Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Mwanachama wa ACT Wazalendo, Luhaga Mpina amesema matamanio yake makuu ni kuona anaruhusiwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuonesha utofauti wa kampeni baina ya vyama vingine na kutimiza kusudio lake la kuongoza nchi baada ya kushinda uchaguzi, akibainisha kuwa Taifa linahitaji viongozi wa aina yake.
Ameyasema hayo leo Oktoba 06, 2025 nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania (Masjala Kuu Dodoma) mara baada ya kusikilizwa kwa Shauri la Kikatiba Na. 24027 la mwaka 2025, analopinga kuondolewa kugombea nafasi hiyo dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Ameyasema hayo leo Oktoba 06, 2025 nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania (Masjala Kuu Dodoma) mara baada ya kusikilizwa kwa Shauri la Kikatiba Na. 24027 la mwaka 2025, analopinga kuondolewa kugombea nafasi hiyo dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.