nawaonea huruma wenye mawazo ya aina hii.