SERIKALI imeweka bayana mkakati mpya wa muda mfupi na mrefu utakaosaidia kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kumaliza kikao na viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alisema barabara za Morogoro na Ali Hassan Mwinyi, zitagawanywa ili kupunguza msongamano nyakati za asubuhi na jioni.
Lowassa, alisema nyakati hizo magari katika Barabara ya Morogoro yatakayokuja mjini, yatatumia barabara tatu na moja itatumika kwa magari yanayotoka katikati ya mjini kwenda nje ya mji, na kuongeza kuwa utaratibu huo utafanyika pia kwenye Barabara ya Alli Hassan Mwinyi.
.....
Serikali ilikurupuka kutekeleza mpango huu....
Tatizo la kwanza kabisa ni makutano ya barabara zetu....ndipo inafuatia na barabara zenyewe.....na ilishindikana kutumia njia tatu kwenye makutano.
La msingi, wakati wenzetu Kenya wanamalizia 'fly overs' zao jijini Nairobi, sisi bado tunapiga porojo za alinacha..