Elections 2010 Moto wa waka - finland (+358) kuhusishwa na sms za uchochezi

Mimi ninawasiwasi Chadema wanahusika na hiyo msg sidhani kama CCM wanaweza kufanya hivyo kwakuwa CCM ni chama kikongwe na wamekomaa kwenye siasa. Sisemi kama hawana mbinu za kisiasa lakini sio za namna hiyo.

Chadema ni chama kinachopigiwa kelele kwa maswala ya udini na ukoo ( watu wa familia moja kuongoza chama na kupeana ubunge wa viti maanlum ) pengine wameamua kutumia hii mbinu ili watu wahamishe mawazo yao kuwa chama hiki kina harufu ya udini.

Haya ni mawazo yangu binafsi maana sote tumeumbwa na akili zetu na sitegemei kwakuwa sipo na baadhi ya watu kwenye hili mkanichukia.\

Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.
Duhh! Sokomoko umenifurahisha kweli.... kwamba Chadema kinashutumiwa kuongozwa na watu wa ukoo umoja na udini sasa CCM kukoje?
Kikwete ni mwenyekiti, Salma ni mjumbe, Ridhiwan ni mjumbe, Mtoto wa miaka 10 ni mwenyekiti.... hii ni familia ya Kikwete in usultani siyo ukoo ndani ya CCM. Udini tuna Kikwete, Makamba, Kinana, Karume, Shein hao ni dini gani hivi??
Acha kuchafua hali ya hewa ..... sema maneno hayo kwa wajinga siyo kwa watanzania wenye elimu ya kati na ya juu kama watu wa JF.
 
Mtazamaji,

Ningelikuwa na namba yako ya simu, ningelituma ujumbe kwa watu na namba ikaonekana ni ya kwako.

Wakati huo huo, mimi mtumaji nakula Fufu hapa Kumasi, Ghana.

Sikonge Sio rahisi kihivyo mtu wangu .sababu kabla ya kuweza kutimia number yangu lazima nitumiwe ujumbe kuwa number yangu itakuwa inatumika kwenye komyuta.Kitaalamu wanasema handshake. Wananitumia code kwenye simu. then zile code za kwenye simu ndo unazitumia ku confirm kwenye website una uhusiano na ile number. sasa wewe utapataje code waati uliandika number yangu. code zitakuja kwangu. Bila mimi kukutumia code iliyotumwa kwenye number yangu hutaweza.

Haya matatizo yalikuwepo zamani lakini Wenzetu wameweka control. Tena kwa sababu ni number ya finland tracebality yake inakuw arahisi zaidi kuliko ingekuwa ya Afghanistan au tanzania. Wenzetu wana resources.
 
Hakuna haja ya kupoteza muda na msg hiyo kwa sababu nia yake inajulikana, na kwa mtu anayeelewa haiwezi kumtisha bali uamuzi ni wake. Kumtafuta aliyetuma hiyo msg ni kupoteza muda kwa sababu ni sera ya nchi husika kama Simcard inauzwa holela basi mtu anaweza kuinunua muda huo na kutuma msg then akaitupa. Ni wazi kuwa COUNTRY CODE haiwezi kubadiilika kwa sababu zinasimaiwa na ITU na hata kama ni SKYPE tena ndiyo rahisi kuipata zaidi. Lakini kwa nini tuhangaike na mambo ya kipuuzi badala ya mambo ya msingi?

Mimi naamini kuwa watanzania wa leo siyo wa miaka ya 95 wanajua nini wanakihitaji na nini hawataki. Mimi nawashauri wanasiasa na hata CCM waache demokrasia ichukue mkondo wake. Kama CCM inasema inakubalika basi waache fitina, mizengwe na vitisho kwani kama ni kweli wametekeleza mahitaji ya watanzania watachaguliwa tu. Lakini huu ujanja ujanja hauwezi kuwa wa kudumu. Na pale wanapoona wanashindwa wakubali kwa sababu nchi nyingi huwa zinakabiliwa na machafuko kwa sababu ya watawala hawataki kuondoka?. Labda kama nimesahau toka nianze kufuatilia siasa chanzo kikubwa cha vurugu ni vyama vinavyotawala.


