Mpenzi wangu anataka nimkopeshe laki 8

Mpenzi wangu anataka nimkopeshe laki 8

Inategemea na uhusiano wenu upoje hata kama haujaelekea ndoa au uchumba.Inategemea na huyo mpenzio yupoje kwani wewe ndo unamjua vizuri.Mimi nimewahi kukopeshana na my bf sana tu na tulikuwa tunarudishiana bila ugomvi na mpaka tunaachana nlikuwa namdai na alinilipa.Hivo hapo inategemea mtu akiwa mrushi hata ungekuwa umemtolea mahari atakutapeli tu.Ukiona anafaa kupewa na atarudisha mpe otherwise mwambie huna

aiseee nikopeshe na mimi basi
 
Hongera mkuu kama shemeji kapona. Anataka kufanya biashara au ni mwendelezo wake wa kudeka!
 
Mambo vipi wakuu,

Kama heading inaavyojieleza je nikifanya hivo nitakua nakosea?

Na je anaweza kunirudishia kweli au ndo changa la macho afu aingie mitini?

Kama unazo mpe tu ila kama huna mwambie ukweli kuwa huna . Pia kama unampa usimkopesha na kama ikitokea ukamkopesha muulize atalipa kwa utaratibu gani maana kila mkopo lazima uwe na payment plan. Me na mamaa tunakopana vizuri na tunalipana kwani ni ngumu mpenzi wako awe na shida akakope kwingine wakati wewe ndie mtu wake wa karibu na una uwezo wa kumkopesha. Mapenzi ni kusaidiana na kuokoa jahazi kipindi kigumu kama alichonacho mpenzi wako
 
laki 8? wanawake sio wa kuwaamini kabisa usithubutu kumpa laki 8.. demu wangu alinikopa elfu 10 hadi leo hajanirudishia

Hahahahahahaaaaaa elf kumi tu unalalama ingekuwa m je????
 
Kama una kipato na huyo ndiye mtu sahihi kwako basi mpatie tu aridhike,mwambie dia chukua laki 850 zikufae katika mambo yako..Atakupendajeee!!!
 
Jmn hakukopiii mbona uelewiii... Anamaanisha umlipe kiinua mgongo ya hizo laki 8.

aisee you made my day kwa kweli .. ts tru wapo ambao wakiona mapenzi hayana maisha yataisha siku si nyingi anajifanya anakupenda sana anaukoleza moto wa mapenzi anakukopa kibunda then anapita hivi .. ndo kashachukua kiinua mgongo chake! dah dunia hadaa ....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom