Mpaka sasa sijaona mgombea urais mwenye sifa hata nusu tu ya zile za Rais Magufuli

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,635
7,005
Ili nchi zetu hizi maskini zisonge mbele,zinahitaji aina ya viongozi wenye maamuzi magumu yanayozingatia uhalisia wa mazingira tuliyo nayo na si kukopi maamuzi kwa kuangalia wakoloni wetu wanafanyaje.

Changamoto pekee ambayo naona Rais wa sasa hajaigusa,ni eneo la elimu.
Alichofanya pekee ni kumwaga pesa za elimu bure na mikopo ya vyuo vikuu bila kijiuliza hiyo elimu unayowekeza pesa hizo ni elimu gani!

Kwa sasa anatakiwa rais ambaye atakuja kufumua kabisa mfumo huu wa elimu unaozalisha watu wajinga wengi wenye vyeti vikubwa.

Inahitaji aina fulani ya ukichaa kubadili mambo.

Kuna watu wanajiita maprofesa na madaktari wenye mawazo mgando sana.

Kwa maoni yangu,mambo yafuatayo ni ya kuangalia upya:

1. Elimu ya msingi -kwa nini miaka saba,nini wanajifunza huko?Yana msaada gani katika jamii yetu ya sasa kama mtu anaweza kumaliza shule asione umuhimu wa kutochafua mazingira yake mwenyewe?

2. Elimu ya sekondari kwa nini miaka sita?Kwa nini miaka miwili ya advanced certificate?Wanasoma nini katika elimu ya sekondari?Je miaka minne mbona ina mambo machache ambayo ni kama kupoteza muda tu iwapo mtu anaweza kuyasoma miaka miwili?

3. Elimu ya vyuo vya kati.Mitaala ni halisi ama ni ya kibabaishaji tu?Kwa nini haisaidii nchi kuzalisha bidhaa zinazotumika sana kwenye mazingira yetu?Vinaitwa Technical Institutions ni ufundi upi?Je unakidhi kweli?Kwa nini hakuna ubunifu kama ilivyo nchi kama china?

4. Elimu ya vyuo vikuu.Je lengo lake ni nini iwapo tunaona wahitimu wengi hawana mwelekeo na wasomi wanapigana vikumbo kwenye siasa tu?
Wangapi wanasoma mambo meengi sana ambayo hawayafanyii kazi hadi wanakufa?Kuna haja ya kulazimisha kusoma kila kitu kwa ajili tu ya kupata ugumu wa kupata degree?Au ni muhimu kusoma vitu ili kusaidia akili iweze kuwa na ubunifu?Leo nikisikiliza kipindi cha njiapanda,nimesikia mhitimu wa udom aliyesoma memkwa hadi kupata degree yake ya ualimu eti hakumbuki kirefu cha memkwa!

5. Malipo ya mshahara,posho,marupu rupu lazima yawe makubwa kuliko kada nyingine yoyote ili kuvutia ushindani wa watu wenye akili kuingia kwenye kada hii.

6.Kuwekeza sana kwenye elimu ya IT kwa kiwango kinachoweza kuwashangaza wengi na kupuuza masomo yanayopoteza muda kama uraia,historia(ambayo ni feki) na kuyafanya kama vitabu vya hadithi tu,ila kwa mtu anayeomba kazi yanakuwa kama added advantage.Ama yanafundishwa jeshini tu k.v jkt

Nchi hii haitasonga kwa hizi elimu za kukariri na kuwaita wale wenye uwezo wa kukariri eti "wenye akili" na kupata vyeti na GPA nyingine za kuhonga ngono.
 
Mkuu huyu anae msifu kwa miaka yote mitano ametekeleza budget zake kwa wastani wa 34% Sasa hapo unaona Kuna kiongozi? Unemployment rate imeongezeka kuliko kipindi chochote Cha history ya nchi hii,mazingira ya biashara yamekuwa magumu,uchumi upo ICU mpaka anasubject watu kwenye corona ili apate pesa za mishahara,Sasa mtu wa namna hii hiyo sifa ya kuwa rais aliyonayo ni ipi Kama sisi si akili za kishirthole?
 
Mie huwa naona elimu yetu haina shida.....

Shida ni medium of communication.

Tunakariri kwasababu hatuelewi.... lugha ndiyo shida kubwa.

Kiingereza kianzie shule ya msingi....vyombo vya habari habari ziwe kwa kiingereza. Maofisini kitumike kiingereza.

Sisi hatutafaidika na mfumo. Kizazi cha wajukuu wetu.

Tukishindwa hilo basi tusome kwa kiswahili kuanzia shule ya msingi.
 
Nimegundua kuwa watu wanachanganya kati ya Uhuru wa Mawazo na Uharo wa mawazo.
Mada hii imeangukia kundi la pili
 
  • Thanks
Reactions: prs
Mkuu huyu anae msifu kwa miaka yote mitano ametekeleza budget zake kwa wastani wa 34% Sasa hapo unaona Kuna kiongozi? Unemployment rate imeongezeka kuliko kipindi chochote Cha history ya nchi hii,mazingira ya biashara yamekuwa magumu,uchumi upo ICU mpaka anasubject watu kwenye corona ili apate pesa za mishahara,Sasa mtu wa namna hii hiyo sifa ya kuwa rais aliyonayo ni ipi Kama sisi si akili za kishirthole?

