Mrejesho: Amerudi analia

Mrejesho: Amerudi analia

wa ilula

Member
Joined
Jan 28, 2023
Posts
33
Reaction score
59
Heshima mbele kama tai Wana jamvi.
Kwa mnaokumbuka January 30 2023 nlileta Uzi unaozungumzia kuhusu Mimi kumwagwa na single mama.
Nimeona nilete mrejesho hapa wadau wanaweza kujifunza mawili matatu kutoka hapa.
Juzi jioni nkiwa nimetulia zangu Gheto mara simu ikaita, nikapokea na kuuliza nani mwenzangu maana namba ilikua ngeni ,akajitambulisha Mimi fulani.
Nikamchangamkia vizuri tuu na kuniuliza habari za masiku.
Basi akaniuliza kesho jioni utakuja na mda nahitaji kuonana na wewe apo kwako?
Fasta tuu nikamwambia Sina uhakika na ratiba yangu ila ntakujuza kama nikipata mda.Kweli Jana jioni mida ya saa Moja nikajisogeza mitaa flani ivi wanauza matunda, ni kasehemu flani kana eneo tulivu .Nikampigia na kumwelekeza aje nilipo,sikutaka aje kwangu Ili kuepuka mitego ya hapa na pale.
Basi akaja eneo nilipo baada ya stori mbili tatu akaja kwenye main reason Kwa Nini ameomba tuonane...
Basi bwana akaniuliza ivi Mimi nimekukosea Nini ? Nikamuuliza kivipi akajibu naona hunitafuti ,hupigi simu Wala hunitumii sms. Nikamuuliza Kwani wewe uliwahi nipigia simu au kuntumia sms?
Akaanza kuleta maneno kibao unajua Mimi nliamua kukaa kimya baada ya kuona wewe hunitafuti nikaona niendelee na maisha yangu.Nikampiga swali Kwa iyo Leo kipi kimekusukuma ukanitafuta?
Akadai kwamba eti mazoea ndio yanamtesa amegundua hawezi kuishi bila Mimi
Baada ya blaa blaa za apa na pale nikamchana live kwamba asiniletee uchuro aendelee na maisha yake tubaki tuu kua marafiki maana hatuwezi kua wapenzi Tena.
Basi akaanza kujiliza pale nikamwacha apo apo nikaondoka zangu.
Baada ya kufika home nikakutana na meseji ndefu mithiri ya gazeti anaomba nimsamehe sana Alidanganyika , Mara anajichanganya kwao walikua wanamsema Kwa Nini ana bwana mkristo na yeye ni mwislamu ,nikaishia tuu kushangaa maana Mimi sijawahi hata kufika kwao
Ikabidi tuu nimchane kwamba Mimi na yeye hatuwezi kua wapenzi Tena na asikanyage apa kwangu.
Vijana wenzangu nawa asa kuweni makini sana na Mapenzi ya siku izi nlichojifunza wanawake wengi (sio wote) kwenye mahusiano anaagalia kipato chako zaidi.Tutafute Hela wanaume.
Na huu ndo mrejesho wangu kwenu wa aliekua shemeji yenu.
POVU RUKSA....
 
FB_IMG_16770484289622108.jpg
 
'Hawezi kuishi bila ya wewe' plus vimachozi flani hivi ili kunogesha.Kwenye mapenzi kuna maneno matamu!!hapo akili yako ndio inayotafutwa ili ifanye maamuzi sahihi...
 
'Hawezi kuishi bila ya wewe' plus vimachozi flani hivi ili kunogesha.Kwenye mapenzi kuna maneno matamu!!hapo akili yako ndio inayotafutwa ili ifanye maamuzi sahihi...
Kweli mkuu,Kuna kitu nimejifunza Jana,migogoro kama hii haitakiwi kutatuliwa ghetto maana Kwa jinsi alivokua anajiliza tungekua geto ningeishia kumpasua
 
Back
Top Bottom