Mpango mchafu: Wanafunzi wa vyuo vikuu Dar kutopiga kura!

Mpango mchafu: Wanafunzi wa vyuo vikuu Dar kutopiga kura!

Twilumba

Platinum Member
Joined
Dec 5, 2010
Posts
13,610
Reaction score
16,545
SOMA MPANGO HUU MCHAFU DHIDI YA WANAFUNZI WA VYUO VYA ELIMU YA JUU VYA DSM

Nitasema tu bila kuogopa chochote. Katika uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura unaoendelea sasa sidhani kama tume imeangalia suala hili kwa umakini.

Uchaguzi wa mwaka 2010 wanafunzi wengi walikosa haki yao ya msingi ya kupiga kura kutokana na muingiliano wa ratiba kati ya eneo la kujiandikisha, tarehe ya kupiga kura na ratiba ya vyuo. Nilidhani mwaka huu tume italiangalia hilo ila naona kuwa limepuuzwa.

Ikiwa imebaki siku moja kabla ya wakazi wa Dar Es Salaam kuanza kujiandikisha ukweli ni kwamba wanafunzi wengi wa vyuo vikuu vilivyopo jijini hapo watakosa haki hii kwani asilimia zaidi ya 90 ya vyuo hivyo vimefungwa wiki 2 zilizopita.

Zoezi la uandikishaji kwa jiji la DSM limekuwa likisogezwa sogezwa mbele bila sababu zozote za kimsingi, nadhani upo mpango maalum wa kuwakwamisha wanafunzi kupiga kura katika uchaguzi mkuu 2015 kwani wanafunzi hao kwasasa wameenda mikoani ambapo tayari zoezi hilo lilishafanyika.

Jiulize wanafunzi hao watajiandikisha wapi maana wameenda likizo mikoani kwao ambapo zoezi lilishafanyika na watakaporudi Dar Es Salaam watakuta zoezi pia limeshafanyika, watakuwa wageni wa nani?

Ombi langu kwa tume ya uandikishaji kuwa kama wanahitaji kila mtu apate haki hii ya msingi basi ni vizuri wakaliangalia hilo na uandikishwaji huo ukarudiwa tena katika vituo maalum hasa vyuoni mara baada ya vyuo kufungiliwa ili kila mtanzania apate haki yake.

Ahsante,

Michael Litanda,

Safari ya matumaini, Inaendelea.....
 
Nikisoma hiyo article na hali ya zoezi lilivyokwenda naona kabisa kuwa hii ikikuwa strategically maana walianza Mkoa mpya wa njombe ambao nadhani una tawi la chuo cha SAUT tu kama sikosei ambao wanafunzi sidhani kama wanafika hata 1,000. Tume wanafanya hivi kwa kufuata maelekezo kutoka serikali ya CCM

Tulipigie kelele hili!
Kupiga kura ni haki ya kila mmoja wetu.
 
Jamani jamani tume chonde chonde.................................................
 
Haitawasaidia sana maana wanafunzi wengi huwa hawaondoki hapa dar. Wanafunzo wanapashwa kuona umuhimu wa kujiandikisha na kuwa wajanja kama nyoka. Mwaka huu ni mwaka wa vita kama mtu andhani ni lelema hatapiga kura ni mwaka wa kujitoa lasivyo inakula kwako. Wanawajua wapinzani wao vizuri hivyo na nyinyi mnapashwa kumjua adui yenu na hila zake zote. Jitoleeni hata kutumia kubumu chenu kusubiria uandikishaji kesho mkimaliza mnasafiri mikoani.
 
Acheni ubishooo pigen kura n haki yako
Mtaishia kulia lia n mikopo ya chai na pilipil
 
Haitawasaidia sana maana wanafunzi wengi huwa hawaondoki hapa dar. Wanafunzo wanapashwa kuona umuhimu wa kujiandikisha na kuwa wajanja kama nyoka. Mwaka huu ni mwaka wa vita kama mtu andhani ni lelema hatapiga kura ni mwaka wa kujitoa lasivyo inakula kwako. Wanawajua wapinzani wao vizuri hivyo na nyinyi mnapashwa kumjua adui yenu na hila zake zote. Jitoleeni hata kutumia kubumu chenu kusubiria uandikishaji kesho mkimaliza mnasafiri mikoani.

unabaki dar kujiandikisha uchague mbunge atakayeleta maendeleo dar na huko kwenu vijijini anakuchagulia nani? ukimaliza chuo unabaki dar unapata kazi dar, wadogo zako wanakuja kujazana sebuleni kwako mama ako anahamia dar kwa kijana wake badae unaanza kulalamikia serikali kumbe ni ujinga wako wa tangu utotoni.
 
mimi sioni tatizo sana,hizi kura zipo tu,watapiga kura wakimaliza masomo,haraka ya nini?,
2020 si mbali kivile,wavute subira....
 
Twilumba

Kulalamika hakutoshi. Ni wakati wa kuchukua hatua.

Kwa level ya chuo, mwanafunzi anatakiwa awe sehemu ya solution ya matatizo yanayomkabili (kwamba ni matatizo ya kupanga ama la).

Kama 2010 mazingira hayakuwezesha wanafunzi kupiga kura (kwa bahati mbaya au kwa makusudi), na mazingira ya sasa yanataka kufanana na yale, amueni kuingia gharama kidogo kwa kujiandikisha kulingana na ratiba iliyotolewa na NEC.

Hakuna mafanikio yasiyokuwa na gharama. Kama unataka viongozi wazuri hakikisha unajiandikisha na unapiga kura.

Kumbukeni mustakabali wenu huko chuoni kwa miaka mingine mitano inategemea sana aina ya viongozi watakochaguliwa Oktoba. Na pia, kuondoa madhaifu kama haya kwenye tume ya uchaguzi, ni vyema kuchagua viongozi watakaokuwa na maono hayo.

Nje ya hapo jiandaeni kulalamika tena 2020!
 
Last edited by a moderator:
mimi sioni tatizo sana,hizi kura zipo tu,watapiga kura wakimaliza masomo,haraka ya nini?,
2020 si mbali kivile,wavute subira....

Kwa viongozi hawa wa serikali ya CCM miaka 5 ni mingi mnoooo!
 
Haitawasaidia sana maana wanafunzi wengi huwa hawaondoki hapa dar. Wanafunzo wanapashwa kuona umuhimu wa kujiandikisha na kuwa wajanja kama nyoka. Mwaka huu ni mwaka wa vita kama mtu andhani ni lelema hatapiga kura ni mwaka wa kujitoa lasivyo inakula kwako. Wanawajua wapinzani wao vizuri hivyo na nyinyi mnapashwa kumjua adui yenu na hila zake zote. Jitoleeni hata kutumia kubumu chenu kusubiria uandikishaji kesho mkimaliza mnasafiri mikoani.

Hivi hijui kunawengine walitakiwa kuripoti field one week baada ya kufunga je nao wangweza kusubiri zoezi la uandikishaji
 
Back
Top Bottom