Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,915
- 30,259
Baada ya matatizo yaliyoniandama katika vitabu hivyo viwili nilivyoandika siku moja mwaka wa 2008 nikapokea email kutoka kwa Prof. Emmanuel Akyeampong kutoka Harvard akaniomba niwe mmoja wa waandishi karibu 500 kutoka kila pembe ya dunia watakaoandika kamusi ya watu mashuhuru Afrika.
Mradi huu ulikuwa unajulikana kama Dictionary of African Biography.
Huu ulikuwa mradi wa Harvard na Oxford University Press New York.
Prof. Akyeampong akaniomba pia niwe mshauri wake kwa majina ya Watanzania ambao mimi naona wamefanya makubwa kwa hiyo wanastahili maisha yao kuandikwa katika hii kamusi.
Prof. Akyeampong akaniomba mimi niandike maisha ya Kleist Sykes yeye akimkusudia Kleist Abdulwahid Sykes.
Mimi hapo hapo nikaanza kazi yangu ya ushauri.
Nikalikata jina la Mayor wa Jiji la Dar es Salaam rafiki na ndugu yangu Kleist, nikamshauri Prof. Akyeampong kuwa anaestahili kuingia katika DAB ni babu yake, Kleist Sykes Mbuwane (1894 - 1949) na si huyu Kleist mtoto wa Abdul Sykes.
Prof. Akyeampong alivutiwa sana na kile alichosoma kuhusu babu yake Kleist Abdulwahid na kamusi ilipochapwa mwaka wa 2011 maisha ya Kleist Sykes Mbuwane babu yake Kleist Abdulwahid yakawa ndani ya DAB.
DAB ina volume sita na ni maarufu hivi sasa duniani kama kitabu vya rejea kwa watu mashuhuri na mashujaa wa Bara la Afrika.
Mradi huu ulikuwa unajulikana kama Dictionary of African Biography.
Huu ulikuwa mradi wa Harvard na Oxford University Press New York.
Prof. Akyeampong akaniomba pia niwe mshauri wake kwa majina ya Watanzania ambao mimi naona wamefanya makubwa kwa hiyo wanastahili maisha yao kuandikwa katika hii kamusi.
Prof. Akyeampong akaniomba mimi niandike maisha ya Kleist Sykes yeye akimkusudia Kleist Abdulwahid Sykes.
Mimi hapo hapo nikaanza kazi yangu ya ushauri.
Nikalikata jina la Mayor wa Jiji la Dar es Salaam rafiki na ndugu yangu Kleist, nikamshauri Prof. Akyeampong kuwa anaestahili kuingia katika DAB ni babu yake, Kleist Sykes Mbuwane (1894 - 1949) na si huyu Kleist mtoto wa Abdul Sykes.
Prof. Akyeampong alivutiwa sana na kile alichosoma kuhusu babu yake Kleist Abdulwahid na kamusi ilipochapwa mwaka wa 2011 maisha ya Kleist Sykes Mbuwane babu yake Kleist Abdulwahid yakawa ndani ya DAB.
DAB ina volume sita na ni maarufu hivi sasa duniani kama kitabu vya rejea kwa watu mashuhuri na mashujaa wa Bara la Afrika.