Kwangu nadhani kila kiongozi alikuwa na mapungufu yake.

Amefanya vizuri baadhi ya mambo na kuna mambo ameharibu saana. Hata kwa JK rudi nyuma tulimsema kwa mengi saana...nchi iligeuka shamba la bibi.

Alichukulia ujiko mapungufu ya JK...siunajua ukisifiwa kukimbia unapapita kwako!!!!
 
Yaani wewe mkuu.ni.kama wale wabunge ikitolewa hoja anasimama anaichambuaaaaaaa anaeleza madhara yake weeeeeeeeee kisha anahitimisha anasema anaunga mkono hoja anakaa.

Umeeleza uozo mtupu hasa kwenye elimu (ambao yawezekana ni kweli) kisha kichwa cha habari jamaa ni bora kabisa! Hakuna anaemkaribia hata nusu!

Kwanini hukutumia hizo hoja zako kum disqualify? Katika miaka 5 kashindwa kuzifanyia kazi unasemaje yeye ni mgombea bora kabisa?
 
Mkuu huyu anae msifu kwa miaka yote mitano ametekeleza budget zake kwa wastani wa 34% Sasa hapo unaona Kuna kiongozi? Unemployment rate imeongezeka kuliko kipindi chochote Cha history ya nchi hii,mazingira ya biashara yamekuwa magumu,uchumi upo ICU mpaka anasubject watu kwenye corona ili apate pesa za mishahara,Sasa mtu wa namna hii hiyo sifa ya kuwa rais aliyonayo ni ipi Kama sisi si akili za kishirthole?
Nyie miaka mitano kwa wizi wa billion 8.9
 
Elimu ni tatizo kubwa mno.
Huwezi kuwekeza mabilioni kwenye elimu watu wanashindwa kutengeneza hata ethanol matokeo yake mnauziwa sanitizer kidogo tu kwa maelfu ya pesa.
Vijijini kuna watu walikimbia shule wanatengeneza gongo na kukamatwa kwa kumiliki mitambo ya kutengeneza kinywaji haram.
Leo nchi inaagiza ethanol China na India!
Mie huwa naona elimu yetu haina shida.....

Shida ni medium of communication.

Tunakariri kwasababu hatuelewi.... lugha ndiyo shida kubwa.

Kiingereza kianzie shule ya msingi....vyombo vya habari habari ziwe kwa kiingereza. Maofisini kitumike kiingereza.

Sisi hatutafaidika na mfumo. Kizazi cha wajukuu wetu.

Tukishindwa hilo basi tusome kwa kiswahili kuanzia shule ya msingi.
 
Rais si malaika.Kwa sehemu aliyofanya naamini siku akishitukia ujinga wa huku kwenye elimu atafanya kitu.

Wasi wasi wangu ni iwapo atawatumia wale wale maprofesa wake wa Chuo kikuu,lazima wataturudisha kule kule.
Yaani wewe mkuu.ni.kama wale wabunge ikitolewa hoja anasimama anaichambuaaaaaaa anaeleza madhara yake weeeeeeeeee kisha anahitimisha anasema anaunga mkono hoja anakaa.

Umeeleza uozo mtupu hasa kwenye elimu (ambao yawezekana ni kweli) kisha kichwa cha habari jamaa ni bora kabisa! Hakuna anaemkaribia hata nusu!

Kwanini hukutumia hizo hoja zako kum disqualify? Katika miaka 5 kashindwa kuzifanyia kazi unasemaje yeye ni mgombea bora kabisa?
 
Elimu ni tatizo kubwa mno.
Huwezi kuwekeza mabilioni kwenye elimu watu wanashindwa kutengeneza hata ethanol matokeo yake mnauziwa sanitizer kidogo tu kwa maelfu ya pesa.
Vijijini kuna watu walikimbia shule wanatengeneza gongo na kukamatwa kwa kumiliki mitambo ya kutengeneza kinywaji haram.
Leo nchi inaagiza ethanol China na India!
Hili si tatizo la Tanzania ni la bara zima na sio bara tu na mabara mengine.


Tulishahamishwa kwenye mfumo wa maisha yetu tukafanywa wategemezi wa kila kitu hadi namna ya kuishi.

Tunasubiri tuone wenzetu wanavyoishi kisha nasi tunaiga.

Hili ni tatizo ambalo haliwezi kuisha leo.
 
Kwangu nadhani kila kiongozi alikuwa na mapungufu yake.

Amefanya vizuri baadhi ya mambo na kuna mambo ameharibu saana. Hata kwa JK rudi nyuma tulimsema kwa mengi saana...nchi iligeuka shamba la bibi.

Alichukulia ujiko mapungufu ya JK...siunajua ukisifiwa kukimbia unapapita kwako!!!!
Mkuu nisaidie kujua angalau Jambo moja lililofanywa vizuri na Magufuli,maana Mimi siona hata moja naona utopolo tu everywhere
 
Ukikosa hoja utabaki na option moja tu ya kuchagua aina ya tusi linalokufurahisha akili yako maana huwezi kupigana humu
Nimegundua kuwa watu wanachanganya kati ya Uhuru wa Mawazo na Uharo wa mawazo.
Mada hii imeangukia kundi la pili
 
Back
Top Bottom