Mpeleke kayumba, watakutana Chuoni

Mpeleke kayumba, watakutana Chuoni

Mrs Gudman

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2015
Posts
613
Reaction score
1,300
Habari zenu wadau, kwa wale ambao hamjui mnapataje ada hadi sasa hivi poleni sana

Usimpeleke mtoto shule yenye ada kubwaaa ambayo unaona kabisa haiendani na kipato chako eti kisa tu watoto wa staff wenzio wote wako shule hizo.

Au majirani watakuchukuliaje, kila mtu anakujua wewe ni msomi mwenye kazi yake sehemu flani so unaona ukimpeleka st. Kayumba unajishushia hadhi,

Pole sana maana unaishi kuridhisha watu, maamuzi na uhalisia wa kipato chako unakijua wewe, una limkopo kama lote benki, wakati huo huo loan board nao wanakukata, kodi ya nyumba, mara gari inataka service na mafuta bila kuangalia ndugu wanakutegemea, acha kuchosha akili hebu mpeleke tu shule ya kawaida hakikisha unamfatilia vizuri anapata muda wa kujisomea vizuri mbona sisi tulipita huko huko na bado tukapass?


#Asubuhi njema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo kuna ombwe kubwa kati ya hizi shule za kanumba na hizo shule za kishua na hilo ombwe linazidi kukua kila siku, wakati wa zamani kidogo 80s mpaka early 90s kwenda shule za private mara nyingi iliashiria kuwa umefeli na umeshindwa kuingia katika shule bora za serikali, tatizo hapa kati elimu iliingiliwa na siasa na kupelekea shule nyingi za serikali kutoa bora elimu na si elimu bora.
Tatizo lingine linalokuja, kwa taratibu za maisha hasa wale wanaokaa mjini, ni ngumu sana kumfuatilia mtoto kiundani masomo yake, hasa pale wazazi wote wanapokuwa wanafanya kazi maofisini, unaondoka kabla watoto hawajaamka unarudi wakati wamelala. Hapo ndio unaweza kukuta mtoto anapotea kabisa, cha msingi ni kujipiga tu mpaka uwezo wako unapoishia basi na kumpeleka shule bora.
 
Kuna wengine wanasomeshwa shule za gharama sana ila wanatoka vichwa maji
Mimi nitajitahidi apate elimu bora itakayomjenga kuelewa maisha na dunia na sio elimu ya kukariri ili awe wa kwanza darasani

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli kabisa nimekutana na watu chuo kikuu wanajua tu kingereza kizuri ila kichwani empty set kabisa, ila kuna watoto wa maskini wamesoma kata wapo very bright, dah unajiuliza angepata nafasi ya kusoma huko sijui angekuwaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo kuna ombwe kubwa kati ya hizi shule za kanumba na hizo shule za kishua na hilo ombwe linazidi kukua kila siku, wakati wa zamani kidogo 80s mpaka early 90s kwenda shule za private mara nyingi iliashiria kuwa umefeli na umeshindwa kuingia katika shule bora za serikali, tatizo hapa kati elimu iliingiliwa na siasa na kupelekea shule nyingi za serikali kutoa bora elimu na si elimu bora.
Tatizo lingine linalokuja, kwa taratibu za maisha hasa wale wanaokaa mjini, ni ngumu sana kumfuatilia mtoto kiundani masomo yake, hasa pale wazazi wote wanapokuwa wanafanya kazi maofisini, unaondoka kabla watoto hawajaamka unarudi wakati wamelala. Hapo ndio unaweza kukuta mtoto anapotea kabisa, cha msingi ni kujipiga tu mpaka uwezo wako unapoishia basi na kumpeleka shule bora.
Hii historia ni ya kweli, lakini bado kuna shule chache za serikali zinajaribu kidogo,

Kikubwa na wewe mzazi naye aweke efforts zake kwa mwanae si kuachia tu walimu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wengine wanasomeshwa shule za gharama sana ila wanatoka vichwa maji
Mimi nitajitahidi apate elimu bora itakayomjenga kuelewa maisha na dunia na sio elimu ya kukariri ili awe wa kwanza darasani

Sent using Jamii Forums mobile app
Anaetoka na div 0 shule ya private, siyo sawa kiakili na yule anaetoka na div 3 shule ya serikali...
 
