PreGE2025 Mpina ataka wenyeviti wa vitongoji warejeshewe Mihuri

PreGE2025 Mpina ataka wenyeviti wa vitongoji warejeshewe Mihuri

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Stuka

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
314
Reaction score
950
MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, ameitaka serikali kuwarejeshea wenyeviti wa vitongoji mihuri yao iliyondolewa kwa madai yasiyo na msingi.

Akizungumza leo Aprili 23 bungeni jijini Dodoma wakati wa mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Mpina amesema hatua hiyo imepunguza mamlaka ya viongozi wa msingi wa serikali.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

“Sababu ya kuondolewa mihuri kwa wenyeviti wa vitongoji haina msingi. Kama hoja ni kuuza ardhi, basi hata watumishi wa wizara wanauza viwanja mara mbili, lakini hatujawahi kuwavua mamlaka yao,” amesema Mpina.

Amesisitiza kuwa mihuri ni nyenzo muhimu kwa viongozi hao katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku, hivyo Serikali inapaswa kuirejesha kwao ili waendelee kutoa huduma kwa ufanisi.
 
Hii mbona ni mpya? Sasa haya mamlaka ya vitongoji yanasimamiwa na nani? CCM ni wahalifu sana. Serikali imepata wapi mamlaka ya kuondoa mamlaka ya vitongoji?
 
Hii mbona ni mpya? Sasa haya mamlaka ya vitongoji yanasimamiwa na nani? CCM ni wahalifu sana. Serikali imepata wapi mamlaka ya kuondoa mamlaka ya vitongoji?
Mkuu, hili mbona lilitekelezeka tangu 2022 kama sikosei, sio jipya.

Hivyo M/kiti wa kitongoji kwasasa hana mamlaka katika kuidhinisha nyaraka yoyote inayomuhusisha zaidi ya saini yake tu na mhuri wa WEO.
 
Mkuu, hili mbona lilitekelezeka tangu 2022 kama sikosei, sio jipya.

Hivyo M/kiti wa kitongoji kwasasa hana mamlaka katika kuidhinisha nyaraka yoyote inayomuhusisha zaidi ya saini yake tu na mhuri wa WEO.
Huu ni ukiukwaji mkubwa sana wa Sheria za serikali za mitaa.
 
MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, ameitaka serikali kuwarejeshea wenyeviti wa vitongoji mihuri yao iliyondolewa kwa madai yasiyo na msingi.

Akizungumza leo Aprili 23 bungeni jijini Dodoma wakati wa mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Mpina amesema hatua hiyo imepunguza mamlaka ya viongozi wa msingi wa serikali.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

“Sababu ya kuondolewa mihuri kwa wenyeviti wa vitongoji haina msingi. Kama hoja ni kuuza ardhi, basi hata watumishi wa wizara wanauza viwanja mara mbili, lakini hatujawahi kuwavua mamlaka yao,” amesema Mpina.

Amesisitiza kuwa mihuri ni nyenzo muhimu kwa viongozi hao katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku, hivyo Serikali inapaswa kuirejesha kwao ili waendelee kutoa huduma kwa ufanisi.
Hapa Dar es Salaam, walikabidhiwa since January
 
Hapa Dar es Salaam, walikabidhiwa since January
Muhuri wa serikali ya mtaa hauna maana wala effect yeyote katika mauzo ya ardhi .
Mwentekiti wa kitongoji pia hana mamlaka wala hatakiwi kuwa na muhuri kabisa kwa sababu serikali za vijiji ni corporate na mwenyekiti na mtendaji (Katibu) wa vijiji ndiyo wana mihuri.

Kwa hiyo kusema eti mwenyekiti wa kitongoji arejeshewe mihuri inaonyesha jinsi wabunge ambao ni watunga sheria, hawazijui sheria walizopitisha.
Str8 up rubber stamp legislator talking "rubb(ish)er stamps.
 
Muhuri wa serikali ya mtaa hauna maana wala effect yeyote katika mauzo ya ardhi .
Mwentekiti wa kitongoji pia hana mamlaka wala hatakiwi kuwa na muhuri kabisa kwa sababu serikali za vijiji ni corporate na mwenyekiti na mtendaji (Katibu) wa vijiji ndiyo wana mihuri.

Kwa hiyo kusema eti mwenyekiti wa kitongoji arejeshewe mihuri inaonyesha jinsi wabunge ambao ni watunga sheria, hawazijui sheria walizopitisha.
Str8 up rubber stamp legislator talking "rubb(ish)er stamps.
Ndugu, Hapa mjini usipo wapa wanajiona hawakustahili hata kugombea.
Wanatumia nguvu kubwa kugombea ili wapate mhuri then..........wanaanza kuvimbiana na watendaji
 
Back
Top Bottom