Kuna shida ya msingi hapa hata wanosimamia vyombo vya usalama hawaamini kuwa kunaweza kukatokea mabadiliko ya ghafla ya utawala na wao lazima wawe tayari kwa lolote. CCM ni chama cha siasa kama vilivyo vingine tu, na ni sawa na watanzania wengine.


Mimi naendelea kuamini kwamba CCM wanabanwa na CHADEMA ndiyo maana maneno yamekuwa mengi lakini hizo ndiyo siasa. CCM kama nilivyowahi kusema kwenye maoni yan gu ya nyuma kuwa imejitakia yenyewe kwa kuacha misingi yake na kuingia katika kuwa chama cha watu wachache matajiri na hilo ndiyo tatizo kubwa.

Siamini kuwa Dr. Slaa anaweza akaleta miujiza sana lakini ana vision sahihi kwa maisha ya watanzania. Anazungumza matatizo ya watanzania na suluhisho la matatizo yake kwa upana na uelewa mkubwa.

Naomba nitoe ushauri tu pia kwa JF iachane na mambo ya Pools opinions kwa sasa, muelekeo unaonekana kinachofanyika sasa na ambacho ninafikiri hata CCM wanafikiria ni kuingilia hizi forum na kupiga kura za kupanga ili kutengeneza hali vizuri kama wamehangaika na REDET na Synovate watashindwa kuivamia usiku mmoja wakapiga kura elfu kumi?


" Kila mtu atavuna alichopanda".

 
Baada ya wadau wa technologia na TCRA kuhangaika kwa siku kadhaa, baathi ya wadau wamegundua kuwa number iliyotumika possibly niya Finland.

mchakato unaandaliwa kuwasiliana na network za finland kutatua tatizo hili.

asanteni wadua kwa kulivalia njuga. mmmh sasa watakoma....!!!

Tuhakikishie ukweli kwa ushahidi kwa uliyoandika hapa sasa hivi. Nyie mlioingia mwezi wa 10 mwaka 2010 mnazungusha sana maneno ya uongo hapa JF. Mnadhani sisi ni wajinga? Hatudanganyiki.
 
Title ya thread haiendani ni content yenyewe.

[COLOR="blue"]Mkuu umenena! lakini ningependa kutoa shule ndogo ya hii kitu:

Technologia ya SMS inatawaliwa na mambo mawili makuu:

1: Mobile Originated (MO)
2: Mobile Terminated (MT)

MO--> Hapa, SMS inatoka kwa mtumaji mwenye kutumia simu ya mkononi au Internet application kwenda kwenye SMS Center (SMSC) ya Mobile Network Operator (MNO) husika.

Kama ni Internet application lazima uwe umejiandikisha kwa third party SMS providers (mfano, Clickatel, Text nation) ambao wanamikataba ya kutumiana SMS na Mobile Network Operators. Na kutumia huduma hii sio lazima uwe kwenye nchi ambako huyo SMS provider ana mitambo yake.

Huyu SMS Provider anaweza kukupa namba yako binafsi au asikupe namba binafsi. Kwa hiyo basi SMS yako itakwenda kwanza kwenye SMS Gateway ya huyo provider wako (Hii ni kama SMSC na huwa inatambulika kwa namba au IP address) halafu ndio itakwenda kwenye SMSC ya MNO husika.


MT--> Hapa, SMS itatoka kwenye SMSC ya Mobile Network Operator husika kwenda kwa mtu aliyetumiwa hiyo SMS.

Kwa hiyo mara nyingi kama SMS imetumwa kwa kutumia Internet application namba inayoonekana sio namba ya mtumaji bali ni Gateway namba ya third party SMS provider.

TCRA wanauwezo wa kumtambua mtumaji wa hizo SMS chafu kwa kuwabana MNOs husika (Hawa wana mikataba na SMS providers). MNOs watamtaja SMS provider husika ambaye nayeye atamtaja mteja wake aliyetuma hizo SMS chafu. kawaida SMS providers wana mikataba ya huduma na wateja wao na SMS chafu huwa haziruhusiwi.

Roaming user: Kama mtumaji wa hizo SMS chafu ana-roam hii itakuwa rahisi sana kumtambua kwa sababu huwezi ku-roam kama MNOs husika hawana mkataba. hapa kuna daftari la wageni linaloitwa Visiting Location Register (VLR) kwa hiyo namba ya mgeni naye-roam lazima itambulike na MNO husika:/COLOR]
 
Back
Top Bottom