Wizara ya Elimu HAMTIMIZI majukumu yenu. ya kuzisimamia hizi shule za Binafsi. na suala hili litatugharimu baadae. Hivi kweli wizara ya Elimu mmnasemaje suala la mtoto wa Chekechea kuingia darasani SAA 1.30 asubuhi afu atoke SAA 10 JIONI ?? tunapojidanganya ni kudhani Elimu ni kusoma makaratasi tu. ninapomtuma mtoto sehemu au kazi ni Elimu, anapocheza ni Eimu, anapoona mambo pale mtaani ni Elimu. mimi nine elimu kubwa tu ,Mmeacha kuzisimamia shule hizi za binafsi sasa ni HOLELA TU !
wao wanaangalia kwamba ili tuhalalishe ADA KUBWA mtoto akae muda mrefu shuleni , hilo watu wa wizara ya Elimu hamjaligundua. SASA HUYU MTOTO ANAYESHINDA SHULENI KUANZIA SAA MOJA ASUBUHI MPAKA SAA 10 JIONI TOKA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 4, SIKU AKIKOSA AJIRA ATAJITEGEMEA KWELI ? wizara ya Elimu embu Timizeni Wajibu wenu !
 
Wizara ya Elimu HAMTIMIZI majukumu yenu. ya kuzisimamia hizi shule za Binafsi. na suala hili litatugharimu baadae. Hivi kweli wizara ya Elimu mmnasemaje suala la mtoto wa Chekechea kuingia darasani SAA 1.30 asubuhi afu atoke SAA 10 JIONI ?? tunapojidanganya ni kudhani Elimu ni kusoma makaratasi tu. ninapomtuma mtoto sehemu au kazi ni Elimu, anapocheza ni Eimu, anapoona mambo pale mtaani ni Elimu. mimi nine elimu kubwa tu ,Mmeacha kuzisimamia shule hizi za binafsi sasa ni HOLELA TU !
wao wanaangalia kwamba ili tuhalalishe ADA KUBWA mtoto akae muda mrefu shuleni , hilo watu wa wizara ya Elimu hamjaligundua. SASA HUYU MTOTO ANAYESHINDA SHULENI KUANZIA SAA MOJA ASUBUHI MPAKA SAA 10 JIONI TOKA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 4, SIKU AKIKOSA AJIRA ATAJITEGEMEA KWELI ? wizara ya Elimu embu Timizeni Wajibu wenu !
Huyu mtoto mdogo sijui anasoma nn, yaan elimu inaanza kuwapotezea mda watoto wakiwa bado wadogo. Kabla ya wizara ila wazazi pia tubadilike mwngne kwavile anashnda kazin anaona n bora mtoto kushinda kutwa nzima shuleni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa nimekutana na watu chuo kikuu wanajua tu kingereza kizuri ila kichwani empty set kabisa, ila kuna watoto wa maskini wamesoma kata wapo very bright, dah unajiuliza angepata nafasi ya kusoma huko sijui angekuwaje

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha uongo! vyuho vikuu hudahili kwa vigezo, kuna pointi lazima uzifikie ndo update admission.

hao vilaza walifikaje chuo?? Bila kuwa na vigezo??
Labda vyuo vyenu vya Kata,

next time usiandike habari za vijiweni kwenye majukwaa ya GT
 
Nimependa heading asee, "... kuwa watakutana Chuoni'

Serious kote huku chini mtakuwa separate kayumba na international flani but huko juu kama ni hapa hapa bongo 'tunakutana chuoni'
 
Acha uongo! vyuho vikuu hudahili kwa vigezo, kuna pointi lazima uzifikie ndo update admission.

hao vilaza walifikaje chuo?? Bila kuwa na vigezo??
Labda vyuo vyenu vya Kata,

next time usiandike habari za vijiweni kwenye majukwaa ya GT
Hahah wewe acha kupanic kuna watu wana A, s tupu kwenye vyeti ila kwenye real life hawajui kitu, hana uwezo wa kutetea hata hizo A zake, naona una mtazamo finyu kuwa akili ni kuwa na division one pole



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom