Mrejesho: Graduates with knowledge in IP/Networking wanahitajika

Lingine swala sio la kuibiwa tu, ninapofanya maombi ya kazi huwa natumia akili na muda. Hizi ni resources ambazo ningeweza kuzitumia kwenye maswala mengine.

Mwisho usikariri kila anayeomba kazi hana kazi. Msalimie Mcharo.
 
Hapa umedai ulishaitwa kwenye interview.

Hapa unakataa huhusiani na hiyo kazi. Mbona hueleweki. Huyo rafiki yako ni muongo kama wewe. Tena nadhani huyo rafiki umemtengeneza sasa hivi kujitetea.
I stand on behalf of my friend ni kazi za kwel amini usiamin that is upon u bro ila this thing is true
 
Lingine swala sio la kuibiwa tu, ninapofanya maombi ya kazi huwa natumia akili na muda. Hizi ni resources ambazo ningeweza kuzitumia kwenye maswala mengine.

Mwisho usikariri kila anayeomba kazi hana kazi. Msalimie Mcharo.
Kumbe una kazi ndo maana unawavuruga wenzio psychological ili wasi apply? Duh it's not fear
 
Screenshot_2017-03-28-07-51-34.png
 
padre una mbwembwe wewe nadhani masister wanakukoma
Habari Wakuu wangu......

Sijui nianzie wapi tu.. Anyway!!

Kwanza nilikua nimepigwa BAN. Kuna utani mmoja JF Chit-Chat tulikua tunatongozana kilugha sasa nikazidisha makeke nikaandika matusi.... Hivo nilikua nje ya JF kwa week moja hivi..

Nimekuta watu mnasema maneno mengi kishenz....
Good People , Askari Muoga , Biobenga , thesym

Mnasema mimi nilikua nawazingua.. Mimi ni tapeli....
Kuna yeyote kati yenu anaweza kuleta ushahidi hapa kuwa aliombwa atoe hata senti 10 kwenye applications??
Aje hapa na ushahidi.....

Mnasema mimi sio Padri, bali ni muhuni tuu....
Naweza nikawa Padri ama sio kwa sababu JF wengi tunatumia Fake ID na wengi wanatumia Real ID.
Kuna mtu anaitwa General Galadudu .... je huyo ni mwanajeshi??
Kuna mtu anaitwa miss chagga ... je huyo ni mchaga???
Mambo ya username yasikubabaishe kuanza ku evaluate cheo / kazi ya mtu...

Kwanza mniwie radhi kwa ukimya na kutorejesha feedback kwa muda mlikoua mnatarajia.
Yote hii ni kwa sababu vijana tuna pambana na soko la ajira, kitaa pachungu asikwambie mtu.

Hivo kijana anapotuma maombi na kisha ghafla anaanza kuuliza
"bado hamjaita watu tu??"
Wala haishangazi. Ndio hali halisi. Sio kwangu sio kwenu.
Mimi kuna Application nilituma Kampuni moja ya Waholanzi (nilifanya nao intership), Oral interview nikafanya nikapita. Wakasema wataniita baada ya week moja, toka October 11, 2016 mpaka leo miezi mingapi hiyo???
Kila nikimpigia cm HR wao anasema Bado MD hajatoa Go ahead lakini nafasi bado ipo wazi hadi leo.
Hivo suala la ku apply kazi ni moja, na suala la kuitwa ni lingine kabisa.

Hivi ushawahi kusikia mtu yuko Over-qualified?? Yaani una vigezo kupitiliza, kampuni inaona bora tuchukue vijana wadogo tukawa train tukaanza nao from the scratch. Watakua na team player nzuri. Kuliko kumchukua mtu more experienced ambae atahitaji tumlipe mpunga mrefu sana kwa kazi ambayo hata fresh graduate anaweza adapt after short training.

