MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 19,373
- 40,178
Natumaini mko poa. Binafsi nashindwa kuelewa nini kimewapata CHADEMA kiasi kwamba kwenye vyombo vya habari hawasikiki kabisa kwenye mambo nyeti ya kitaifa. Angalau wiki hii wamekuja na ishu ya kuagiza Helikopta.
Kiujumla kuna uwezekano mkubwa Mh. Mpina akawa anavuma sana kama mpinzani aliye ndani ya CCM kuliko wanaojiita wapinzani huko CHADEMA. Kwa siku za hivi karibuni Mpina amesikika zaidi kwa hoja zake dhidi ya serikali hivyo kujikuta anatokea sana kwenye vyombo vya habari. Kisiasa ni muhimu sana kupata publicity kwa namna yoyote ile. Mwanasiasa unatakiwa uongelewe kila siku.
Pamoja na kwamba CHADEMA kina wabunge 20 ndani ya bunge la Tanzania ambapo mmoja ni wa kuchaguliwa na 19 ni wa viti maalum lakini bado CHADEMA kama imepooza pamoja na kuwa wa wabunge 20 huko Dodoma. Ni wakati sasa kina Mdee, Bulaya, Hawa Bananga, Nusrat Hanje na wenzao kuibua hoja zitakazokifufua chama chao CHADEMA kwenye siasa za bunge.
Kiujumla kuna uwezekano mkubwa Mh. Mpina akawa anavuma sana kama mpinzani aliye ndani ya CCM kuliko wanaojiita wapinzani huko CHADEMA. Kwa siku za hivi karibuni Mpina amesikika zaidi kwa hoja zake dhidi ya serikali hivyo kujikuta anatokea sana kwenye vyombo vya habari. Kisiasa ni muhimu sana kupata publicity kwa namna yoyote ile. Mwanasiasa unatakiwa uongelewe kila siku.
Pamoja na kwamba CHADEMA kina wabunge 20 ndani ya bunge la Tanzania ambapo mmoja ni wa kuchaguliwa na 19 ni wa viti maalum lakini bado CHADEMA kama imepooza pamoja na kuwa wa wabunge 20 huko Dodoma. Ni wakati sasa kina Mdee, Bulaya, Hawa Bananga, Nusrat Hanje na wenzao kuibua hoja zitakazokifufua chama chao CHADEMA kwenye siasa za bunge.