Sasa Vijana wenzangu, Feedback iko namna hii:
Kazi yangu ilikua kupokea applications (CV za watu) na kwa kushirikiana na HR (ambae ni Mbongo mwenzangu) tulifanya screening ya CV 20 (out of 50+ applications). Zoezi hili limekamilika.
Kila aliyetuma CV nilikua nam reply kuwa nimepokea CV, na hakuna aliyeombwa pesa wala desa.

Kazi iliyobaki ni kwa management kuandaa interview panel + other processes na kuita watu kwa ajili ya oral interview.
Sasa mimi siwezi kuwafata na kuwa provoke kuwa:
"Kwanini hammuiti watu jamani mpaka sasa hivi, watu wanaulizia huko"
Nimefanya part yangu imebaki yao.

Nadhani watakua wana target trainers wamalize ongoing project moja SA, ili wakija moja kwa moja vijana waingie training (kampuni gani inajili watu leo halafu training waanze mwezi wa nane!!!)
Hivo vijana kuweni na subira... Msijifnge akili kuwa nime apply kazi pale nikipata.....!!!
wakati unasubiri majibu unaangalia na fursa zingine mahali kwingine pia....

Askari Muoga alishangaa kuniona naulizia mshahara wa watu wa IT kwenye nafasi za TPA zilizotangazwa na tume na utumishi..... Nikacheka sana.....................
Kuwa na kazi mahali, kusikufanye uache kuangalia na green pasture kwingine ndugu....

Waliokua wanauliza ofisi..... Hexatechnoway T LTD zipo masaki mwisho mkabala na zilipo ofisi za Humphrey Consultants (mambo ya kitalu na block number... site engineer mambo ya ofisi wapi na wapi).

Namaliza kwa kusema hivi:
Nina imani vijana mtaitwa (ingawa sio wote) but 20 out 50+ ni wengi (ingawa mwanzo demand ilikua ni vijana 6).
Sasa kama project zikiongezeka na vijana wakaonesha kuwa suitable mnaweza kuchukuliwa more than that initial figure.
Mimi siwezi kuwajulisha ambao mmekua shortlisted na ambao bado mpaka management ikae na kuita watu...
Sababu sina uhakika kama Demand inapungua ama kuongezeka.

Asanteni wakuu wangu... Niko Chalinze naitafuta kibamba taratibu.
 
Mcharo umemuona Biobenga, hujamuona pettymarcel aliyetaka kutuaminisha amefanya interview. Wewe unadai interview bado.

Mkuu nimesoma post yako iliyofanya upigwe ban, inasikitisha. Kwenye hili swala la kazi umekua makini kuandika vitu vya msingi lakini posts zako nyingine hazifai.

Jf hatufahamiani, tunakujudge kutokana posts zako, kwa hilo ujirekebishe mkuu.

Kuhusu kazi tuombe uzima, ukweli utajulikana tu.
 
Padri mcharo vipii??mbona kimya mkuu
Mkuu bado unamsubiri mcharo, nakushauri fanya mambo yako mengine.

Ningekua na nafasi ningeenda hapo masaki, Mcharo anapodai kuna ofisi zao lakini huo muda wa kupoteza sina.

Ninachojiuliza Mcharo ananufaika vipi na huu mchezo anaofanya; inaweza kuwa kuna information alikua anahitaji kwenye hizo applications au anatafuta kiki jf. Kwa kifupi ni mtu hatari anayependa kucheza na akili za watu.

Mcharo alidai alikwenda South Africa kwenye training, baada ya siku nne kasema yupo chalinze, akadai shortlisting mpka trainers warudi Dar wako S.A, sasa yeye alienda kufanya nini huko? Ina maana aliattend training ambayo hajui inaisha lini. Haiwezekani apewe jukumu la kurecruit watu halafu apewe information nusu nusu.

Baada ya muda akaja na sababu nyingne kuwa swala la kuita watu lipo nje ya uwezo wake, kalipeleka kwa senior management.

Wacha nimsubirie aje na stori yake nyingine.
 
Back
Top Bottom